Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g93 4/22 kur. 5-8
  • Kuna Tumaini Gani kwa Mwisho wa Vita?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuna Tumaini Gani kwa Mwisho wa Vita?
  • Amkeni!—1993
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Tumaini Bandia
  • Wale Wanaotimiza Ahadi ya Mungu
  • Jinsi Mwisho wa Vita Utakavyokuja
  • Vita Ambayo Itavimaliza Vita
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Vita
    Amkeni!—2017
  • Amani Ile ya Uhalisi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Karibuni—Ulimwengu Usio na Vita!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1993
g93 4/22 kur. 5-8

Kuna Tumaini Gani kwa Mwisho wa Vita?

VITA YA ULIMWENGU 1, iliyopiganwa kutokea 1914 hadi 1918, iliitwa vita ya kumaliza vita vyote. Lakini tangu wakati huo kumekuwa na zaidi ya vita 200, kutia ndani ile kuu zaidi kufikia leo—Vita ya Ulimwengu 2.

Kwa wazi, jitihada za binadamu kukomesha vita zimeshindwa kabisa. Basi, je, ishangaze kwamba watu wengi husema, “Vita vitakuwapo nyakati zote”? Je! unaamini hivyo?

Kufanyizwa kwa Umoja wa Mataifa katika 1945 baada ya Vita ya ulimwengu 2 kulikusudiwa kuwape binadamu waliochoka na vita tumaini la ulimwengu usio na vita. Tumaini hilo linaloonyeshwa katika mwandiko kwenye ukuta wa ua wa UM katika Jiji la New York, lasema hivi: NAO WATAFUA PANGA ZAO ZIWE MAJEMBE. NA MIKUKI YAO IWE MIUNDU: TAIFA HALITAINUA UPANGA DHIDI YA TAIFA. WALA HAWATAJIFUNZA VITA TENA KAMWE.

Kwa kuhuzunisha, mataifa yamedhihaki tumaini hilo la amani lililoonyeshwa vizuri kwa kupendelea kwao vita. Hata hivyo, maneno hayo yatatimizwa! Hiyo ni kwa sababu kwa zaidi ya miaka 2,500 iliyopita hayo yalitokana na Chanzo kilicho juu zaidi ya wanadamu wasio wakamilifu. Maneno hayo ni ahadi iliyotolewa na Mungu Mweza Yote.—Isaya 2:4.

Tumaini Bandia

Wengi wametumaini makanisa yasaidie kufanyiza ulimwengu usiokuwa na vita. Lakini makanisa yamejithibitisha kuwa yenye kugawanya na yenye kuchochea vita zaidi katika historia. Kwa mfano, Frank P. Crozier, brigedia jenerali wa Uingereza wakati wa Vita ya Ulimwengu 1, alisema hivi: “Makanisa ya Kikristo ndiyo wasababishi wakuu zaidi ya umwagaji-damu ambao tunao na tuliwatumia sana.”

Hivyo, ni muhimu kwamba tupambanue kati ya Ukristo wa kweli na wa bandia. Ili kutusaidia tufanye hivyo, Yesu alitoa kanuni rahisi: “Mtawatambua kwa matunda yao.” (Mathayo 7:16) Maneno, au kazi ya maisha hayatoshi. Ili kufafanua hilo Steve Whysall, mwandikaji wa gazeti la Vancouver Sun, alisema hivi: “Si watu wote wanaovaa ovaroli buluu, zenye uchafu wa mafuta walio mamekanika, hata ikiwa wanafanana na mamekanika, . . . hata wakisema ‘Sisi ni mamekanika.’”

Akitumia kielezo chake kwa Ukristo, Whysall alisema hivi: “Mara nyingi utasikia watu wakisema jinsi jambo hili au lile lilivyofanywa kwa jina la Ukristo na jinsi lilikuwa jambo baya sana kufanywa. Naam, kwa kweli lilikuwa jambo baya sana. . . . Lakini ni nani aliyepata kusema ni Wakristo waliofanya mambo hayo mabaya sana?

“Ah, wasema, makanisa mashuhuri yasema hivyo. Basi, ni nani aliyepata kusema kwamba makanisa mashuhuri ni ya Kikristo?

“Hivyo, papa alimbariki Mussolini, na kuna uthibitisho wa papa wengine waliofanya matendo maovu katika nyakati zilizopita. Basi, ni nani alisema hao ni Wakristo?

“Unafikiri kwamba kwa sababu mtu ni papa ni lazima awe Mkristo? Kwa sababu tu mtu anasema ‘Mimi ni Mkristo’ hakumaanishi kwamba yeye ni Mkristo—kama ilivyo na mtu anayedai kuwa mekanika huenda asiwe mekanika.

“Biblia huwaonya hata Wakristo dhidi ya watu wanaojifanya kuwa ni Wakristo . . . Hakuna Mkristo anayeweza kupiga vita dhidi ya Mkristo mwenzake—ingekuwa ni kama mtu anayejipiga mwenyewe.

“Wakristo wa kweli ni ndugu na dada katika Yesu Kristo. . . . Hawawezi kamwe kuumizana kwa kukusudia.”

Kwa hiyo tunahitaji kutumia kanuni ya Yesu na kutazama matunda ambayo yametokezwa na makanisa. Lakini matunda gani? Biblia yataja moja hususa, ikisema: “Katika hili watoto wa Mungu ni dhahiri, na watoto wa Ibilisi nao. Mtu ye yote asiyetenda haki hatokani na Mungu, wala yeye asiyempenda ndugu yake. Maana, hii ndiyo habari mliyoisikia tangu mwanzo, kwamba tupendane sisi kwa sisi; si kama Kaini alivyokuwa wa yule mwovu, akamwua ndugu yake.”—1 Yohana 3:10-12.

Badala ya kutia moyo upendo kwa ndugu zao, makanisa yameunga mkono na hata kuendeleza uuaji wa ndugu zao vitani. Hivyo, yametumiwa na Shetani Ibilisi kama tu ilivyokuwa kwa hakika zile dini za Wamisri, Waashuru, wale waliokuwa wakatili, na Waroma wa kale. Yesu Kristo alimwita Shetani “mkuu wa ulimwengu huu” na kusema hivi kuhusu wafuasi Wake wa kweli: “Wao si wa ulimwengu, kama mimi nisivyo wa ulimwengu.” (Yohana 12:31; 17:16; 2 Wakorintho 4:4) Na bado, makanisa yamekuwa sehemu muhimu ya ulimwengu huu.

Kwa wazi basi, Mungu hatumii makanisa ili kutimiza kusudi lake la kufanyiza ulimwengu usiokuwa na vita. Hata makasisi wa kijeshi na wawakilishi wengine wa kanisa waseme nini, Mungu haungi mkono upande wowote katika vita vya mataifa.

Basi ahadi ya Mungu ya kuondoa vita itatimizwaje? Je! kuna watu wowote ambao kwa kweli wamefua panga zao kuwa majembe? Kwa kweli kunao.

Wale Wanaotimiza Ahadi ya Mungu

Mwanahistoria mashuhuri wa kanisa C. J. Cadoux alitaja hivi: “Wakristo wa mapema walitii maneno ya Yesu . . . Walitambulisha dini yao kwa ukaribu sana na amani; walishutumu vita kwa ukali kwa sababu ya umwagaji damu uliohusika; walijipatanisha na unabii wa Agano la Kale uliotabiri kugeuzwa kwa silaha za vita kuwa vifaa vya kilimo.”—Isaya 2:4.

Lakini vipi leo? Je! kuna watu wanaotii maneno ya Yesu na kupendana kikweli? Je! hao kwa kweli wamefua panga zao kuwa majembe? Basi, Encyclopedia Canadiana yaonelea hivi: “Kazi ya Mashahidi wa Yehova ni kuanzishwa na kusimamishwa upya kwa Ukristo wa kale uliozoewa na Yesu na wafuasi wake wakati wa karne ya kwanza na ya pili ya wakati wetu. . . Wote ni ndugu.”

Hivyo, wakitii amri ya Yesu ya kupendana, Mashahidi wa Yehova hukataa kuchukia au kuua ndugu zao, hata ingawa wao huenda wakawa wa kabila au taifa jingine. (Yohana 13:34, 35) Martin Niemoeller, kiongozi wa Protestanti katika Ujerumani, alitaja kwamba “katika enzi zote zilizopita, [makanisa] yamekubali sikuzote kubariki vita, wanajeshi na silaha na kwamba yaliomba kwa njia isiyo ya Kikristo kabisa kuangamizwa kwa maadui wao.” Na kwa kutofautisha, alisema, Mashahidi “wameenda katika kambi za mateso kwa mamia na maelfu na kufa kwa sababu walikataa kutumika vitani na kukataa kupiga risasi wanadamu.”

Ndiyo, tofauti na watu wa dini nyinginezo, Mashahidi wa Yehova kwa kweli wamefua panga zao zikawa majembe. Kwa kubaki wakiwa “si sehemu ya ulimwengu huu,” kama Kristo alivyoelekeza, kwa kweli wao ni tofauti na dini nyinginezo. (Yohana 15:19) Kichapo cha Roma Katoliki St. Antony’s Messenger kilionelea hivi: “Mashahidi wa Yehova huwa tofauti na ‘mfumo wa dini’ na hukataa wajibu wa kubariki chochote serikali ya kilimwengu inaamua kufanya.”

Kwa hiyo, Je, ahadi ya Mungu inayohusu kuondolewa kwa silaha itatimizwa kwa sababu tu mamilioni machache ya watu kutoka kwa mataifa yote wanafua panga zao kuwa majembe? Bila shaka sivyo! Ahadi ya Mungu itatimizwa kwa njia yenye utukufu zaidi na yenye kutazamisha zaidi.

Jinsi Mwisho wa Vita Utakavyokuja

Muumba, Yehova Mungu, atakomesha vita kwa kuondoa kabisa vifaa vyote vya vita na wale wanaosababisha vita. Mtunga zaburi mmoja wa Biblia aliwaalika wasomaji wafikirie tarajio hili linalopendeza. “Njoni,” aliandika, “myatazame matendo ya BWANA [Yehova, NW], jinsi alivyofanya ukiwa katika nchi. Avikomesha vita hata mwisho wa dunia.” (Zaburi 46:8, 9) Ni tangazo lenye kutokeza na kuchochea kama nini!

Je! tarajio la ulimwengu usiokuwa na vita ni nzuri sana hivi kwamba haliwezekani? Watu wenye mashaka huenda wakafikiria hivyo. Hata yule mwanahistoria wa vita ambaye masimulizi yake yako katika kurasa 9 hadi 13 za gazeti hili alifikiri hivyo. Lakini alichukua wakati achunguze uthibitisho kwa uangalifu. Matokeo yakawa kwamba, alijithibitishia kwamba kwa kweli Biblia inategemeka. Aligundua kwamba unabii mbalimbali unaohusu matukio ya mapema ya historia ulitimizwa bila kukosa, kwa wakati barabara. Jambo hilo lilimpa sababu ya kuamini kwamba yale matukio yaliyotabiriwa na ambayo hayajatukia yatatimizwa kwa wakati barabara.

Kwa mfano, fikiria jinsi matukio makubwa yanayotendeka sasa yanavyopatana kabisa na matukio yaliyotabiriwa na Biblia kwamba yangetia alama siku za mwisho za mfumo huu wa mambo. (Mathayo 24:3-14; 2 Timotheo 3:1-5) Hilo lamaanisha kwamba sasa tunaishi katika wakati wa kuja kwa Ufalme wa Mungu, katika utimizo wa sala ambayo Yesu aliwafunza wafuasi wake, yaani: “Baba yetu uliye mbinguni, jina lako litukuzwe, ufalme wako uje, mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni.”—Mathayo 6:9, 10.

Tunatazamia Ufalme wa Mungu uje kwa njia gani? Unabii mmoja wa Biblia wasema hivi kuhusu jambo hilo: “Na katika siku za wafalme hao [yaani, serikali zile zinazotawala sasa] Mungu wa mbinguni atausimamisha ufalme ambao hautaangamizwa milele, wala watu wengine hawataachiwa enzi yake; bali utavunja falme [au, serikali] hizi zote vipande vipande na kuziharibu, nao [serikali ya Ufalme wa Mungu] utasimama milele na milele.”—Danieli 2:44.

Ndiyo, Ufalme wa Mungu utakuja katika njia yenye kutazamisha ili uondoe serikali zote za sasa, kama vile Gharika ya duniani pote iliyotabiriwa ilivyokuja katika siku za Noa. (Mathayo 24:36-39; 1 Yohana 2:17) Kwa sababu ya uangamivu unaokaribia sana wa serikali za sasa, pamoja na dini zinazoziunga mkono, ni muhimu kwamba sisi sote tuchunguze hali yetu. Je! tutatia bidii tujifunze juu ya Yehova Mungu na Mwanae, Yesu Kristo, na kisha tufanye wanayotutaka tufanye? (Yohana 17:3) Je! tutapendana, tukikataa kudhuru binadamu mwenzetu, na hivyo kuonyesha kwamba tumefua panga zetu kuwa majembe?

Ikiwa unakubali kwamba vita havina maana na kwamba ungependa kuishi katika dunia yenye amani inayoenea kotekote, basi wasiliana na Mashahidi wa Yehova. Watafurahi kukusaidia ujifunze zaidi jinsi vita vitaondolewa hivi karibuni, chini ya utawala wa Ufalme wa Mungu.

[Sanduku katika ukurasa wa 7]

Mipango ya Himmler kwa Mashahidi wa Yehova

HEINRICH Himmler alikuwa mkuu wa polisi wa Nazi walioitwa SS, au Kikosi Maalumu cha Polisi, na wakati wa Vita ya Ulimwengu 2 alikuwa mtu wa pili kwa ukuu katika Ujerumani, akifuata Adolf Hitler. Ingawa Himmler alichukia Mashahidi wa Yehova kwa sababu walikataa kushiriki katika mipango ya Nazi ya ushindi wa ulimwengu, alikuja kuwastahi. Katika mojapo barua zake kwa mkuu wa Gestapo Ernst Kaltenbrunner, Himmler aliandika hivi:

“Habari na uchunguzi fulani wa hivi karibuni umeniongoza nifanye mipango ambayo ningependa kukujulisha. Hiyo inahusu Mashahidi wa Yehova. . . . Tutatawala na kutiisha Urusi kwa njia gani . . . tutakapokuwa tumeshinda sehemu kubwa-kubwa za eneo yayo? . . . Aina zote za dini na madhehebu yenye kupendelea amani ni lazima yaungwe mkono . . . , miongoni mwa mengine ni itikadi za Mashahidi wa Yehova. Ni jambo linalojulikana wazi kwamba hao wa mwisho [Mashahidi wa Yehova] wana tabia ambazo zinaweza kutufaa sana: Licha ya uhakika wa kwamba wao hukataa utumishi wa kijeshi na chochote kinachohusu vita . . . , wanategemeka sana, hawanywi, hawavuti sigareti; ni wafanyakazi wenye bidii na ni wanyoofu sana. Kwao maneno ya mdomo yanatosha. Hizo ni tabia zinazofaa sana . . . , sifa zenye kutamaniwa.”

La, Himmler hakutaka sifa za Mashahidi wenye kupenda amani kwa ajili yake mwenyewe au kwa watu wake, bali alitaka Warusi wawe na sifa hizo nzuri. Hilo lingewafanya wawe watu wenye amani, likiwafanya wafue panga zao kuwa majembe.

[Picha katika ukurasa wa 8]

Ufalme wa Mungu utaondoa vifaa vyote vya vita na kuingiza watu katika ulimwengu mpya wenye amani

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki