Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g92 12/8 uku. 11
  • Chagua Uhai Katika Huo Ulimwengu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Chagua Uhai Katika Huo Ulimwengu Mpya
  • Amkeni!—1992
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Una Mambo ya Kuchagua
  • Paradiso Iko Karibu!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2021
  • Yehova Anatupatia Uhuru wa Kuchagua
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Wakati Wako Ujao, Upo Mikononi Mwako!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2018
  • Ulimwengu Mpya Usio na Taabu
    Amkeni!—1991
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1992
g92 12/8 uku. 11

Chagua Uhai Katika Huo Ulimwengu Mpya

BILA shaka, Mungu alikuwa na kusudi katika kuiumba sayari hii ndogo isiyo na kifani, iliyo kama kito. Na alipanga binadamu awe na sehemu ya maana katika hilo. (Isaya 45:18) Hali mbaya sana ya dunia yetu haimletei Mungu heshima. Lakini je! unaamini kwelikweli kwamba ataruhusu hali hiyo iendelee? Bila shaka sivyo!

Tamaa ya mwanadamu ya kupata ulimwengu mpya hasa ni kwa kuitikia tamaa ya jambo fulani ambalo ainabinadamu ilikuwa nayo hapo kwanza. Hiyo ilikuwa paradiso halisi ya kidunia, inayoweza kuonwa. Wenzi wa kwanza wa kibinadamu waliwekwa katika makao kama hayo, na lilikuwa kusudi la awali la Muumba kwamba ainakibinadamu ifurahie Paradiso hiyo duniani milele.—Mwanzo 1:28.

Yehova Mungu sasa anakutolea fursa ya uhai katika ulimwengu wake mpya, ambako atabariki watu waaminifu kwa kuwapa tamaa za mioyo yao. (Zaburi 10:17; 27:4) Je! utachagua kuishi huko?

Una Mambo ya Kuchagua

Waisraeli waliosikia hotuba ya kuaga ya Musa walikuwa na chaguo hilohilo la kufanya. Walilazimika kuchagua ama utawala wa Mungu ama ule wa mataifa ya wakati huo. Hili ndilo lililokuwa shauri la Musa: “Nimekuwekea mbele yako uzima na mauti . . . basi chagua uzima, ili uwe hai, wewe na uzao wako; kumpenda BWANA [Yehova, NW], Mungu wako, kuitii sauti yake, na kushikamana naye.” (Kumbukumbu la Torati 30:19, 20) Naam, chaguo lako ni jambo la uhai au kifo.

Hiyo ndiyo sababu makala hizi kuhusu ulimwengu mpya wa Mungu zimetangazwa—ili kugusa moyo wako hivi kwamba uweze kuuchagua badala ya kuweka tumaini lako katika ahadi tupu za wanadamu za kubuni ulimwengu mpya. Kuna mambo mengi ya kupendeza ambayo unahitaji kujifunza kuhusu ulimwengu mpya wa Mungu.

Kwa mfano, kuna ithibati gani kwamba huo ulimwengu mpya u karibu? Utachukuaje mahali pa serikali zote za dunia? Ni matukio gani yatakayoongoza kwa hayo? Tunaweza kuwaje na uhakika kwamba yale ambayo Biblia inaahidi yatatimia?

Majibu ya maswali hayo na mengine mengi yanapatikana. Mashahidi wa Yehova wangefurahi kukuonyesha mistari katika nakala yako ya Biblia ambayo hueleza, si baraka tu za ulimwengu mpya wa Mungu, bali pia inaonyesha ni lini na jinsi gani hasa serikali ya Mungu inaanza utawala wayo na hatimaye kupanua utawala huo ili kutawala dunia nzima.

Unahimizwa kuitikia kama vile Waberoya wa karne ya kwanza waliomsikiliza mtume Paulo. Walitumia wakati “wakayachunguza maandiko kila siku, waone kwamba mambo hayo ndivyo yalivyo.” (Matendo 17:11) Kwa hekima, unapaswa kufanya vivyohivyo. Uwe na uhakika kwamba mazungumzo yako ya Biblia na Mashahidi wa Yehova yatakuletea uradhi mkubwa wa kiroho unapojifunza kuhusu ule wakati ujao wenye kufurahisha ambao Mungu anatuahidi.

Unahitaji kuchagua—ama kumtumikia Mungu na masilahi ya serikali yake ya Ufalme ama kuweka itibari na tumaini lako katika jitihada za wanadamu za kujitawala wenyewe. Tunakutia moyo ujifunze mengi kadiri uwezayo kuhusu ahadi za Mungu ili kwamba uamuzi wako uwe wenye kutegemea maarifa. Kupata maarifa ya Biblia kutatia nguvu tumaini lako la wakati ujao na pia kutasaidia kukuweka ukiwa hai kiroho kupitia siku za mwisho za utawala wa kibinadamu.—2 Timotheo 1:13.

Miaka mingi ya mwanadamu ya kutamani ulimwengu mpya imekaribia kwisha. Mashahidi wa Yehova wanakutaka upate kibali kuingia katika huo ulimwengu mpya na ufurahie maisha milele. Hilo ndilo Mungu anataka pia. Inatumainiwa kikweli kwamba utachagua ulimwengu mpya wa Mungu. Ukifanya hivyo, basi utaona kwamba tamaa ya ainabinadamu ya kupata ulimwengu mpya haikuwa ya bure kamwe.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki