Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwb24 Septemba kur. 14-15
  • Oktoba 28–Novemba 3

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Oktoba 28–Novemba 3
  • Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2024
Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2024
mwb24 Septemba kur. 14-15

OKTOBA 28–NOVEMBA 3

ZABURI 103-104

Wimbo 30 na Sala | Utangulizi (Dak. 1)

HAZINA ZA NENO LA MUNGU

1. Anakumbuka “Kwamba Sisi Ni Mavumbi”

(Dak. 10)

Huruma ya Yehova humchochea kuwa na usawaziko (Zb 103:8; w23.07 21 ¶5)

Anaendelea kutuonyesha subira tunapomkosea (Zb 103:​9, 10; w23.09 6-7 ¶16-18)

Hatarajii mengi kutoka kwetu kuliko tunavyoweza kufanya (Zb 103:14; w23.05 26 ¶2)

Mume akimsikiliza mke wake kwa makini anapoeleza hisia zake.

JIULIZE, ‘Je, ninamtendea mwenzi wangu wa ndoa kwa njia inayoonyesha ninamwiga Yehova katika kuonyesha usawaziko?’

2. Hazina za Kiroho

(Dak. 10)

  • Zb 104:24—Mstari huu unatufundisha nini kuhusu uwezo wa Yehova wa kuumba vitu vya aina mbalimbali? (cl 55 ¶18)

  • Ungependa kushiriki nasi hazina gani kutoka kwenye usomaji wa Biblia wa juma hili?

3. Usomaji wa Biblia

(Dak. 4) Zb 104:​1-24 (th somo la 11)

BORESHA HUDUMA YAKO

4. Kuanzisha Mazungumzo

(Dak. 3) MAHUBIRI YA UMMA. (lmd somo la 3 jambo kuu la 4)

5. Kufuatia Upendezi

(Dak. 4) NYUMBA KWA NYUMBA. Zungumzia video Karibu Kwenye Funzo Lako la Biblia na mtu aliyekubali funzo la Biblia. (th somo la 9)

6. Hotuba

(Dak. 5) lmd nyongeza A jambo kuu la 6—Kichwa: Mume Anapaswa “Kumpenda Mke Wake Kama Anavyojipenda Mwenyewe.” (th somo la 1)

MAISHA YA MKRISTO

Wimbo 44

7. Je, Unajua Mipaka Yako?

(Dak. 15) Mazungumzo.

Yehova anafurahi tunapompa kilicho bora, nasi tunapata shangwe pia. (Zb 73:28) Hata hivyo, kujaribu kufanya kilicho bora bila kuzingatia mipaka yetu kunaweza kutusababishia mahangaiko yasiyo ya lazima na kutuvunja moyo.

Msichana aliye kwenye video “Tunaweza Kutimiza Mengi Tukiwa na Matarajio Halisi.”

Onyesha VIDEO Tunaweza Kutimiza Mengi Tukiwa na Matarajio Halisi. Kisha waulize wasikilizaji:

  • Yehova anataka nini kutoka kwetu? (Mik 6:8)

  • Picha kutoka kwenye video “Tunaweza Kutimiza Mengi Tukiwa na Matarajio Halisi.” Msichana akiwa pamoja na rafiki yake, akimtia moyo mwanafunzi wake wa Biblia kwenye mkahawa.
  • Ni nini kilichomsaidia dada huyo aache kuwa na mahangaiko kuhusu kufikia lengo lake?

TUNAWEZA KUTAMBUAJE MIPAKA YETU?

  • Epuka mwelekeo wa kujilinganisha. (Gal 6:4) Usiruhusu mambo ambayo wengine wanafanya yadhibiti mambo unayofanya au unachofikiri unaweza kufanya. Huenda ukaweza kutimiza mengi au machache zaidi kuliko mtu mwenye umri kama wako au ambaye hali ya familia yake inafanana na yako

  • Usiruhusu woga ukuzuie kujaribu mambo mapya. (Ro 12:1; 1Ko 7:31) Usiogope kujaribu aina ya utumishi ambao, mwanzoni huenda ukaonekana ni vigumu kuutimiza au ambao huenda ukafikiri hutaufurahia.—Mal 3:10

  • Chunguza unachoweza kutimiza kwa kujiwekea malengo ya muda mfupi. Kwa mfano, je, unaweza kuwa painia wa kawaida? Kwa nini usijaribu kuongeza muda unaotumia katika huduma kwa miezi kadhaa au kufanya upainia msaidizi? Je, unaweza kujaribu kufanya upainia wa kawaida kwa mwaka mmoja? Hata ikiwa utafikia mkataa kwamba huwezi kuwa painia wa kawaida au kufanya hivyo kwa mwaka mmoja, hutajutia malengo madogo uliyofaulu kutimiza.—Mhu 6:9.

  • Uwe tayari kubadilikana na hali. Hali zetu hubadilika, na mipaka yetu hubadilika pia. Kwa hiyo, chunguza upya malengo yako kwa ukawaida

8. Funzo la Biblia la Kutaniko

(Dak. 30) bt sura ya 17 ¶8-12, sanduku uk. 137

Umalizio (Dak. 3) | Wimbo 55 na Sala

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki