Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w24 Januari uku. 19
  • Je, Wajua?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Wajua?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2024
  • Habari Zinazolingana
  • Filipo Ambatiza Ofisa Mwethiopia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Kutangaza “Habari Njema Kumhusu Yesu”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
  • Filipo—Mweneza-Evanjeli Mwenye Bidii
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Msaada wa Kuielewa Biblia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2024
w24 Januari uku. 19
Filipo ameketi pamoja na mwanamume Mwethiopia, anamfafanulia Maandiko wakiwa katika gari la kukokotwa na farasi lenye magurudumu manne na mwendeshaji.

Je, Wajua?

Ni gari la aina gani ambalo towashi Mwethiopia alikuwa akitumia Filipo alipomkaribia?

NENO la awali lililotafsiriwa “gari” katika Tafsiri ya Ulimwengu Mpya linaweza kurejelea aina mbalimbali za magari ya kukokotwa na farasi. (Mdo. 8:28, 29, 38) Hata hivyo, inaonekana kwamba towashi Mwethiopia alikuwa akiendesha gari kubwa, si gari dogo la kukokotwa lililotumiwa vitani au kwenye mashindano. Fikiria baadhi ya sababu za kufikia mkataa huu.

Towashi Mwethiopia alikuwa ofisa wa cheo cha juu aliyekuwa amesafiri umbali mrefu. Alikuwa “mwanamume aliyekuwa na mamlaka chini ya Kandake, malkia wa Waethiopia, na ambaye alisimamia hazina yote ya malkia.” (Mdo. 8:27) Ethiopia ya kale ilitia ndani maeneo ya nchi ambayo sasa inaitwa Sudan na baadhi ya maeneo ya upande wa kusini kabisa wa nchi ya sasa ya Misri. Ingawa huenda mwanamume huyo hakutumia gari lilelile katika safari yake yote, lazima alikuwa na mizigo kwa ajili ya safari hiyo ndefu. Baadhi ya magari yaliyotumiwa kusafirisha abiria katika karne ya kwanza W.K. yalikuwa na magurudumu manne. Kitabu kinachoitwa Actsy​—An Exegetical Commentary kinasema hivi: “Magari hayo ya kukokotwa yalikuwa na nafasi ya kutosha ya kubeba mizigo na kufanya safari iwe yenye kustarehesha zaidi, na huenda yalimwezesha mtu kusafiri umbali mrefu zaidi.”

Towashi Mwethiopia alikuwa akisoma, Filipo alipomkaribia. Simulizi hilo linasema kwamba “Filipo akakimbia kandokando na kumsikia [towashi] akimsoma kwa sauti kubwa nabii Isaya.” (Mdo. 8:30) Magari ya kukokotwa kwa ajili ya safari hayakutengenezwa ili yaende kasi. Mwendo huo wa polepole ulimwezesha towashi asome na pia Filipo aliyekuwa akitembea kwa miguu aweze kumfikia.

Towashi Mwethiopia “akamsihi Filipo apande aketi pamoja naye.” (Mdo. 8:31) Katika gari la kukokotwa la mashindano, waendeshaji walisimama. Hata hivyo, kwenye gari la kukokotwa kwa ajili ya safari kungekuwa na nafasi ambayo towashi na Filipo wangeweza kuketi.

Kulingana na rekodi iliyoongozwa na roho inayopatikana kwenye Matendo sura ya 8 na uthibitisho wa kihistoria unaopatikana, machapisho yetu ya hivi karibuni yanaonyesha towashi Mwethiopia akitumia gari kubwa badala ya gari dogo la kukokotwa la kivita au la mashindano.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki