MAISHA YA MKRISTO
Kuboresha Ustadi Wetu Katika Huduma—Kuhubiri Katika Maeneo Yenye Ulinzi Mkali
KWA NINI NI MUHIMU: Kwa sababu ya kuongezeka kwa uhalifu, watu wameweka mifumo ya ulinzi katika nyumba zao, kama vile, kamera, simu za mlangoni, kuta ndefu, kufuga mbwa, na kuweka walinzi. Tunaweza kufanya nini ili kuwafikishia watu kama hao ujumbe wa habari njema? Kufuata vikumbusho vifuatavyo kunaweza kutusaidia kutoa ushahidi kwa ujasiri.
JINSI YA KUFANYA HIVYO:
Epuka kuchungulia dirishani au kuzunguka-zunguka nyumba ukimtafuta mwenye nyumba (w14 5/15 13 ¶10)
Epuka kufanya jambo lolote linaloweza kuwaudhi watu katika eneo unalohubiri (w14 5/15 13 ¶10)
Heshimu nyumba na mali ya wale walio katika eneo, huenda mwenendo wetu ukawavutia watu kwenye kweli.—1Pe 2:12 (w14 5/15 13 ¶10)
Epuka kupiga picha nyumba za watu katika eneo
Mwenye nyumba anapojibu kupitia kamera, zungumza kana kwamba unazungumza naye moja kwa moja. Tabasamu na utoe ishara kama kawaida. Sema jambo ulilopanga kusema ikiwa mwenye nyumba angefungua mlango. Usiweke uso wako karibu sana na kamera. Baada ya kumaliza kumbuka kwamba huenda bado mwenye nyumba akawa anakutazama au kukusikiliza