HAZINA ZA NENO LA MUNGU | MAMBO YA WALAWI 8-9
Uthibitisho wa Baraka za Yehova
Makuhani wa uzao wa Haruni walipowekwa rasmi, Yehova alitokeza moto ulioteketeza dhabihu ya kwanza ya kuteketezwa. Hilo lilionyesha kwamba Yehova alikubali na kuunga mkono mpango huo. Kwa kufanya hivyo Yehova alikuwa akiwatia moyo Waisraeli wote waliojionea tukio hilo waunge mkono kabisa ukuhani huo. Leo, Yehova anamtumia Yesu Kristo aliyetukuzwa kuwa Kuhani Mkuu zaidi. (Ebr 9:11, 12) Mnamo 1919, Yesu aliweka rasmi kikundi kidogo cha wanaume watiwa-mafuta kuwa “mtumwa mwaminifu na mwenye busara.” (Mt 24:45) Ni uthibitisho gani unaoonyesha kwamba mtumwa mwaminifu ana kibali, baraka, na utegemezo wa Yehova?
Licha ya upinzani wa kuendelea, mtumwa mwaminifu ameendelea kutoa chakula cha kiroho
Kama ilivyotabiriwa, habari njema inahubiriwa “katika dunia yote inayokaliwa.”—Mt 24:14
Tunawezaje kumuunga mkono kikamili mtumwa mwaminifu na mwenye busara?