Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • yb15 uku. 86-uku. 89 fu. 2
  • Ugunduzi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ugunduzi
  • 2015 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
  • Vichwa vidogo
  • Mwanzo wa Ugunduzi
  • Ziara ya Ndugu Knorr na Franz
  • Kazi Inapanuka
2015 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
yb15 uku. 86-uku. 89 fu. 2
Picha katika ukurasa wa 86

JAMHURI YA DOMINIKA

Ugunduzi

Mwanzo wa Ugunduzi

Jumapili, Aprili 1, 1945, wahitimu wa Shule ya Gileadi, Lennart na Virginia Johnson waliwasili Ciudad Trujillo (sasa Santo Domingo), mji mkuu wa Jamhuri ya Dominika. Wakiwa Mashahidi wa kwanza nchini, waliingia katika nchi iliyokuwa na historia ya migogoro na vita.a Kitabu cha Mwaka wa 1946 kiliripoti hivi: “Kwa kweli hili ni eneo jipya kabisa, na wahitimu hawa wa Gileadi wanalazimika kuanzia sifuri.” Hebu wazia: Hakukuwa na ofisi ya tawi, Majumba ya Ufalme, wala makutaniko. Wamishonari hao hawakumfahamu mtu yeyote katika nchi hiyo, hawakujua vizuri Kihispania, na hawakuwa na nyumba wala fanicha yoyote. Wangefanya nini?

Grafu katika ukurasa wa 86

“Tulienda kwenye Hoteli ya Victoria na kukodi chumba—tulihitaji kulipa dola tano kwa siku, kutia ndani chakula,” alikumbuka Lennart. “Siku hiyohiyo alasiri tulianzisha funzo la kwanza la Biblia. Mambo yalikuwa hivi: Wanawake wawili raia wa Dominika ambao tuliwafundisha Biblia mjini Brooklyn walikuwa wametupatia majina ya marafiki na ndugu zao wa ukoo, mmoja wao alikuwa Dakt. Green. Tulipomtembelea, tulikutana pia na jirani yake Moses Rollins. Walipojua jinsi tulivyopata majina na anwani zao, walisikiliza kwa makini ujumbe wa Ufalme na wakakubali kujifunza Biblia. Baada ya muda mfupi, Moses akawa mwenyeji wa kwanza kuwa mhubiri wa Ufalme.”

Wamishonari wengine wanne waliwasili mwanzoni mwa Juni 1945, na baada ya muda mfupi waligawanya machapisho mengi na kuanzisha mafunzo mengi ya Biblia. Kufikia Oktoba ikawa wazi kwamba walihitaji mahali pa kufanyia mikutano. Kwa hiyo, wamishonari hao walirekebisha sebule na vyumba vyao vya kulia chakula ili vitumiwe kama Jumba la Ufalme. Zaidi ya watu 40 walikuwa wakihudhuria mikutano hiyo.

Picha katika ukurasa wa 90

Miongoni mwa watu wa kwanza kukubali kweli alikuwa Pablo Bruzaud, wengi walimjua kama Palé. Alikuwa dereva wa basi lililofanya safari zake kati ya Santiago na Ciudad Trujillo, hivyo alisafiri mara nyingi kwenda katika mji mkuu. Siku moja alipokuwa Ciudad Trujillo, Palé alikutana na Mashahidi, na baada ya mazungumzo akakubali kitabu “The Truth Shall Make You Free.” Wamishonari hao walianza kumfundisha Biblia kila siku. Baada ya muda, Palé alianza kuhubiri na wamishonari na aliwasaidia kusafiri. Baadaye, alikutana na Lennart Johnson kisha wakasafiri kutoka Ciudad Trujillo kuelekea Santiago na kuvuka milima hadi kwenye mji wa pwani wa Puerto Plata ili kutembelea kikundi cha watu waliopendezwa ambao walikuwa wametuma barua makao makuu Brooklyn, New York, wakiomba habari zaidi.

Ziara ya Ndugu Knorr na Franz

Machi 1946, Nathan Knorr na Frederick Franz kutoka makao makuu walitembelea Jamhuri ya Dominika. Ziara hiyo ilisubiriwa kwa hamu sana, na mbali na ndugu na dada, watu 75 waliopendezwa na ujumbe wa Ufalme walihudhuria hotuba iliyotolewa na Ndugu Knorr. Wakati wa ziara hiyo, Ndugu Knorr alifanya mipango ya kuanzishwa kwa ofisi ya tawi katika Jamhuri ya Dominika.

Picha katika ukurasa wa 89

Ndugu Knorr na Franz wakiwa katika Jumba la kwanza la Ufalme, Ciudad Trujillo

Wamishonari zaidi waliwasili, na kufikia mwishoni mwa mwaka wa utumishi wa 1946, kulikuwa na wahubiri 28 nchini. Kwa kuwa habari njema ilikuwa imeanza tu kuhubiriwa katika nchi hiyo, wamishonari hao walitumia muda mwingi wakati wa jioni kuchora ramani sahihi za maeneo ili kuhakikisha kwamba kampeni ya kuhubiri inafanywa kwa utaratibu na kwa ukamili.

Kazi Inapanuka

Mnamo 1947, wahubiri zaidi ya 59 walikuwa wakishiriki katika kazi ya kuhubiri. Mwaka huohuo, baadhi ya wamishonari waliotumikia nchini Kuba walipewa mgawo mpya wa kutumikia katika Jamhuri ya Dominika. Miongoni mwao walikuwa Roy na Juanita Brandt. Ndugu Brandt aliwekwa rasmi kuwa mtumishi wa tawi na akaifanya kazi hiyo kwa miaka kumi.

Kufikia mwishoni mwa mwaka wa utumishi wa 1948, kulikuwa na wahubiri 110 hivi, ambao walishirikiana na wamishonari wenye bidii kuhubiri habari njema. Hata hivyo, wahubiri hao wenye bidii hawakujua kwamba kungekuwa na nyakati ngumu sana katika siku za usoni.

a Machapisho ya Watch Tower yaligawanywa katika Jamhuri ya Dominika mapema mwaka wa 1932, hata hivyo watu binafsi walianza kufundishwa Biblia mwaka wa 1945, Lennart na Virginia Johnson walipowasili.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki