Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • yb15 uku. 94-uku. 97 fu. 1
  • Wafungwa na Kupigwa Marufuku

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wafungwa na Kupigwa Marufuku
  • 2015 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
  • Vichwa vidogo
  • Wafungwa Gerezani kwa Kutounga Mkono Upande Wowote
  • Mashahidi wa Yehova Wapigwa Marufuku
2015 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
yb15 uku. 94-uku. 97 fu. 1

JAMHURI YA DOMINIKA

Wafungwa na Kupigwa Marufuku

Wafungwa Gerezani kwa Kutounga Mkono Upande Wowote

Picha katika ukurasa wa 95

Enrique Glass na chumba cha shimo alimofungwa kwa majuma mawili

Juni 19, 1949, kikundi cha Wadominika waliokuwa uhamishoni walirudi katika Jamhuri ya Dominika kwa lengo la kumpindua dikteta Rafael Trujillo. Ingawa uvamizi huo ulisambaratishwa haraka, serikali ya Trujillo iliwafunga gerezani wale wote waliokataa utumishi wa kijeshi, na pia mtu yeyote aliyeonekana kuipinga serikali. Miongoni mwa Mashahidi wa kwanza waliofungwa kwa kukataa utumishi wa kijeshi ni León, Enrique, na Rafael Glass, pamoja na Mashahidi wengine waliofanya kazi pamoja na León.

León alieleza hivi: “[Mimi na wafanya kazi wenzangu] tulikamatwa na kuhojiwa na maofisa wa jeshi. Baada ya kutishwa vikali, tuliachiwa huru, lakini siku chache baadaye bila maofisa kufuata utaratibu rasmi, walituamuru tujiandikishe jeshini. Tulipokataa kujiandikisha, tulitupwa gerezani. Tukiwa humo tulikutana na Mashahidi wengine wanne, wawili kati yao walikuwa ndugu zangu wa kimwili. Baada ya kuachiliwa, tulikamatwa na kufungwa tena. Tulifungwa mara tatu, kila tulipoachiliwa tulikamatwa tena baada ya siku moja ua mbili. Kwa ujumla, tulifungwa karibu miaka saba gerezani, na kifungo cha mwisho kilikuwa cha miaka mitano.”

‘Hata tulipochapwa kwa mijeledi au kupigwa kwa fimbo na vitako vya bunduki, tulivumilia yote hayo, kwa kuwa Yehova alitupatia nguvu za kuvumilia’

Maisha ya gerezani yalijaribu sana imani ya akina ndugu. Wafungwa na askari waliwadhihaki usiku na mchana. Mkuu wa gereza la Fort Ozama, ambako mwanzoni akina ndugu walifungwa, alisema: “Mashahidi wa Yehova, mtakapokuwa mashahidi wa Ibilisi, niambieni, ili niwaachilie huru.” Hata hivyo, wapinzani hawakuweza kuvunja utimilifu wa ndugu hao waaminifu. León alieleza sababu: ‘Sikuzote Yehova alitupatia nguvu za kuvumilia na tuliona jinsi alivyoingilia kati na kutusaidia hata katika mambo madogo sana. Hata tulipochapwa kwa mijeledi au kupigwa kwa fimbo na vitako vya bunduki, tulivumilia yote hayo, kwa kuwa Yehova alitupatia nguvu za kuvumilia.’

Mashahidi wa Yehova Wapigwa Marufuku

Katika maeneo mengine nchini, maadui wa ibada ya kweli walizidisha mateso. Hata hivyo, kufikia Mei 1950, mbali na wamishonari, kulikuwa na wahubiri wengine 238 katika Jamhuri ya Dominika. Wahubiri 21 kati yao walikuwa watumishi wa wakati wote.

Picha katika ukurasa wa 97

Makala ya gazeti yenye habari kuhusu hukumu ya kifungo cha gerezani cha ndugu waliokataa kuunga mkono upande wowote

Wakati huohuo, ofisa fulani wa usalama alimwandikia Waziri wa Ofisi ya Rais, akisema: “Waumini wa dhehebu la Mashahidi wa Yehova wameendeleza kwa bidii shughuli zao katika sekta mbalimbali za jiji hili [Ciudad Trujillo].” Kisha akaongezea hivi: “Kwa mara nyingine ninapendekeza kwamba ni lazima Mashahidi wa Yehova wachunguzwe kwa makini kwani mahubiri na shughuli zao zinapotosha maoni ya umma katika sekta fulani, na hasa watu wa kawaida.”

Waziri wa Mambo ya Ndani na Polisi, J. Antonio Hungría, alimtaka Ndugu Brandt awasilishe barua inayoeleza msimamo wa Mashahidi kuhusiana na utumishi wa kijeshi, kupigia bendera saluti, na kulipa kodi. Ndugu Brandt aliandika barua hiyo kwa kutegemea habari zilizo kwenye kitabu “Let God Be True.” Hata hivyo, Juni 21, 1950, Waziri Hungría alitoa tangazo ambalo lilipiga marufuku shughuli za Mashahidi wa Yehova katika Jamhuri ya Dominika. Ndugu Brandt aliitwa kwenye ofisi ya Hungría ili asikilize tangazo hilo likitolewa moja kwa moja. Ndugu Brandt aliuliza ikiwa wamishonari walipaswa kuondoka nchini. Hungría alimhakikishia kwamba wanaweza kubaki ikiwa tu watatii sheria na kuacha kuongea na watu kuhusu dini yao.a

a Majuma machache kabla ya tangazo hilo, makasisi Wakatoliki waliandika makala kadhaa kwenye magazeti wakiwashutumu Mashahidi wa Yehova na kuwahusianisha kwa uwongo na ukomunisti.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki