Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwb24 Mei kur. 6-7
  • Mei 27–Juni 2

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mei 27–Juni 2
  • Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2024
Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2024
mwb24 Mei kur. 6-7

MEI 27–JUNI 2

ZABURI 42-44

Wimbo 86 na Sala | Utangulizi (Dak. 1)

HAZINA ZA NENO LA MUNGU

1. Nufaika Kikamili Kutokana na Mafundisho ya Yehova

(Dak. 10)

Tumia nafasi zote unazopata za kumwabudu Yehova pamoja na wengine, ikiwezekana fanya hivyo uso kwa uso (Zb 42:​4, 5; w06 6/1 9 ¶4)

Sali kabla ya kujifunza Neno la Mungu (Zb 42:8; w12 1/15 15 ¶2)

Iruhusu Biblia ikuongoze katika kila jambo unalofanya maishani (Zb 43:3)

Akina dada wakisikiliza kwa makini na kuandika mambo makuu wakati wa kusanyiko la eneo.

Mafundisho ya Yehova yanatuimarisha tukabiliane na majaribu na kutuwezesha kuishi kupatana na wakfu wetu.—1Pe 5:10; w16.09 5 ¶11-12.

2. Hazina za Kiroho

(Dak. 10)

  • Zb 44:19—Huenda maneno “mahali ambapo mbwamwitu wanakaa” yanamaanisha nini? (it-1 1242)

  • Ungependa kushiriki nasi hazina gani kutoka kwenye usomaji wa Biblia wa juma hili?

3. Usomaji wa Biblia

(Dak. 4) Zb 44:​1-26 (th somo la 11)

BORESHA HUDUMA YAKO

4. Kuanzisha Mazungumzo

(Dak. 4) NYUMBA KWA NYUMBA. Mwalike ajifunze Biblia. (lmd somo la 5 jambo kuu la 5)

5. Kufuatia Upendezi

(Dak. 5) NYUMBA KWA NYUMBA. Mwalike mwenye nyumba asikilize hotuba ya watu wote ifuatayo. Tumia video Ni Nini Hutendeka Katika Jumba la Ufalme? (lmd somo la 7 jambo kuu la 5)

6. Hotuba

(Dak. 3) lmd nyongeza A jambo kuu la 4—Kichwa: Kila Mtu Atakuwa na Afya Kamilifu. (th somo la 2)

MAISHA YA MKRISTO

Wimbo 21

7. Fanya Maamuzi Yenye Hekima Kuhusu Kazi na Elimu

(Dak. 15) Mazungumzo.

Picha: Ndugu kijana akisoma Biblia na kutafakari atafanya nini baada ya kumaliza sekondari. 1. Akizungumza na mshauri shuleni. 2. Akihudhuria Shule ya Waeneza-Injili wa Ufalme. 3. Akihubiri katika nchi ya kigeni.

Vijana, je, mmepanga mtakachofanya baada ya kumaliza shule ya sekondari? Huenda tayari unafikiria kufanya kazi ambayo itakuruhusu kuwa painia. Au huenda ukawa unafikiria kupata mafunzo fulani ambayo yatakusaidia kupata ustadi, leseni, au diploma itakayokuwezesha kupata kazi ya aina hiyo. Bila shaka unasisimka kufikiria kuhusu mambo hayo! Hata hivyo, huenda ukahisi umelemewa kwa sababu ya maamuzi unayopaswa kufanya au ukahisi una mkazo kwa sababu ungependa kufanya uamuzi utakaowafurahisha wengine. Ni nini kinachoweza kukusaidia kufanya maamuzi yenye hekima?

Soma Mathayo 6:​32, 33. Kisha waulize wasikilizaji:

  • Kwa nini ni muhimu kujiwekea miradi hususa ya kiroho kabla ya kufanya maamuzi muhimu kuhusu kazi na elimu?

  • Wazazi wanaweza kuwasaidiaje watoto wao kutumia ushauri ulio kwenye Mathayo 6:​32, 33?—Zb 78:​4-7

Uwe mwangalifu usiruhusu tamaa ya kuwa na usalama wa kifedha au umashuhuri iathiri maamuzi yako. (1Yo 2:​15, 17) Kumbuka kwamba kuwa na mali nyingi kunaweza kufanya iwe vigumu kwa mtu kukubali ujumbe wa Ufalme. (Lu 18:​24-27) Ikiwa mtu anafuatilia utajiri ni vigumu kwake kukua kiroho na kukazia fikira kumpendeza Yehova.—Mt 6:24; Mk 8:36.

Onyesha VIDEO Jihadhari Usitegemee Vitu Visivyodumu!—Utajiri. Kisha waulize wasikilizaji:

  • Methali 23:​4, 5 inaweza kukusaidiaje kufanya maamuzi yenye hekima?

MADOKEZO

  • Jiwekee miradi ya kiroho ya muda mfupi na ya muda mrefu

  • Hakikisha kwamba maamuzi unayofanya kuhusu elimu na kazi unayopanga kufanya wakati ujao, haitakuzuia kufikia miradi yako ya kiroho

  • Chagua masomo ambayo yatakusaidia na uwe tayari kunyumbulika. Ukichagua kufuatia elimu au mafunzo fulani, hakikisha kuna nafasi nyingi za kazi katika fani unayosomea

8. Funzo la Biblia la Kutaniko

(Dak. 30) bt sura ya 10 ¶5-12

Umalizio (Dak. 3) | Wimbo 47 na Sala

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki