MAISHA YA MKRISTO
Kampeni ya Pekee ya Mwezi Novemba ya Kutangaza Ufalme wa Mungu
Yesu alitangaza “habari njema ya Ufalme wa Mungu.” (Lu 4:43) Pia, aliwafundisha watu kusali kwa ajili ya Ufalme huo. (Mt 6:9, 10) Mwezi wa Novemba, tutakuwa na kampeni ya pekee ya kutangaza Ufalme wa Mungu. (Mt 24:14) Panga ratiba yako ili ushiriki kikamili katika kampeni hiyo. Wote watakaotumikia wakiwa mapainia wasaidizi wanaweza kuchagua kutimiza takwa la saa 30 au 50 mwezi huo.
Waonyeshe watu wengi kadiri iwezekanavyo andiko linalozungumzia Ufalme wa Mungu. Unapochagua andiko utakalosoma, zingatia dini ya watu katika eneo lako. Mtu akionyesha upendezi katika ziara ya kwanza, mpe nakala ya toleo la watu wote la Mnara wa Mlinzi Na. 2 2020. Kisha fuatia upendezi haraka iwezekanavyo, na ujaribu kuanzisha funzo la Biblia ukitumia chapisho lililo katika Sanduku la Vifaa vya Kufundishia. Umebaki muda mfupi tu kabla ya Ufalme wa Mungu kupondaponda serikali zote zinazoupinga Ufalme huo. (Da 2:44; 1Ko 15:24, 25) Hivyo, acheni tutumie nafasi hii ya pekee kuonyesha kwamba tuko upande wa Yehova na Ufalme wake!
Ufalme wa Mungu utaifanya dunia iwe Paradiso!