NOVEMBA 4-10
ZABURI 105
Wimbo 3 na Sala | Utangulizi (Dak. 1)
1. “Anakumbuka Agano Lake Milele”
(Dak. 10)
Yehova alimpa Abrahamu ahadi na akairudia kwa Isaka na Yakobo (Mwa 15:18; 26:3; 28:13; Zb 105:8-11)
Huenda ilionekana kwamba ahadi hiyo haingeweza kutimia (Zb 105:12, 13; w23.04 28 ¶11-12)
Yehova hakusahau kamwe agano lake na Abrahamu (Zb 105:42-44; it-2 1201 ¶2)
JIULIZE, ‘Ni nini kinachoweza kunihakikishia kwamba ninaweza kumtumaini Yehova kikamili?’
2. Hazina za Kiroho
(Dak. 10)
Zb 105:17-19—“Neno la Yehova” lilimsafishaje Yosefu? (w86 11/1 19 ¶15)
Ungependa kushiriki nasi hazina gani kutoka kwenye usomaji wa Biblia wa juma hili?
3. Usomaji wa Biblia
(Dak. 4) Zb 105:24-45 (th somo la 5)
4. Kuanzisha Mazungumzo
(Dak. 1) NYUMBA KWA NYUMBA. Mwenye nyumba ana shughuli nyingi. (lmd somo la 2 jambo kuu la 5)
5. Kuanzisha Mazungumzo
(Dak. 2) NYUMBA KWA NYUMBA. Maliza mazungumzo kwa njia nzuri mwenye nyumba anapoanza kubishana. (lmd somo la 4 jambo kuu la 5)
6. Kufuatia Upendezi
(Dak. 4) NYUMBA KWA NYUMBA. Toa gazeti linalohusu habari ambayo mwenye nyumba alipendezwa nayo wakati uliopita. (lmd somo la 8 jambo kuu la 3)
7. Kufuatia Upendezi
(Dak. 4) MAHUBIRI YASIYO RASMI. Mweleze mtu huyo kuhusu programu ya JW Library®, na umsaidie kuipakua. (lmd somo la 9 jambo kuu la 5)
Wimbo 84
8. Wonyesho wa Upendo Wako
(Dak. 15) Mazungumzo.
Tunapotumia wakati, nguvu, na mali zetu ili kuunga mkono utendaji wa Ufalme, tunaonyesha upendo wetu kwa Mwana wa Yehova aliyewekwa rasmi ili kuwa Mfalme, Yesu Kristo. Kuonyesha upendo wetu kwa njia hiyo kunatufanya tupendeze machoni pa Yehova na kuwanufaisha ndugu na dada zetu. (Yoh 14:23) Makala za mfululizo kwenye jw.org zenye kichwa “Jinsi Michango Yako Inavyotumiwa” zinaonyesha jinsi michango yetu inavyosaidia sana undugu wetu wa ulimwenguni pote.
Onyesha VIDEO Michango Yako Ina Nguvu. Kisha waulize wasikilizaji:
Kutumia michango yetu ili kutetea uhuru wetu wa ibada kumewanufaishaje ndugu zetu?
“Usawazisho” wa michango umesaidiaje katika ujenzi wa Majumba ya Ufalme?—2Ko 8:14
Kumekuwa na manufaa gani ya kutumia michango kutegemeza kazi ya kutafsiri Biblia katika lugha nyingi?
9. Funzo la Biblia la Kutaniko
(Dak. 30) bt sura ya 17 ¶13-19