APRILI 28–MEI 4
METHALI 11
Wimbo 90 na Sala | Utangulizi (Dak. 1)
1. Usiseme!
(Dak. 10)
Usiseme jambo lolote linaloweza kumuumiza ‘jirani yako’ (Met 11:9; w02 5/15 26 ¶4)
Usiseme jambo linaloleta mgawanyiko (Met 11:11; w02 5/15 27 ¶2-3)
Usiseme jambo la siri la mwenzako (Met 11:12, 13; w02 5/15 27 ¶5)
JAMBO LA KUTAFAKARI: Maneno ya Yesu kwenye Luka 6:45 yanaweza kutusaidiaje tuepuke kusema mambo yenye kudhuru?
2. Hazina za Kiroho
(Dak. 10)
Met 11:17—Kuonyesha fadhili kunatunufaishaje? (g20.1 11, sanduku)
Ungependa kushiriki nasi hazina gani kutoka kwenye usomaji wa Biblia wa juma hili?
3. Usomaji wa Biblia
(Dak. 4) Met 11:1-20 (th somo la 5)
4. Kuanzisha Mazungumzo
(Dak. 4) MAHUBIRI YASIYO RASMI. Tafuta nafasi ya kumweleza mtu huyo jambo ambalo ulijifunza kwenye mkutano hivi karibuni. (lmd somo la 2 jambo kuu la 4)
5. Kufuatia Upendezi
(Dak. 4) MAHUBIRI YASIYO RASMI. Tumia video kutoka kwenye Sanduku la Vifaa vya Kufundishia. (lmd somo la 8 jambo kuu la 3)
6. Kufanya Wanafunzi
(Dak. 4) MAHUBIRI YA UMMA. Mwalike ajifunze Biblia na umwonyeshe jinsi linavyoongozwa. (lmd somo la 10 jambo kuu la 3)
Wimbo 157
7. Usiache Ulimi Wako Uharibu Amani
(Dak. 15) Mazungumzo.
Kwa kuwa sisi si wakamilifu, tunaweza kujikwaa katika maneno yetu. (Yak 3:8) Hata hivyo, tukifikiria madhara yanayoweza kutokea, tutaepuka kusema mambo ambayo tutajutia baadaye. Ulimi wetu unaweza kuharibu amani ya kutaniko katika njia zifuatazo:
Kujisifu isivyofaa. Haya ni mazungumzo ya kujisifu na yanaweza kuchochea mashindano na wivu.—Met 27:2
Udanganyifu. Mbali na kusema uwongo moja kwa moja, mazungumzo haya yanatia ndani kuwapotosha watu kimakusudi. Hata udanganyifu mdogo unaweza kumfanya mtu asitumainiwe na kuharibu sifa yetu.—Mhu 10:1
Porojo Zenye Kuumiza. Haya ni mazungumzo ya ovyoovyo kuhusu watu na maisha yao. Mazungumzo hayo hupotosha ukweli au kufunua mambo ya siri. (1Ti 5:13) Yanaweza kutokeza ugomvi na migawanyiko
Maneno Yanayosemwa kwa Hasira. Haya ni maneno yanayosemwa kwa ukali na bila kujizuia dhidi ya mtu aliyetukasirisha. (Efe 4:26) Yanaweza kuwaumiza wengine.—Met 29:22
Onyesha VIDEO ‘Vua’ Mazoea Yanayoharibu Amani—Kisehemu. Kisha waulize wasikilizaji:
Umejifunza nini kuhusu jinsi mazungumzo yetu yanavyoweza kuharibu amani ya kutaniko?
Ili uone jinsi amani ilivyorudishwa, tazama video yenye kichwa “Tafuta Amani na Kuifuatilia.”
8. Funzo la Biblia la Kutaniko
(Dak. 30) bt sura ya 25 ¶14-21