MAISHA YA MKRISTO
Jinsi ya Kutumia Mapendekezo ya Kuanzisha Mazungumzo
Kazi kubwa inafanywa ili kutayarisha mapendekezo ya kuanzisha mazungumzo, na wahubiri wengi wamepata matokeo mazuri wanapoyatumia katika eneo lao. Hata hivyo, kwa sababu kuna hali tofauti-tofauti ulimwenguni, wahubiri wanaposhiriki katika huduma wanaweza kutumia njia tofauti au habari tofauti zitakazowavutia watu katika eneo lao. Bila shaka, sote tunapaswa kufuata maagizo yoyote tunayopewa kwa ajili ya kampeni za pekee. Lengo letu ni kutii agizo la Yesu la kuhubiri habari njema ya Ufalme.—Mt 24:14.
Wahubiri wanaposhughulikia migawo ya wanafunzi, wanapaswa kuzungumzia habari iliyo katika pendekezo la kuanzisha mazungumzo katika Daftari la Huduma na Maisha. Hata hivyo, wahubiri wanaweza kuchagua swali, andiko, ziara inayofuata, au kikao kinachofaa katika eneo lao, isipokuwa kuwe na maagizo tofauti. Mwongozo huu mpya unarekebisha mwongozo uliokuwepo katika ukurasa wa 8 wa toleo la daftari la mkutano la Juni 2020.