Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwb21 Januari uku. 9
  • Mungu na Kristo Watatuletea Uhuru Wakati Ujao

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mungu na Kristo Watatuletea Uhuru Wakati Ujao
  • Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2021
  • Habari Zinazolingana
  • Yehova Anatusaidia Kukabiliana na Majaribu Yetu
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2023
  • Tuyaoneje Majaribu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2017
  • Uvumilivu
    Ufahamu wa Kina wa Maandiko
Pata Habari Zaidi
Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2021
mwb21 Januari uku. 9
Yesu ameketi katika kiti chake cha utawala mbinguni akitazama chini, na nyuma yake kuna mwangaza kutoka katika kiti cha ufalme cha Yehova.

MAISHA YA MKRISTO

Mungu na Kristo Watatuletea Uhuru Wakati Ujao

Unakabili changamoto gani kila siku? Je, wewe ni kichwa cha familia uliye na majukumu mengi? Je, wewe ni mzazi unayewalea watoto ukiwa peke yako huku ukijitahidi kuwaandalia riziki? Je, wewe ni kijana unayevumilia dhihaka kutoka kwa wanafunzi wenzako shuleni? Je, unasumbuliwa na matatizo ya afya au madhara yanayotokana na kuzeeka? Kila mtu anakabili changamoto fulani. Wakristo wengi wanakabili majaribu mbalimbali kwa wakati mmoja. Hata hivyo, tunajua kwamba hivi karibuni tutawekwa huru kutokana na matatizo hayo yote.—2Ko 4:16-18.

Hadi wakati huo tunafarijika kujua kwamba Yehova anajua changamoto tunazokabili, anathamini ushikamanifu na uvumilivu wetu, na ametuahidi baraka nyingi wakati ujao. (Yer 29:11, 12) Yesu pia anapendezwa na kila mmoja wetu. Tunapotimiza wajibu wetu wa Kikristo, Yesu anatuhakikishia hivi: “Mimi nipo pamoja nanyi.” (Mt 28:20) Tunapotua na kutafakari uhuru tutakaopata wakati ujao chini ya Ufalme wa Mungu, tunaimarisha tumaini na azimio letu la kuvumilia majaribu tunayokabili.—Ro 8:19-21.

TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA KADIRI DHORUBA INAVYOZIDI KUKARIBIA, ENDELEA KUMTAZAMA YESU KWA MAKINI!​—BARAKA ZA WAKATI UJAO, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:

  • Wanadamu walitenganishwaje na Mungu, na kulikuwa na matokeo gani?

  • Watumishi waaminifu wa Yehova watafurahia nini wakati ujao?

  • Ni nini kilichofanya iwezekane kuwa na wakati huo ujao wenye kupendeza?

  • Unatazamia kujionea baraka zipi katika ulimwengu mpya?

Picha: Watu wakifurahia Baraka katika Paradiso. 1. Dada akimkumbatia mtu aliyefufuliwa. 2. Wanafurahia chakula kingi, dunia safi, na amani.

Jiwazie katika ulimwengu mpya

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki