Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwb25 Januari kur. 2-3
  • Januari 6-12

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Januari 6-12
  • Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2025
Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2025
mwb25 Januari kur. 2-3

JANUARI 6-12

ZABURI 127-134

Wimbo 134 na Sala | Utangulizi (Dak. 1)

HAZINA ZA NENO LA MUNGU

1. Wazazi—Endeleeni Kuutunza Urithi Wenu Wenye Thamani

(Dak. 10)

Wazazi wanaweza kuwa na uhakika kwamba Yehova atawasaidia kupata mahitaji ya familia zao (Zb 127:​1, 2)

Watoto ni zawadi yenye thamani kutoka kwa Yehova (Zb 127:3; w21.08 5 ¶9)

Mzoeze kila mtoto kulingana na mahitaji yake (Zb 127:4; w19.12 27 ¶20)

Baba akitumia broshua “Masomo Yangu ya Biblia” kujifunza na watoto wake wawili. Watoto wanajiwazia wakicheza na tembo na sokwe katika paradiso.

Yehova anafurahi sana wazazi wanapomtegemea na kufanya yote wanayoweza kuwatunza watoto wao

2. Hazina za Kiroho

(Dak. 10)

  • Zb 128:3—Kwa nini mtunga-zaburi analinganisha wana na machipukizi, au miche, ya mzeituni? (w00 5/15 27 ¶3-5)

  • Ungependa kushiriki nasi hazina gani kutoka kwenye usomaji wa Biblia wa juma hili?

3. Usomaji wa Biblia

(Dak. 4) Zb 132:​1-18 (th somo la 2)

BORESHA HUDUMA YAKO

4. Kuanzisha Mazungumzo

(Dak. 3) MAHUBIRI YASIYO RASMI. (lmd somo la 1 jambo kuu la 3)

5. Kuanzisha Mazungumzo

(Dak. 4) MAHUBIRI YASIYO RASMI. Mtu huyo anataja jambo lisilopatana na fundisho fulani la Biblia. (lmd somo la 5 jambo kuu la 4)

6. Kufanya Wanafunzi

(Dak. 5) lff somo la 16 jambo kuu la 4-5. Zungumza na mwanafunzi wako kuhusu mipango uliyofanya ili aendelee na funzo wakati ambapo hutakuwepo. (lmd somo la 10 jambo kuu la 4)

MAISHA YA MKRISTO

Wimbo 13

7. Wazazi—Je, Mnatumia kwa Ufanisi Kifaa Hiki Kilicho na Nguvu Sana?

(Dak. 15) Mazungumzo.

Tengenezo la Yehova limetokeza machapisho na vifaa vingine vingi vya kuwasaidia wazazi kuwafundisha watoto wao kumhusu Yehova. Hata hivyo, kifaa kilicho na nguvu zaidi ambacho wazazi wanaweza kutumia ni mfano wao mzuri.—Kum 6:​5-9.

Yesu alitumia kifaa hicho muhimu kuwafundisha wanafunzi wake.

Soma Yohana 13:​13-15. Kisha waulize wasikilizaji:

  • Kwa nini unafikiri njia ya Yesu ya kufundisha kupitia mfano wake ilikuwa na matokeo mazuri?

Ukiwa mzazi, matendo yako yanaweza kukazia umuhimu wa mambo unayomfundisha. Pia, mfano wako mzuri utamfanya aheshimu mambo unayofundisha na kumchochea mtoto wako kusikiliza.

Picha: Picha kutoka kwenye video “Kuwafundisha Watoto Kupitia Mfano Wetu.” 1. Familia ya Garcia wakiwa ndani ya gari wakiwa tayari kwenda kwenye mkutano wa kutaniko. 2. Familia hiyo ikiwa imeketi mezani baada ya kutoka mkutanoni. Wanafurahia vitafunwa na mazungumzo. 3. Ndugu Garcia anaacha kujifunza kwa muda ili kumsikiliza binti yake. 4. Ndugu na Dada Garcia wakitumia Biblia kuzungumza na binti yao.

Onyesha VIDEO Kuwafundisha Watoto Kupitia Mfano Wetu. Kisha waulize wasikilizaji:

  • Ndugu na Dada Garcia waliwafundisha binti zao masomo gani muhimu?

  • Video hii inakuchocheaje kuendelea kuwawekea watoto wako mfano mzuri?

Kupitia mfano wako, unaweza kuwafundisha watoto wako . . .

  • kufanya maamuzi mazuri kuhusu burudani, kileo, na matumizi ya mitandao ya kijamii

  • kutanguliza mambo ya kiroho

  • kumtendea mwenzi wa ndoa kwa upendo na heshima

8. Funzo la Biblia la Kutaniko

(Dak. 30) bt sura ya 20 ¶13-20

Umalizio (Dak. 3) | Wimbo 73 na Sala

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki