Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g90 4/8 kur. 9-10
  • Miujiza na Mizuka—Kwa Nini Haihitajiwi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Miujiza na Mizuka—Kwa Nini Haihitajiwi
  • Amkeni!—1990
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kusudi la Miujiza
  • Njia ya Utambulisho
  • Mizuka Haihitajiwi
  • Kiwango Kile Halisi
  • Je, Kweli Miujiza Hutukia?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Miujiza ya Yesu Unaweza Kujifunza Nini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
  • Kwa Nini Upendezwe na Miujiza?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Kutazama Baadhi ya Miujiza ya Yesu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1990
g90 4/8 kur. 9-10

Miujiza na Mizuka—Kwa Nini Haihitajiwi

ALIPOKUWA duniani, Yesu alifanya miujiza mingi. Alibadili maji yakawa divai, akaandaa chakula kwa ajili ya umati wa watu, akaponya wagonjwa, na kufukuza mashetani. Fundisho la Yesu na uhakika wa kwamba alitimiza unabii mbalimbali wa Biblia kuhusu Mesiya lilisadikisha wengi wa marika wake. Wengine walisababu mambo hivi: “Atakapokuja Kristo, je! atafanya ishara nyingi zaidi kuliko hizi alizozifanya huyu?”—Yohana 7:31.

Kusudi la Miujiza

Miujiza aliyofanya Yesu ilikuwa na kusudi gani? Biblia yaeleza kwamba Yesu alipaswa kuwa ‘nabii kama Musa.’ (Kumbukumbu 18:15, 18) Yehova Mungu alimpa Musa nguvu za kufanya miujiza fulani ili kuthibitisha alikuwa ndiye kiongozi aliyechaguliwa akomboe Waisraeli watoke katika utekwa Misri. (Kutoka 4:1-9, 30, 31) Akiwa sawasawa ‘kama Musa,’ Yesu alifanya miujiza ili kujitambulisha kuwa ndiye Mesiya, kuwa ndiye Mkombozi aliyeahidiwa wa Wayahudi.—Matendo 3:22.

Lakini pia miujiza ya Yesu ilithibitisha kwamba yeye alikuwa amepokea nguvu za pekee kutoka kwa Mungu. Ufalme wa Mungu utawalapo dunia bila kupingwa, Yesu atazitumia kikamili nguvu alizoonyesha kwa kadiri ndogo akiwa duniani. Kutoa kielezi, acheni tuchukue ule muujiza wa mikate na samaki. (Luka 9:12-17) Katika ulimwengu mpya wa Mungu, Yesu atahakikisha kwamba aina ya binadamu yote ina chakula cha kutosha. (Zaburi 72:16) Pia ataponya magonjwa na maradhi yote, hivyo awezeshe wanadamu watiifu kuishi milele. (Ufunuo 21:4) Kwa kufanya mafufuo matatu yaliyoandikwa katika kumbukumbu, yeye alithibitisha ana uwezo wa kuinua mamilioni watoke kwa wafu.—Luka 7:11-17; 8:40-56; Yohana 5:28, 29; 11:11-44.

Njia ya Utambulisho

Sababu nyingine iliyofanya Yehova afanye miujiza kwa ajili ya Israeli ilikuwa kuthibitisha kwa njia isiyoweza kutiliwa shaka lolote kwamba wao walikuwa watu wake wachaguliwa. (Kumbukumbu 4:32-34) Wenye kupata fadhili hizo walikuwa kikundi kizima cha watu, si watu wachache mmoja mmoja wenye kupendelewa.

Vivyo hivyo, miujiza ya karne ya kwanza ilikuwa moja la mathibitisho ya kwamba Yehova alikuwa amehamisha upendeleo wake ukatoka kwenye Israeli wa kimnofu na kuja kwenye kundi la mapema la Kikristo. (Mathayo 21:43; 27:51; Warumi 9:6; 11:7) Ile miujiza mingi iliyofanywa na mitume ilikuwa ushuhuda wa kibali cha Mungu kwa lile kundi likiwa chini ya uongozi wa Mwana wa Mungu, Yesu Kristo.—Matendo 2:22, 43; 4:29, 30; Waebrania 2:3, 4.

Zaidi ya hilo, katika siku hizo, watu walikuwa wakilaza wagonjwa katika mahali mbalimbali ambapo wangeweza kuangukiwa angalau na kivuli cha Petro, na Biblia yataarifu kwamba wale walioletwa kwake “walikuwa wakiponywa wote mmoja mmoja.” (Matendo 5:15, 16, NW) Basi, kwa nini wote wale ambao leo huenda kwenye maabadi wakiwa na imani hawaponywi?

Mizuka Haihitajiwi

Sababu ya msingi ni kwamba ishara na miujiza haihitajiwi tena kuthibitisha kwamba Mungu amehamisha upendeleo wake kutoka kwenye Israeli wa kimnofu ukaja kwenye kundi la kweli la Kikristo. Katika barua moja kwa waandamani wake Wakristo, mtume Paulo alieleza wazi kwamba zawadi za kimuujiza zingeondolewa mbali hatimaye. Wakati ungekuja ambapo hazingekuwa tena njia ya kutambulisha Wakristo wa kweli.—1 Wakorintho 13:8-13.

Hata kuliitia jina la Yesu hakungethibitisha kwamba mtu ni Mkristo wa kweli. Katika Mahubiri ya Mlimani aliyoyatoa, Yesu alitabiri kwamba yeye angekataa watu fulani wenye kudai hivi: “Bwana, Bwana, sisi . . . hatukufanya miujiza mingi kwa jina lako?” Ni kwa sababu gani Yesu angewakataa wafanya miujiza hawa? Yeye ajibu hivi: “Mimi sijapata kamwe kuwajua nyinyi; niondokeeni mbali, nyinyi watu waovu!” Kwa uwazi, baadhi yao wangefanya miujiza kwa jina la Kristo, lakini kwa uhakika wangekuwa walaghai.—Mathayo 7:22, 23, The Jerusalem Bible.

Kiwango Kile Halisi

Kwa sababu ya yaliyotangulia, yawezekanaje kutambua Wakristo wa kweli leo? Yesu aliandaa kiwango alipojulisha hivi: “Mti mwema hauwezi kuzaa matunda mabaya . . . Ndiposa kwa matunda yao mtawatambua.” Siku iliyotangulia kufa kwake, Yesu aliwakumbusha hivi mitume wake: “Mkipendana, watu wote watajua kwamba ninyi ni wanafunzi wangu.” Basi kufanya miujiza siko kungekuwa kiwango milele. Lakini wote wangelazimika kujithibitisha kuwa wanafunzi wa Kristo kwa upendo wao wa kweli.—Mathayo 7:18-20, UV; Yohana 13:34, 35, HNWW.

Kwa hiyo je! imani yako yapasa kuwekwa, hata kwa sehemu ndogo, juu ya msingi wa “miujiza” ambayo hufanywa leo kwa jina la Kristo? Au yapasa kuwekwa kabisa juu ya msingi wa ukweli upatikanao katika Neno la Mungu, Biblia? Ni jambo la maana sana kuchunguza kwa msaada wa Neno la Mungu mwenendo wa wale wanaodai kuwa watumishi wa Mungu.

Katika sehemu zote za ulimwengu leo, ni nani wanaojulisha Neno la Mungu na kujitahidi kuishi kupatana nalo? Ni nani wajulikanao ulimwenguni pote kwa umoja wao? Ni nani wasio na vizuizi vyovyote vya kitaifa, vya kisiasa, vya rangi, au vya kidini miongoni mwao? Ni nani huhubiri kwa bidii zile habari njema za Ufalme wa Mungu? Ikiwa wewe mtu mwenye moyo mweupe una maswali zaidi, Mashahidi wa Yehova watafurahia kukuandalia mambo ya uhakika ambayo wahitaji ili ujihukumie mwenyewe. Tafadhali jihisi ukiwa huru kuonana na Mashahidi katika ujirani wako au kwenye Jumba la Ufalme lao lililo katika eneo lenu. Watakusaidia uweke tegemeo lako katika Yehova na Yesu Kristo, Mwana wake, kwa maana “hakuna wokovu katika mtu yeyote mwingine.”—Matendo 4:12, NW.

[Picha katika ukurasa wa 10]

Miujiza ya kuponya haihitajiwi tena ili kutambulisha kundi la kweli la Kikristo

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki