Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwb24 Mei kur. 2-3
  • Mei 6-12

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mei 6-12
  • Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2024
Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2024
mwb24 Mei kur. 2-3

MEI 6-12

ZABURI 36-37

Wimbo 87 na Sala | Utangulizi (Dak. 1)

HAZINA ZA NENO LA MUNGU

1. “Usikasirike kwa Sababu ya Waovu”

(Dak. 10)

Waovu hutusababishia maumivu na mateso (Zb 36:​1-4; w17.04 10 ¶4)

Kuendelea kuwa na hasira dhidi ya “waovu” kunaweza pia kutusababishia madhara (Zb 37:​1, 7, 8; w22.06 10 ¶10)

Kutumaini ahadi za Yehova kunatuletea amani (Zb 37:​10, 11; w03 12/1 13 ¶20)

Dada mwenye wasiwasi akisoma habari kwenye simu yake. Anaona picha za waandamanaji wenye hasira, polisi akichukua hongo, wanajeshi wakifyatua risasi, mwanamume aliye na silaha akiwa kwenye eneo la kuegesha magari, umati wa watu wakiiba vitu dukani, msukosuko wa kijamii, na wanaotoa huduma za dharura wakiwa kwenye eneo la aksidenti ya gari.

JIULIZE, ‘Je, mimi hukazia fikira sana matendo ya ukatili yanayotangazwa kwenye vyombo vya habari?’

2. Hazina za Kiroho

(Dak. 10)

  • Zb 36:6—Huenda mtunga-zaburi alikuwa akimaanisha nini aliposema kwamba uadilifu wa Yehova ni “kama milima mikubwa [au, “kama milima ya Mungu,” maelezo ya chini]”? (it-2 445)

  • Ungependa kushiriki nasi hazina gani kutoka kwenye usomaji wa Biblia wa juma hili?

3. Usomaji wa Biblia

(Dak. 4) Zb 37:​1-26 (th somo la 10)

BORESHA HUDUMA YAKO

4. Kuanzisha Mazungumzo

(Dak. 3) NYUMBA KWA NYUMBA. (lmd somo la 1 jambo kuu la 5)

5. Kufuatia Upendezi

(Dak. 4) MAHUBIRI YASIYO RASMI. Mwalike mtu ambaye alikataa kujifunza Biblia zamani aanze kujifunza. (lmd somo la 9 jambo kuu la 4)

6. Hotuba

(Dak. 5) ijwbv 45—Kichwa: Ni Nini Maana ya Zaburi 37:4? (th somo la 13)

MAISHA YA MKRISTO

Wimbo 33

7. Je, Umejitayarisha kwa Ajili ya “Nyakati za Taabu”?

(Dak. 15) Mazungumzo.

Ulimwenguni pote, akina ndugu na dada wamepoteza mali zao na kufiwa na wapendwa wao kwa sababu ya misiba ya asili au inayosababishwa na wanadamu. (Zb 9:​9, 10) Kwa kusikitisha, ukweli ni kwamba sisi sote tunaweza kupatwa na “nyakati za taabu” wakati wowote ule, kwa hiyo tunapaswa kuwa tayari kukabiliana na majaribu hayo.

Tunaweza kufanya matayarisho gani mengine mbali tu na kuhifadhi vitua ambavyo vitatusaidia kukabiliana na janga?

  • Jitayarishe kiakili: Kubali kwamba janga linaweza kutokea, na ufikirie mambo unayoweza kufanya linapotokea. Usiruhusu moyo wako ushikamane sana na vitu vyako vya kimwili. Hilo litakusaidia kutenda kwa hekima na kufanya maamuzi yatakayokusaidia kuzingatia usalama na kuokoa uhai badala ya kuhangaikia kuokoa vitu vyako vya kimwili. (Mwa 19:16; Zb 36:9) Isitoshe, kuepuka kufanya hivyo kutakusaidia kuwa na maoni yaliyosawazika unapopoteza mali zako wakati wa janga, na pia hutaumia kihisia kupita kiasi.—Zb 37:19

  • Jitayarishe kiroho: Imarisha imani yako katika uwezo wa Yehova wa kukutunza na ujihakikishie kwamba anatamani kukutunza. (Zb 37:18) Kabla ya janga, jikumbushe kwa ukawaida kwamba Yehova atawaongoza na kuwategemeza watumishi wake hata ikiwa huenda tutaokoa tu ‘uhai wetu.’—Yer 45:5; Zb 37:​23, 24.

Tukiwa na uhakika kabisa kwamba Yehova atatimiza ahadi zake, tunamfanya kuwa “ngome [yetu] wakati wa taabu.”—Zb 37:39.

Picha: Picha mbalimbali kutoka kwenye video yenye kichwa “Je, Umejitayarisha Kukabiliana na Majanga?” 1. Ndugu akisoma Biblia. 2. Mawimbi ya tsunami. 3. Mawingu mazito ya dhoruba. 4. Watu wakibeba mali zao katika eneo lililofurika.

Onyesha VIDEO Je, Umejitayarisha Kukabiliana na Majanga? Kisha waulize wasikilizaji:

  • Yehova anaweza kutusaidiaje wakati wa janga?

  • Tunaweza kuchukua hatua zipi ili kujitayarisha?

  • Tunaweza kuwasaidiaje wale ambao wameathiriwa na majanga?

LENGO

  • Unaposoma na kujifunza Biblia, hifadhi maandiko unayoweza kutumia kujifariji na kuwafariji wengine. Huenda ikafaa kuorodhesha mistari hiyo ukitumia “Vibandiko” kwenye sehemu ya “Funzo la Kibinafsi” katika programu ya JW Library®. Kwa mfano, ona baadhi ya maandiko yaliyoorodheshwa katika makala yenye kichwa “Biblia Inasema Nini Kuhusu Misiba ya Asili?” kwenye jw.org.

8. Funzo la Biblia la Kutaniko

(Dak. 30) bt sura ya 9 ¶8-16

Umalizio (Dak. 3) | Wimbo 57 na Sala

a Ona Amkeni! Na. 5 2017, ukurasa 4-6.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki