Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lff somo la 56 jambo kuu la 1-6
  • Dumisha Umoja Katika Kutaniko

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Dumisha Umoja Katika Kutaniko
  • Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • CHIMBA ZAIDI
  • MUHTASARI
  • CHUNGUZA ZAIDI
  • Kusitawisha Urafiki wa Karibu na Waabudu Wenzetu Ni Jambo Jema Kwetu!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2025
  • Msiwakwaze “Hawa Wadogo”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2021
  • ‘Endeleeni Kusameheana kwa Hiari’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Dumisheni Muungano Katika Siku Hizi za Mwisho
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
Pata Habari Zaidi
Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
lff somo la 56 jambo kuu la 1-6
Somo la 56. Dada wawili kutoka jamii tofauti wanasalimiana kwa furaha.

SOMO LA 56

Dumisha Umoja Katika Kutaniko

Makala Iliyochapishwa
Makala Iliyochapishwa
Makala Iliyochapishwa

Tunapokuwa pamoja na waabudu wenzetu, tunahisi kama Mfalme Daudi aliyesema hivi: “Jinsi ilivyo vema na jinsi inavyopendeza ndugu kukaa pamoja kwa umoja!” (Zaburi 133:1) Umoja wetu haujitokezi wenyewe. Kila mmoja wetu anachangia kudumisha umoja huo.

1. Watu wa Mungu wana jambo gani la pekee?

Unapohudhuria mkutano wa kutaniko katika nchi nyingine, huenda usielewe lugha inayozungumzwa, lakini utastarehe na kuhisi kwamba umekaribishwa. Kwa nini? Kwa sababu duniani pote tunajifunza Biblia kwa kutumia machapisho yaleyale. Na tunafanya yote tunayoweza ili kuonyeshana upendo. Hata iwe tunaishi wapi, sisi sote ‘tunaliitia jina la Yehova na kumwabudu kwa umoja.’​—Sefania 3:9, maelezo ya chini.

2. Unaweza kufanya nini ili kuchangia umoja?

“Pendaneni sana kutoka moyoni.” (1 Petro 1:22) Unawezaje kufuata ushauri huo? Badala ya kukazia fikira udhaifu wa wengine, kazia fikira sifa zao nzuri. Jitahidi kuwafahamu ndugu na dada wenye malezi mbalimbali badala ya kushirikiana tu na wale walio na mapendezi kama yako. Pia, tunapaswa kujitahidi kabisa kuondoa hisia zozote za ubaguzi ambazo huenda tunazo.​—Soma 1 Petro 2:17.a

3. Utafanya nini hali ya kutoelewana ikitokea kati yako na Mkristo mwenzako?

Ingawa tuna umoja, sisi si wakamilifu. Wakati fulani, tunaweza kuwavunja moyo waabudu wenzetu au kuwaumiza hisia. Kwa hiyo, Neno la Mungu linatuhimiza hivi: “Endeleeni . . . kusameheana,” kisha linaongeza hivi: “Kama vile Yehova alivyowasamehe kwa hiari, nanyi lazima mfanye vivyo hivyo.” (Soma Wakolosai 3:13.) Sisi humkosea Yehova mara nyingi sana, hata hivyo bado anatusamehe. Basi anataka tuwasamehe ndugu zetu. Ukigundua kwamba umemkosea mtu fulani, chukua hatua ya kwanza ili kusuluhisha tatizo hilo.​​—Soma Mathayo 5:​23, 24.b

CHIMBA ZAIDI

Chunguza njia unazoweza kuchangia umoja na amani katika kutaniko.

Picha: Ndugu akifanya amani. 1. Ndugu mwingine anazungumza naye kwa hasira. 2. Anafikiria mambo ambayo ndugu huyo alisema. 3. Anachunguza ushauri wa Biblia kuhusu jinsi anavyopaswa kutenda anapokosewa. 4. Anakutana na yule ndugu, wanakunywa kahawa pamoja na kufanya amani.

Utachukua hatua gani ili kufanya amani?

4. Epuka ubaguzi

Tunapaswa kuwapenda ndugu zetu wote. Lakini huenda ikawa vigumu kushirikiana na mtu ambaye tunamwona kuwa tofauti. Ni nini kitakachotusaidia? Soma Matendo 10:34, 35, kisha mzungumzie maswali haya:

  • Yehova anakubali watu wa kila aina wawe Mashahidi wake. Unawezaje kuwa na maoni kama ya Yehova kuhusu watu walio na malezi tofauti na yako?

  • Ni ubaguzi wa aina gani ulio katika eneo lenu ambao ungependa kuepuka?

Soma 2 Wakorintho 6:11-13, kisha mzungumzie swali hili:

  • Unawezaje kuimarisha upendo kati yako na ndugu na dada walio na malezi tofauti na yako?

5. Samehe kwa hiari na ufanye amani

Yehova hutusamehe kwa hiari ingawa yeye hahitaji kamwe sisi tumsamehe. Soma Zaburi 86:5, kisha mzungumzie maswali haya:

  • Yehova husamehe kwa njia kubwa jinsi gani?

  • Kwa nini unathamini msamaha wake?

  • Ni hali gani zinazoweza kusababisha kutoelewana kati yetu na watu wengine?

Tunawezaje kumwiga Yehova na kuendelea kushirikiana na ndugu na dada zetu kwa umoja? Soma Methali 19:11, kisha mzungumzie swali hili:

  • Mtu anapofanya jambo linalokuudhi au kukukasirisha, unaweza kufanya nini ili kusuluhisha hali hiyo?

Wakati fulani sisi huwakosea wengine. Unapaswa kufanya nini hilo linapotokea? Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie swali linalofuata.

VIDEO: Kufanya Amani Huleta Baraka (6:01)

  • Katika video hiyo, dada huyo alichukua hatua gani ili kufanya amani?

6. Kazia fikira sifa nzuri za ndugu na dada zako

Tunapozidi kuwafahamu ndugu na dada zetu, tunatambua sifa zao nzuri na pia udhaifu wao. Tunawezaje kukazia fikira sifa zao nzuri? Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie swali linalofuata.

VIDEO: Boresha Utu Wako wa Kikristo! (5:10)

  • Ni nini kinachoweza kukusaidia kuona sifa nzuri za ndugu na dada zako?

Yehova hukazia fikira sifa zetu nzuri. Soma 2 Mambo ya Nyakati 16:9a, kisha mzungumzie swali hili:

  • Unahisije kujua kwamba Yehova anakazia fikira sifa zako nzuri?

Pete ya almasi.

Hata almasi maridadi ina kasoro lakini bado ni yenye thamani. Vivyo hivyo, ndugu na dada zetu wote si wakamilifu, lakini ni wenye thamani mbele za Yehova

WATU FULANI HUSEMA: “Ili nimsamehe mtu, lazima kwanza aniombe msamaha.”

  • Kwa nini tunapaswa kuwa tayari kuwasamehe wengine?

MUHTASARI

Unaweza kudumisha umoja kutanikoni kwa kuwasamehe na kuwapenda ndugu na dada zako wote.

Ungejibuje?

  • Unawezaje kuepuka ubaguzi?

  • Utafanya nini hali ya kutoelewana ikitokea kati yako na Mkristo mwenzako?

  • Kwa nini unapaswa kuiga mfano wa Yehova wa kuwasamehe wengine?

Lengo

CHUNGUZA ZAIDI

Jifunze jinsi mfano ambao Yesu alitoa unavyoweza kutusaidia kuepuka kuwahukumu wengine.

Toa Boriti (7:01)

Je, tunahitaji kuomba msamaha hata ikiwa tunahisi kwamba hatujakosea?

“Kuomba Msamaha​—Ni Njia Bora ya Kufanya Amani” (Mnara wa Mlinzi, Novemba 1, 2002)

Ona jinsi wengine walivyojifunza kuacha kuwabagua wengine..

Usihukumu Kwa Sura ya Nje (5:06)

Jifunze jinsi ya kutatua hali ya kutoelewana kati yako na Mkristo mwenzako kabla haijavuruga amani kutanikoni.

“Suluhisha kwa Upendo Hali ya Kutoelewana” (Mnara wa Mlinzi, Mei 2016)

a Maelezo ya Ziada 6 yanazungumzia jinsi upendo unavyowachochea Wakristo waepuke kueneza magonjwa yanayoambukiza.

b Maelezo ya Ziada 7 yanazungumzia jinsi ya kusuluhisha matatizo ya kibiashara na kisheria.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki