Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwbr18 Agosti kur. 1-2
  • Marejeo ya Daftari la Huduma na Maisha

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Marejeo ya Daftari la Huduma na Maisha
  • Marejeo ya Daftari la Huduma na Maisha—2018
  • Vichwa vidogo
  • AGOSTI 6-12
  • AGOSTI 13-19
  • AGOSTI 20-26
  • AGOSTI 27–SEPTEMBA 2
Marejeo ya Daftari la Huduma na Maisha—2018
mwbr18 Agosti kur. 1-2

Marejeo ya Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha

AGOSTI 6-12

HAZINA ZA NENO LA MUNGU | LUKA 17-18

“Onyesheni Shukrani”

nwtsty habari za utafiti—Lu 17:12, 14

wanaume kumi wenye ukoma: Katika nyakati za Biblia, inaonekana kwamba watu wenye ukoma walikutana au waliishi katika vikundi, na hivyo wangeweza kusaidiana. (2Fa 7:3-5) Sheria ya Mungu ilisema watu wenye ukoma wanapaswa kuishi katika eneo lililotengwa. Pia, mtu mwenye ukoma alipaswa kuwatangazia wengine kutoka mbali akisema: “Mimi si safi, mimi si safi!” (Law 13:45, 46) Kupatana na Sheria, watu hao wenye ukoma walisimama mbali kutoka kwa Yesu.—Ona habari za utafiti—Mt 8:2 na Kamusi, “Ukoma; Mwenye ukoma.”

mkajionyeshe kwa makuhani: Yesu Kristo, akiwa chini ya Sheria alipokuwa hapa duniani, alitambua kwamba ukuhani wa Haruni ulikuwa bado unatenda, naye aliwaelekeza wale aliowaponya ukoma waende kwa kuhani. (Mt 8:4; Mk 1:44) Kulingana na Sheria ya Musa, kuhani alipaswa kuhakikisha kwamba mtu mwenye ukoma alikuwa ameponywa. Mtu huyo mwenye ukoma alihitaji kusafiri kwenda hekaluni na alienda akiwa na matoleo, au zawadi, za ndege safi wawili walio hai, tawi la mwerezi, kitambaa cha rangi nyekundu, na tawi la hisopo.—Law 14:2-32.

Kutafuta Hazina za Kiroho

nwtsty habari za utafiti—Lu 17:10

wasiofaa kitu: Tnn., “bure; wasio na thamani.” Kusudi la mfano wa Yesu halikuwa kwamba watumwa, yaani, wanafunzi wake, wajione kuwa bure au wasio na thamani. Kulingana na muktadha, maneno “wasiofaa kitu” yanatokeza wazo la watumwa walio na maoni yenye kiasi kujielekea, kwamba hawastahili sifa ya pekee. Wasomi fulani husema kwamba maneno hayo yanatumiwa hapo kwa njia iliyotiwa chumvi ili kumaanisha “sisi ni watumwa wasiostahili kukaziwa uangalifu wa pekee.”

nwtsty habari za utafiti—Lu 18:8

imani hii: Au “imani kama hii.” Tnn., “ile imani.” Katika Kigiriki neno “imani” linatanguliwa na kibainishi wazi kuonyesha kwamba Yesu hakuwa akizungumzia imani kwa ujumla, lakini imani fulani hususa, imani kama ya yule mjane katika mfano wa Yesu. (Lu 18:1-8) Hilo lingetia ndani kuwa na imani katika nguvu za sala kutia ndani imani kwamba Mungu atahakikisha kwamba haki inatekelezwa kwa watu wake waliochaguliwa. Yesu hakujibu swali hilo ili kuwafanya wanafunzi wake wafikirie ubora wa imani yao wenyewe. Mfano kuhusu sala na imani ulifaa kabisa kwa sababu Yesu alikuwa ametoka tu kufafanua majaribu ambayo wanafunzi wake wangekabili.—Lu 17:22-37.

AGOSTI 13-19

HAZINA ZA NENO LA MUNGU | LUKA 19-20

Kutafuta Hazina za Kiroho

nwtsty habari za utafiti—Lu 19:43

ngome yenye miti iliyochongoka: Neno la Kigiriki khaʹrax linapatikana hapa tu katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. Limefafanuliwa kuwa “mti au nguzo iliyochongoka iliyotumiwa kuweka uzio wa eneo fulani; mti” na pia umefafanuliwa kuwa “ukuta uliojengwa na jeshi kwa kutumia miti; ukuta.” Maneno ya Yesu yalitimia katika mwaka wa 70 W.K. wakati ambapo Waroma, wakiongozwa na Tito, walisimamisha ukuta kuzunguka Yerusalemu. Tito alikuwa na makusudi matatu ya kuujenga—kuwazuia Wayahudi wasitoroke, kuwalazimisha wasalimu amri, na kusababisha njaa ili wasalimu amri. Ili kupata vifaa vya kujenga ukuta huo kuzunguka Yerusalemu, askari Waroma walikata miti yote katika maeneo yaliyozunguka.

nwtsty habari za utafiti—Lu 20:38

kwa maana kwake, wote wako hai: Au “kwa maoni yake wote wako hai.” Biblia inaonyesha kwamba kwa maoni ya Mungu watu ambao wako hai lakini wametengwa na Mungu wamekufa. (Efe 2:1; 1Ti 5:6) Vivyo hivyo, kwa maoni ya Yehova watumishi wa Mungu wanaokufa wakiwa na kibali chake bado wako hai, kwa sababu kusudi lake la kuwafufua halitakosa kutimia.—Ro 4:16, 17.

AGOSTI 20-26

HAZINA ZA NENO LA MUNGU | LUKA 21-22

Kutafuta Hazina za Kiroho

nwtsty habari za utafiti—Lu 21:33

Mbingu na dunia zitapitilia mbali: Maandiko mengine yanaonyesha kwamba mbingu na dunia zitadumu milele. (Mwa 9:16; Zb 104:5; Mhu 1:4) Kwa hiyo, maneno ya Yesu hapa yanaweza kueleweka kuwa ya kutia chumvi, kumaanisha kwamba hata ikiwa jambo lisilowezekana lingetendeka, kama vile mbingu na dunia kupitilia mbali, maneno ya Yesu bado yangetimizwa. (Linganisha Mt 5:18.) Hata hivyo, huenda mbingu na dunia zinazotajwa hapa zikawa zinarejelea mbingu na dunia za mfano ambazo huitwa “mbingu ya kwanza na dunia ya kwanza” kwenye Ufu 21:1.

maneno yangu hayatapitilia mbali kamwe: Katika Kigiriki maneno mawili ya kukanusha yanatumiwa kupinga wazo fulani kwa mkazo, na hivyo kukazia kwamba maneno ya Yesu ni ya kudumu.

AGOSTI 27–SEPTEMBA 2

HAZINA ZA NENO LA MUNGU | LUKA 23-24

Kutafuta Hazina za Kiroho

nwtsty habari za utafiti—Lu 23:31

wakati mti ni mbichi, . . . utakapokauka: Inaonekana kwamba Yesu anarejelea taifa la Kiyahudi. Lilikuwa kama mti unaokufa ambao bado ulikuwa na unyevunyevu fulani ndani yake kwa sababu Yesu bado alikuwepo na pia Wayahudi kadhaa waliomwamini walikuwepo. Hata hivyo, baada ya muda mfupi Yesu angeuawa, na Wayahudi waaminifu wangetiwa mafuta kwa roho takatifu na kuwa sehemu ya Israeli wa kiroho. (Ro 2:28, 29; Gal 6:16) Wakati huo, taifa halisi la Israeli litakuwa limekufa kiroho, likifanana na mti uliokauka.—Mt 21:43.

nwtsty picha

Msumari Ndani ya Mfupa wa Kisigino

Hii ni picha ya umbo la mfupa wa kisigino cha mwanadamu uliopigiliwa msumari wenye urefu wa sentimita 11.5. Mfupa halisi wa kisigino cha mwanadamu ulipatikana mwaka wa 1968, uchimbuzi ulipofanywa katika eneo la kaskazini la Yerusalemu. Inakadiriwa kuwa mfupa huo ni wa enzi za Waroma. Huo ni uthibitisho wa kiakiolojia unaoonyesha kwamba labda misumari ilitumiwa kuwaning’iniza watu kwenye nguzo za mbao. Huenda msumari kama huo ulitumiwa na askari-jeshi Waroma kumpigilia Yesu Kristo kwenye mti. Kisigino hicho kilipatikana kwenye sanduku la mifupa lililotengenezwa kwa mawe ya chokaa (ossuary) ambalo lilitumiwa kuhifadhi mifupa ya mtu aliyekufa baada ya nyama kuoza. Hilo linaonyesha kwamba mtu aliyetundikwa mtini angeweza kuzikwa.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki