HAZINA ZA NENO LA MUNGU | MWANZO 42-43
Yosefu Aonyesha Sifa ya Kujizuia
Je, unaweza kuwazia hisia ambazo Yosefu alikuwa nazo alipojikuta ghafla uso kwa uso na ndugu zake? Angeweza kujitambulisha moja kwa moja kisha awakumbatie au kulipiza kisasi. Lakini hakutenda bila kufikiri. Utafanya nini ukitendewa isivyo haki na watu wa familia au wengine? Mfano wa Yosefu unatufundisha faida za kujizuia na kuwa watulivu badala ya kufuata moyo wetu wenye hila na kutenda kupatana na hisia zetu zisizo kamilifu.
Unaweza kumwigaje Yosefu unapokabili hali mbalimbali?