Wakristo wa Kweli na Vita
YESU aliwaambia wanafunzi wake: “Amri mpya nawapa, Mpendane kama vile nilivyowapenda ninyi, nanyi mpendane vivyo hivyo.” (Yohana 13:34) Je, Wakristo wa kweli waweza kuonyeshana upendo kama huo na wakati uleule waende vitani na kuuana?
Fikiria pia lile swali lililoulizwa na mtume Paulo: “Je! Kristo amengawanyika?” (1 Wakorintho 1:13) Jiulize hivi: Je, kuna mngawanyiko uliomkubwa kuliko ule unaotokea washiriki wa dini moja wanapouana?
Hakika, hatupaswi kushangaa tusomapo ya kwamba Wakristo wa mapema hawakwenda vitani. Encyclopædia of Religion and Ethics inayojulikana ya Hasting ilisema hivi: “Mtazamo huo ulienea kwa wengi wa Wakristo wa mapema ya kwamba vita ni uovu ulioratibiwa ambao Kanisa na wafuasi wa Kristo ni lazima waepuke.”[1]
Wakristo wa mapema waliishi kwa amri ya Yesu ya kupendana. Mwanatheolojia Mjerumani Peter Meinhold alilieza: “Agano Jipya lijapokosa kutoa maelezo kuhusiana na lile swali kama Wakristo wasiwe askari na kama ni lazima waache jeshi wawapo Wakristo, kanisa la kale lilichukua msimamo katika suala hilo. Kuwa Mkristo na askari kulionekana kusikopatana.”[2] Je, kuna yeyote leo anayechukua msimamo kama ule wa “kanisa la kale”?
Kuna Wakristo Wowote wa Kweli Leo?
Encyclopedia Canadiana yasema hivi: “Kazi ya Mashahidi wa Yehova ni urudishaji na uanzilishi upya wa Ukristo uliozoelewa na Yesu na wanafunzi wake katika karne ya kwanza na ya pili ya wakati wetu. . . . Wote ni ndugu.”[3]
Hilo latumikaje? “Mashahidi wa Yehova hudumisha kikamili kutokuwemo katika wakati wa vita,” yaeleza Australian Encyclopædia.[4] Wakiwa mmoja-mmoja huenda wachangue kuchukua msimamo huu, wao hawajihusishi katika mambo ya serikali inayowatawala. Hivyo, hawakuunga mkono vita vya Hitler, na hivyo basi hakuna mmoja wao alihukumiwa katika mahakama ya Nuremberg kama mhalifu wa kivita.
Mjerumani mmoja aliyepatwa na hatia na akahukumiwa kifo alikuwa Alfred Rosenberg, mkuu wa Chama cha Nazi wa idara ya mambo ya kigeni. Akitetea sera ya Nazi ya kuweka Mashahidi wa Yehova katika kambi za mateso, Rosenberg alithibitisha katika jaribio lake hivi: “Kasisi wa jeshi Mwamerika alinipatia kwa fadhili karatasi habari la kanisa ndani ya seli yangu kutoka Columbus [Ohio]. Nikapata kutoka kwalo kwamba pia Marekani, iliwashika Mashahidi wa Yehova katika kipindi cha vita na kufikia Desemba 1945, kulikuwepo 11,000 katika kambi za mateso bado”[5] Ni kweli kwamba Mashahidi wa Yehova wamekosa kuwemo kikamili, bila kuchukua msimamo katika mifoko ya kisiasa. Hawajamwaga damu yoyote, katika vita vya Ulimwengu vya 2 au katika vita vyovyote vile.
Katika Hungaria, mwandishi katika gazeti Ring la Novemba 4, 1992, alisema kuhusu Mashahidi wa Yehova: “Wao watachagua kufa kuliko kuua mtu mwingine. Kwa hivyo, nina uhakika kama Mashahidi wa Yehova wangeishi duniani peke yao hakungetokea vita popote.””[6] Reo M. Christenson, profesa wa sayansi ya siasa, alizungumzia katika The Christian Century kama Mkristo halisi aweza kushiriki katika vita, na aliamua hivi:
“Je, yoyote aweza kuwazia Yesu akirusha gruneti za mkono kwa maadui wake, akitumia bunduki, akitengeneza miali-mrusho, akiangusha mabomu ya nyuklia au akianzisha mrusho wa kombora la ICBM litakaloua au kulemaza maelfu ya akina mama na watoto? Swali hilo liko wazi sana hivi kwamba halihitaji jibu lolote. Ikiwa Yesu hangefanya hivyo na wakati uleule awe mwaminifu, basi twaweza kufanyaje hivyo na tuwe waaminifu kwake”? Ni swali lenye kuchochea kufikiri.
Hata hivyo dini za ulimwengu huendelea kuunga mkono vitani. Wakatoliki huendelea kuua Wakatoliki, na wale wa dini zile zingine ama huuwa watu wa dini zao au washiriki wa makanisa yale mengine. Ili kufuata mafundisho ya Yesu Kristo usadikisho imara na moyo mkuu zahitajiwa, kama kisa kifuatacho cha kweli kinavyoonyesha.
[Picha katika ukurasa wa 7]
Je, yoyote aweza kuwazia Yesu akitumia bunduki vitani?
[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 7]
U.S. National Archives photo