MAISHA YA MKRISTO
Mwige Yosefu—Ukimbie Uasherati
Yosefu anatuwekea mfano mzuri tunaposhawishiwa kufanya uasherati. Kila mara mke wa bwana wake alipojaribu kumshawishi, alikataa. (Mwa 39:7-10) Jibu lake: “Ninawezaje kufanya uovu huu mkubwa na kwa kweli nimtendee Mungu dhambi?” lilionyesha kwamba tayari alikuwa amefikiria maoni ya Yehova kuhusu uaminifu katika ndoa. Kisha hali ilipokuwa mbaya, alikimbia badala ya kukaa hapo na kumpa mwanamke huyo nafasi ya kulegeza msimamo wake.—Mwa 39:12; 1Ko 6:18.
TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA UKIMBIE UASHERATI, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:
Jin alikabili hali gani?
Jin alijiuliza swali gani muhimu Mee-Kyong alipomwomba amsaidie katika somo la hesabu?
Ombi la Mee-Kyong lilimwathirije Jin?
Jin alipata msaada gani?
Jin alifanya nini ili kuukimbia uasherati?
Umejifunza masomo gani kutokana na video hiyo?