Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • yb15 uku. 156-uku. 159 fu. 2
  • Matarajio Yenye Kusisimua

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Matarajio Yenye Kusisimua
  • 2015 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
  • Vichwa vidogo
  • Sifa Nzuri
  • Matarajio ya Wakati Ujao
2015 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
yb15 uku. 156-uku. 159 fu. 2
Picha katika ukurasa wa 158, 159

JAMHURI YA DOMINIKA

Matarajio Yenye Kusisimua

Sifa Nzuri

Mashahidi wa Yehova wamekuwa katika Jamhuri ya Dominika kwa miaka 70 hivi. Kwa kipindi hicho chote wamejulikana kuwa wenye sifa nzuri. Mara nyingi watu huwaomba machapisho wanapohubiri, na ni kawaida kuwasikia watu wakisema: “Ninaipenda dini hii” au “Kweli ninyi mnaishi kupatana na Biblia.”

Kwa mfano, fikiria jambo lililotokea baada ya Jumba la Ufalme kujengwa katika uwanja ambao ndugu fulani aliutoa. Ndugu huyo alipoenda kusajili uwanja huo, aligundua kwamba mtu mwingine alikuwa ameusajili, na alidai kwamba ndugu yetu alikuwa akijaribu kumnyang’anya. Kesi hiyo ilipelekwa mahakamani. Ilikuwa kesi ngumu kwa sababu mtu huyo alikuwa na nyaraka alizodai zilithibitisha kwamba alikuwa mmiliki wa ardhi hiyo.

Katika kesi hiyo, hakimu aliuliza ni nani aliyewakilishwa na wakili huyo. Wakili alipomweleza kwamba alikuwa akiwakilisha shirika la Mashahidi wa Yehova, hakimu alijibu hivi: “Kama ni hivyo, hakuna haja ya kutilia shaka ukweli wa madai ya wakili huyo. Ninawajua vizuri Mashahidi wa Yehova, wao ni watu wanyofu. Hawawezi kamwe kumdanganya mtu au kuchukua mali yake.”

Ushahidi ulipotolewa ilikuwa wazi kwamba mshtakiwa alitumia udanganyifu, hivyo hakimu akawapa ushindi Mashahidi wa Yehova. Wakili huyo alisema hivi: “Si kesi hii pekee. Katika mahakama zote nchini, kila mara Mashahidi wa Yehova wanapotajwa, sikuzote wanaheshimiwa sana.”

Matarajio ya Wakati Ujao

Baada ya muda, watu wengi wenye mwelekeo mzuri watajifunza Biblia na kuwa waabudu wa Mungu wa kweli. Kwa sasa tunajitahidi kuwafikia watu hao. Kwa mfano, mwaka wa 2013 Mashahidi wa Yehova katika Jamhuri ya Dominika walitumia zaidi ya saa milioni 11 kuhubiri na kuongoza mafunzo ya Biblia 71,922. Pia, inatia moyo kwamba ndugu na dada 9,776 walishiriki katika kazi ya upainia. Mwezi wa Agosti mwaka huo, wahubiri 35,331 walihubiri. Isitoshe, watu 127,716 walihudhuria Ukumbusho, jambo linatokeza matarajio ya ukuzi mkubwa wa kiroho baadaye.

Kazi ya kuhubiri na kufundisha katika Jamhuri ya Dominika imeendelea kufanywa tangu Jumapili, Aprili 1945, Lennart na Virginia Johnson walipowasili na kuanza kuhubiri habari njema ya Ufalme. Mashahidi wa Yehova katika Jamhuri ya Dominika wanathamini urithi wao mwingi wa kiroho. Wanathamini roho ya kujidhabihu ya waabudu wa kweli wa wakati uliopita. Zaidi ya hayo wanathamini pendeleo la “kutoa ushahidi kamili kuhusiana na Ufalme wa Mungu.” (Matendo 28:23) Wanatazamia kwa hamu siku ambayo watu wote katika kisiwa hicho pamoja na waabudu wenzao ulimwenguni pote wataimba pamoja wimbo huu: “Yehova amekuwa Mfalme! Dunia na ishangilie. Na vile visiwa vingi vishangilie.”—Zaburi 97:1.

Kibanda cha JW.ORG Chapata Matokeo Mazuri

Kibanda kilichowekwa katika maonyesho ya vitabu kiliwavutia wageni 4,723 katika siku 12 tu.

  • Karibu watu 400 walitembelea kibanda hicho kila siku.

  • Watu 265 waliomba kujifunza Biblia.

  • Wageni 1,159 walionyeshwa jinsi ya kutumia Tovuti ya jw.org.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki