HAZINA ZA NENO LA MUNGU | MAMBO YA WALAWI 1-3
Kusudi la Dhabihu
Waisraeli waliamriwa katika Sheria ya Musa watoe dhabihu, au matoleo. Dhabihu hizo zilimpendeza Yehova na zilimwakilisha Yesu na dhabihu ya fidia au faida zilizotokana na dhabihu hiyo.—Ebr 8:3-5; 9:9; 10:5-10.
Kama tu wanyama wote waliotolewa dhabihu walivyopaswa kuwa bila kasoro, Yesu alitoa mwili wake mkamilifu na usio na kasoro kuwa dhabihu.—1Pe 1:18, 19
Kama tu sehemu zote za dhabihu ya kuteketezwa zilivyopaswa kutolewa kwa Mungu, Yesu alijitoa kikamili kwa Yehova
Kama tu wale wanaotoa dhabihu ya ushirika inayokubalika walivyokuwa na amani pamoja na Mungu, watiwa-mafuta wanaoshiriki Mlo wa Jioni wa Bwana wana amani pamoja na Mungu