Amani Ile ya Uhalisi
NI WATU wachache tu ambao wangechambua mawazo yenye kuongoza jitihada za Umoja wa Mataifa kutafuta amani. “[Yale maneno yasemayo] ‘Na Tufue Panga Ziwe Plau za Kulimia’ yataja mradi wa Umoja wa Mataifa kuleta amani ya ulimwengu,“yasema “The WorId Book Encyclopedia,” ikiongezea kwamba, “Umoja wa Mataifa una miradi miwili mikubwa: kuleta amani na kudumisha heshima ya kibinadamu.“
Maandishi yaliyo chini ya sanamu iliyoonyeshwa hapa yafafanua maneno ya unabii wa Biblia kwenye Isaya sura ya 2, mstari wa 4. Maneno hayo yasomwa hivi, kulingana na tafsiri moja ya ki-siku-hizi:
“Nao watalazimika kufua panga zao ziwe plau za kulimia na mikuki yao iwe makasi ya kupogolea.”
Hakika maneno haya yenye adhama yangalipasa kuvuvia mataifa yaliyo washirika wa UM yajipatie amani ya kudumu na kuondoa silaha daima. Lakini, kwa kuhuzunisha, tangu ilipoanzishwa kwenye umalizio wa vita ya ulimwengu ya pili katika 1945, historia ya UM imefunua kwamba mambo ni mengine. Kwa nini? Hasa kwa sababu maneno yaliyo juu yaliyonukuliwa kutoka Isaya hayawezi kufuatwa kwa kuyatenganisha na yale mengine yenye kuambatana nayo, kama vile serikali za kibinadamu zimeyatenganisha. Habari zenye kuzunguka maneno hayo ni za maana kabisa. Fikiria sababu.
Ujumbe wa Isaya
Isaya alikuwa nabii. Yeye anena juu ya njozi tukufu ya upatano na amani kwa ajili ya watu wa rangi zote. Ili njozi hii iwe uhalisi, ni lazima watu wafanye jambo fulani. Jambo gani? Fikiria maana kuu ionyeshwayo na mistari ya 2 na 3 kwa kuhusiana na mstari wa 4.
“[2] Na lazima itukie katika sehemu ya mwisho ya zile siku kwamba mlima wa nyumba ya Yehova utakuwa wenye kuthibitishwa imara juu ya kileleta cha milima, nao kwa uhakika utainuliwa juu ya vilima; na ni lazima mataifa yote yamiminike kuuendea. [3] Na vikundi vingi vya watu kwa uhakika vitaenda na kusema: ‘Njoni, nyinyi watu, na acheni twende juu kwenye mlima wa Yehova, kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo; na yeye atatuagiza kuhusu njia zake, na sisi tutatembea katika vijia vyake.’ Kwa maana kutoka Sayuni sheria itatokeza mbele, na neno la Yehova kutoka Yerusalemu. [4] Na yeye kwa uhakika atatoa hukumu miongoni mwa mataifa na kunyoosha mambo kwa habari ya vikundi vingi vya watu. Na wao watalazimika kufua panga zao ziwe plau za kulimia na mikuki yao iwe makasi ya kupogolea. Taifa halitainua upanga dhidi ya taifa, wala hawatajifunza vita tena.“
Kwanza, ni lazima sisi tukiri kwamba Muumba wetu, Yehova, ana haki ya kutuagiza “kuhusu njia zake,“ambazo, kama vile Isaya alivyoandika baadaye, ziko ‘juu kuliko njia zetu.’ (Isaya 55:9) Watu wengi, hasa viongozi wa ulimwengu wenye kujihesabu wenyewe kuwa mashuhuri, huona ikiwa vigumu kukiri hivyo. Njia zao wenyewe ndizo tu zilizo sawa machoni pao wenyewe. Na bado, uhakika wa kwamba njia zao hazijaongoza kwenye amani ya ulimwengu wala kwenye ondoleo la silaha zaonyesha kwa uhakika kwamba ni ubatili kuendelea kufuatia mwendo huo.
Pili, angalia tamaa yenye hamu nyingi ya watu mmoja mmoja kujipatanisha na sheria za Mungu: “Sisi tutatembea katika vijia vyake.“Ni kwa msingi huo tu kwamba panga zitafuliwa ziwe plau za kulimia na mikuki iwe makasi ya kupogolea duniani pote. Ni jinsi gani mradi huo wenye kutamaniwa sana waweza kuja kufikiliwa?
Maagizo ya Kimungu
Watu wengi wana nakala ya Biblia, kile kitabu kilicho na maagizo ya Yehova Mungu, lakini mengi zaidi yatakwa kuliko kuwa nacho tu. Isaya asema kwamba sheria na maneno ya Yehova yatokana na “Yerusalemu.“Hiyo yamaanisha nini? Katika siku ya Isaya, lile jiji halisi lilikuwa ndicho chanzo cha mamlaka ya kifalme iliyotegemewa na Waisraeli wote waaminifu. (Isaya 60:14) Baadaye, wakati wa mitume wa Yesu Kristo, Yerusalemu palikuwa pangali ndipo mahali pakuu pa maagizo yenye kutoka kwa baraza lenye kuongoza la Kikristo lililokuwa katika jiji hilo.—Matendo 15:2; 16:4.
Namna gani leo? Angalia kwamba Isaya atanguliza dibaji ya ujumbe wake kwa taarifa hii: “Ni lazima itukie katika sehemu ya mwisho ya zile siku.” Tafsiri nyinginezo husema: “Katika siku za mwisho.” (Union Version) Ushuhuda hutokezwa kwa ukawaida katika kurasa za gazeti hili kuunga mkono jambo la kwamba tumekuwa tukiishi katika siku za mwisho za taratibu hii ya sasa ya mambo ya ulimwengu tangu 1914. Kwa hiyo, yatupasa tutarajie kuona nini, kulingana na mistari ya 3 na 4?
Umati mkubwa wa watu ambao hawajifunzi vita tena na ambao tayari wamefua ‘panga zao zikawa plau za kulimia.’ Na kweli twawaona! Wanaume, wanawake, na watoto wa rangi zote ambao ni zaidi ya milioni 3.5 katika mabara zaidi ya 200 wamejiunga kwa upatano mmoja, wakiishi kwa amani mmoja na mwenzake na kuhubiria jirani zao ujumbe wa Biblia wa amani. Wao wajulikana katika sehemu zote za ulimwengu kuwa Mashahidi wa Yehova.
Wao wana Baraza Linaloongoza la ki-siku-hizi la wanaume wazee walio Wakristo kutoka sehemu mbalimbali za dunia ambao hutoa uangalizi wenye kuhitajiwa kwa utendaji mbalimbali wa watu wa Mungu ulimwenguni pote. Wanaume hawa, kama wale mitume na wanaume wazee katika Yerusalemu katika karne ya kwanza, ni washirika wapakwa-mafuta wa jamii ya mtumwa mwaminifu mwenye uangalifu aliyewekwa na Yesu kutunza masilahi yake yote ya Ufalme hapa duniani. Historia imethibitisha kwamba wao waweza kuaminiwa wafuate mwelekezo wa roho takatifu na kwamba hawategemei hekima ya kibinadamu katika kulifundisha kundi la kondoo za Mungu njia za amani ya kweli.—Mathayo 24:45-47; 1 Petro 5:1-4.
Ibada ya Kweli
Kuishi kwa amani kwahusisha mengi kuliko kuwa na maarifa ya kichwani tu au hata tamaa ya kuishi kulingana na maagizo ya kimungu. Ujitoaji wa moyoni na ibada kwa Muumba wetu, Yehova, yahitajiwa sana, kama vile Isaya aonyesha wazi pia.
Nabii ataarifu kwamba “mlima wa nyumba ya Yehova utakuwa wenye kuthibitishwa imara juu ya kileleta cha milima” na “utainuliwa juu ya vilima.” Nyakati za kale, milima na vilima fulani vilitumika kuwa nyanja za ibada ya sanamu na maabadi matakatifu ya miungu bandia. Mfalme Daudi alipoleta lile Sanduku takatifu kwenye hema alilokuwa amepiga juu ya Mlima Sayuni (Yerusalemu), meta 760 hivi juu ya usawa wa bahari, kwa uwazi yeye alikuwa akitenda kupatana na mwelekezo wa kimungu. Baadaye, wakati lile hekalu kubwa la Yehova lilipojengwa juu ya Mlima Moria, mtajo “Sayuni” ukaja kuhusisha ndani uwanja wa hekalu, kwa hiyo hekalu lilikuwa na mwinuko ulio juu kuliko baadhi ya mahali-mahali pa kipagani palipolizunguka. Yerusalemu lenyewe liliitwa pia “mlima mtakatifu” wake; hivyo, ibada ya Yehova ilibaki katika cheo kilichokwezwa. —Isaya 8:18; 66:20.
Kwa hiyo leo, ibada ya Yehova Mungu imekuwa yenye kuinuka kama mlima wa ufananisho. Imeinuka juu kwa umashuhuri kwa njia yenye kuonekana na wote, kwa maana imefanya jambo ambalo hakuna dini nyingine imeweza kulifanya. Jambo gani hilo? Imeungamanisha vizuri waabudu wote wa Yehova, ambao wameterema kufua panga zao zikawa plau za kulimia na hawajifunzi vita tena. Vizuizi vya kitaifa na vya rangi haviwagawanyi tena. Wao huishi wakiwa kikundi cha watu walioungamana, udugu mmoja, hata ingawa wametapakaa sehemu zote za mataifa ya ulimwengu.—Zaburi 33:12.
Wakati wa Uamuzi
Yote haya yakuathiri wewe jinsi gani? Maneno ya nabii mwingine Mwebrania yafaa sana: “Makutano makubwa, makutano makubwa, wamo katika bonde la kukata maneno [la uamuzi, NW]! kwa maana siku ya Bwana [Yehova, NW] i karibu, katika bonde la kukata maneno.” (Yoeli 3:14) Ni wakati wa haraka wa kufanya azimio kwa aina ya binadamu yote, ama wa kujifunza njia za amani ya kweli mkononi mwa Mungu au kuendelea kuunga mkono maisha yenye kutegemea silaha ambayo yataisha karibuni.
Yesu alitabiri kwamba kazi kubwa ya kuhubiri ingefanywa katika siku yetu. Uhubiri huo wahusu “habari njema” za kwamba Ufalme wa Mungu utayaletea amani mataifa yenye kukumbwa sana na vita. (Mathayo 24:14) Mwaka jana mafunzo ya nyumbani ya Biblia yenye kuzidi sana milioni tatu yaliongozwa na Mashahidi wa Yehova kwa ukawaida katika sehemu zote za ulimwengu. Baadhi ya mafunzo haya ya kila juma yalifanywa pamoja na watu mmoja mmoja, lakini mengi yalifanywa pamoja na vikundi vya jamaa. Kwa njia hiyo mamilioni ya watoto wanapewa tumaini hakika kwa wakati ujao wao, na wazazi wao wapata uhakikishio wa kwamba vita, kama vile ambavyo wameshuhudia na labda hata wakavishiriki, havitakuwa sehemu ya ulimwengu mpya wenye kufanyizwa na Yehova Mungu.
Lo, huo utakuwa ulimwengu wa uaminiano na amani iliyoje! Wasiwasi hautahitajiwa kuhusu kuondoa silaha, kwa maana silaha za vita zitakuwa vitu vya zamani. Nazo shukrani zote zimwendee Yehova, “yule Mungu apaye amani,” ambaye atuagiza sasa ili tupate kujitayarisha kuishi maisha yenye ukamili chini ya Ufalme wake wa uadilifu.—Warumi 15:33.