Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwbr20 Agosti kur. 1-3
  • Marejeo ya Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Marejeo ya Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha
  • Marejeo ya Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha—2020
  • Vichwa vidogo
  • AGOSTI 3-9
  • AGOSTI 10-16
  • AGOSTI 17-23
  • AGOSTI 24-30
  • AGOSTI 31–SEPTEMBA 6
Marejeo ya Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha—2020
mwbr20 Agosti kur. 1-3

Marejeo ya Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha

AGOSTI 3-9

HAZINA ZA NENO LA MUNGU | KUTOKA 13-14

Kutafuta Hazina za Kiroho

it-1 1117

Barabara Kuu, Barabara

Tangu zamani barabara kuu na barabara nyingine, kutia ndani njia fulani muhimu za biashara, ziliunganisha majiji na falme katika eneo la Palestina. (Hes 20:17-19; 21:21, 22; 22:5, 21-23; Yos 2:22; Amu 21:19; 1Sa 6:9, 12; 13:17, 18; ona BARABARA YA MFALME.) Barabara kuu ilitoka Misri hadi majiji ya Wafilisti ya Gaza na Ashkeloni kisha ikapinda upande wa kaskazini mashariki kuelekea Megido. Ilielekea hadi Hazori, Kaskazini ya Bahari ya Galilaya, kisha ikaelekea Damasko. Barabara hiyo iliyopitia eneo la Ufilisti ndiyo iliyokuwa fupi zaidi kutoka Misri hadi Nchi ya Ahadi. Lakini kwa fadhili Yehova aliwaelekeza Waisraeli wapitie njia nyingine ili wasivunjike moyo wanaposhambuliwa na Wafilisti.—Kut 13:17.

it-1 782 ¶2-3

Kutoka

Ni sehemu gani ya Bahari Nyekundu iliyogawanywa ili Waisraeli wavuke?

Ni muhimu kutambua kwamba baada ya Waisraeli kufika Ethamu, “ukingoni mwa nyika” kwenye awamu ya pili ya safari yao, Mungu alimwamuru Musa kwamba anapaswa “kurudi na kupiga kambi mbele ya Pihahirothi.” Jambo hilo lingemfanya Farao aamini kwamba Waisraeli “wanatangatanga . . . kwa sababu wamechanganyikiwa.” (Kut 13:20; 14:1-3) Wasomi wanaosema kwamba njia waliyotumia ni ile ya el Haj wanasema kwamba kitenzi cha Kiebrania “kurudi” hakimaanishi tu “kubadili mkondo” au “kugeuka,” lakini kinatokeza wazo la kurudi ulikotoka. Wanadokeza kwamba walipofika mahali fulani Kaskazini kwenye Ghuba ya Suez, Waisraeli walirudi nyuma na kuzunguka upande wa Mashariki wa Jebel ʽAtaqah, ambayo ni safu ya milima inayofanyiza mpaka wa Magharibi wa Ghuba hiyo. Isingekuwa rahisi kwa kikundi kikubwa cha watu kama vile Waisraeli, kuondoka haraka kutoka eneo kama hilo ikiwa wangeshambuliwa kutoka Kaskazini, na hivyo wangezuiwa na bahari ili wasiondoke.

Mapokeo ya Wayahudi ya karne ya kwanza W.K. yanatokeza picha kama hiyo. (Ona PIHAHIROTHI.) Lakini, jambo muhimu zaidi ni kwamba maelezo hayo yanapatana na simulizi linalotajwa katika Biblia, ilhali maoni ya wasomi wengi hayapatani na maelezo hayo. (Kut 14:9-16) Inaonekana kwamba mahali ambapo Waisraeli walivukia palikuwa mbali sana na ukingo wa Ghuba hiyo (au ukingo wa magharibi wa Bahari Nyekundu) hivi kwamba majeshi ya Farao hayangeweza kuzunguka tu na kuwakamata Waisraeli upande ule mwingine wa bahari hiyo.—Kut 14:22, 23.

AGOSTI 10-16

HAZINA ZA NENO LA MUNGU | KUTOKA 15-16

“Msifu Yehova kwa Wimbo”

it-2 454 ¶1

Muziki

Inaonekana kwamba nyimbo nyingi zilizoimbwa katika Israeli ziliimbwa na vikundi viwili vilivyopokezana kuimba mistari ileile, au mtu mmoja aliimba na kwaya ikamjibu. Katika Maandiko mbinu hiyo inarejelewa kuwa ya ‘kuitikia.’ (Kut 15:21; 1Sa 18:6, 7) Mbinu hiyo ya uimbaji inaonekana kupitia njia ambayo zaburi fulani zimeandikwa, kama vile Zaburi 136. Ufafanuzi wa makundi mawili makubwa yaliyoimba nyimbo za shukrani katika siku za Nehemia na yaliyoimba pia wakati wa kuzinduliwa kwa ukuta wa Yerusalemu unadokeza kwamba walitumia mbinu hii ya uimbaji.—Ne 12:31, 38, 40-42; ona WIMBO.

it-2 698

Nabii wa Kike

Miriamu ndiye mwanamke wa kwanza kuitwa nabii katika Biblia. Ni wazi kwamba Mungu aliwasilisha ujumbe au jumbe kadhaa kupitia kwake, huenda kupitia nyimbo zilizoongozwa kwa roho. (Kut 15:20, 21) Hivyo, yeye na Haruni wanarekodiwa kuwa walimwambia Musa hivi: “Je, [Yehova] hajazungumza kupitia sisi pia?” (Hes 12:2) Yehova mwenyewe, kupitia nabii Mika, alisema kwamba aliwatuma “Musa, Haruni, na Miriamu” mbele ya Waisraeli alipokuwa akiwatoa Misri. (Mik 6:4) Ingawa Miriamu alipewa pendeleo la kutumiwa kuwasilisha ujumbe kutoka kwa Mungu, uhusiano wake na Mungu akiwa nabii ulikuwa mdogo kuliko ule wa Musa ndugu yake. Alipokosa kutambua mahali pake, aliadhibiwa vikali na Mungu.—Hes 12:1-15.

AGOSTI 17-23

HAZINA ZA NENO LA MUNGU | KUTOKA 17-18

Kutafuta Hazina za Kiroho

it-1 406

Vitabu vya Biblia Vinavyokubalika

Uthibitisho wa kwamba maandishi ya Musa yaliyotoka kwa Mungu, ni sehemu ya vitabu vinavyokubalika, yaliandikwa kwa roho ya Mungu, na yanafaa kutoa mwongozo kwa ajili ya ibada safi, unaonekana wazi tunapochunguza uthibitisho wa ndani. Musa hakujipendekeza kuwa kiongozi wa Waisraeli; mwanzoni Musa alijaribu kukataa wazo hilo. (Kut 3:10, 11; 4:10-14) Badala yake, Mungu alimwinua Musa na kumpa nguvu za kimuujiza hivi kwamba hata makuhani wachawi wa Farao walilazimika kukubali kwamba kile ambacho Musa alifanya kilitoka kwa Mungu. (Kut 4:1-9; 8:16-19) Kwa hiyo, Musa hakujitafutia cheo cha kuwa msemaji na mwandikaji. Badala yake, kwa sababu ya kutii amri ya Mungu na akiwa amewekwa rasmi na roho takatifu, Musa alichochewa kwanza kusema na kisha kuandika sehemu ya vitabu vya Biblia vinavyokubalika.—Kut 17:14.

AGOSTI 24-30

HAZINA ZA NENO LA MUNGU | KUTOKA 19-20

Kutafuta Hazina za Kiroho

it-2 687 ¶1-2

Kuhani

Ukuhani wa Kikristo. Yehova alikuwa ameahidi kwamba ikiwa taifa la Israeli lingedumisha agano alilofanya pamoja nao wangekuwa “ufalme wa makuhani na taifa takatifu.” (Kut 19:6) Hata hivyo, ukuhani wa ukoo wa Haruni ungeendelea tu hadi wakati ambapo ukuhani mkuu uliowakilishwa nao ungekuja. (Ebr 8:4, 5) Ungeendelea kuwepo mpaka wakati ambapo agano la Sheria lingekoma kutenda na wakati ambapo agano jipya lingeanza kutenda. (Ebr 7:11-14; 8:6, 7, 13) Mwaliko huo ulitolewa kwanza kwa Waisraeli peke yao, walioalikwa watumikie wakiwa makuhani wa Yehova chini ya mpango wa ufalme wa Mungu ulioahidiwa; baadaye mwaliko huo ulitolewa pia kwa wasio Wayahudi.—Mdo 10:34, 35; 15:14; Ro 10:21.

Ni Wayahudi wachache tu waliomkubali Yesu, kwa hiyo taifa hilo lilishindwa kutokeza ufalme halisi wa makuhani na taifa takatifu. (Ro 11:7, 20) Kwa sababu ya ukosefu wa uaminifu wa taifa la Israeli, Mungu alikuwa amewaonya karne nyingi mapema kupitia nabii wake Hosea akisema: “Kwa sababu mmekataa ujuzi, nitawakataa pia msinitumikie mkiwa makuhani wangu; na kwa sababu mmesahau sheria ya Mungu wenu, Mimi mwenyewe nitawasahau wana wenu.” (Ho 4:6) Vivyo hivyo, Yesu aliwaambia hivi viongozi Wayahudi: “Ufalme wa Mungu utaondolewa kwenu na kupewa taifa linalozaa matunda yake.” (Mt 21:43) Hata hivyo, kwa kuwa Kristo alikuwa chini ya Sheria alipokuwa duniani alitambua kwamba ukuhani wa Haruni bado ulikuwa unatenda na aliwaelekeza wale aliokuwa anawaponya wamwendee kuhani na watoe dhabihu iliyopaswa kutolewa.—Mt 8:4; Mk 1:44; Lu 17:14.

AGOSTI 31–SEPTEMBA 6

HAZINA ZA NENO LA MUNGU | KUTOKA 21-22

“Onyesha Kwamba Una Maoni Kama ya Yehova Kuhusu Uhai”

it-1 271

Kupiga

Mwebrania aliyemiliki mtumwa aliruhusiwa kumpiga mtumwa wake wa kiume au wa kike kwa fimbo ikiwa mtumwa huyo angekosa kutii au angekuwa mwasi. Lakini ikiwa mmiliki huyo angemuua mtumwa wake alipokuwa akimpiga alipaswa kuadhibiwa. Lakini ikiwa mtumwa huyo angeishi kwa siku moja au mbili baada ya kupigwa hilo lingeonyesha kwamba mmiliki wake hakukusudia kumuua, alikuwa na haki ya kumpiga mtumwa huyo kwa sababu alimnunua “kwa pesa” zake. Ni vigumu kwa mtu kuharibu mali yake yenye thamani kwa sababu hilo lingemletea hasara. Pia ikiwa mtumwa huyo angekufa baada ya siku moja au zaidi, haingekuwa wazi ikiwa alikufa kwa sababu ya kupigwa au kwa sababu nyingine. Kwa hiyo, ikiwa mtumwa angeendelea kuishi kwa siku moja au mbili, bwana wake hakupaswa kuadhibiwa.—Kut 21:20, 21.

Kutafuta Hazina za Kiroho

it-1 1143

Pembe

Maneno yanayopatikana katika Kutoka 21:14 yanaweza kumaanisha kwamba hata kuhani angeweza kuuawa kwa kosa la uuaji, au kwamba tendo la kushika pembe za madhabahu lisingemlinda mtu yeyote aliyeua kimakusudi.—Linganisha 1Fa 2:28-34.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki