Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g95 5/8 kur. 26-27
  • Ni Nini Maana ya Uhai?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ni Nini Maana ya Uhai?
  • Amkeni!—1995
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • “Kani ya Msingi Ihamasishayo”
  • Uvumbuzi wa Sulemani Wahakikishwa na Yesu
  • Kuvumbua Maana ya Uhai
  • “Kwa Jumla Ndiyo Impasayo Mtu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Uhai Wako—Kusudi Lao ni Nini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Je! Wewe Unayatumiaje Maisha Yako?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Ni Nini Kinachofanya Maisha Yawe Yenye Kusudi?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1995
g95 5/8 kur. 26-27

Maoni ya Biblia

Ni Nini Maana ya Uhai?

“WANANADHARIA YA DARWIN HUBISHA KWAMBA UTEUZI ASILIA NI MAELEZO YALIYOTOSHA YA UHAI WA KIKABONI. HATA HIVYO LAONEKANA KUWA JAMBO LA KIAKILI KWAMBA, IKIWA KIUMBE HAI CHAKUA KUELEKEA UTATA MKUBWA, KUJIELEWA NA KUWA NA AKILI, BASI NI KWA SABABU SIFA HIZO ZATAKIWA.”—DYLAN THOMAS (1914-1953, MSHAIRI NA MWANDISHI WA WELSH).

UTAFUTAJI wa maana ya uhai si mpya. Umeshughulisha akili za wadadisi kwa karne nyingi. Uchunguzi wa hivi majuzi waonyesha kwamba umo akilini mwa watu wa New Zealand zaidi leo kuliko miaka kumi iliyopita. Asilimia 49 ya idadi ya watu, walio na umri wa miaka 15 na wakubwa zaidi, yasema ripoti iliyochapishwa katika Listener, “walifikiri juu ya maana ya uhai mara nyingi,” ambayo ni ongezeko kutoka asilimia 32 wakati uchunguzi kama huo ulipofanywa katika 1985.

Watu wa New Zealand yaelekea wanaonyesha hisia wanazoshiriki watu wa mataifa mengine. Listener laendelea hivi: “Mwelekeo wenye kuendelea wa kushuku umaana wa kuwako kwetu huenda ukaonyesha kwamba tunahangaika zaidi sasa kuliko tulivyohangaika katika miaka ya 1980, bila kuwa na uhakika kamili wa mkondo upaswao kuchukuliwa.”

Kwa msingi wa uthibitisho ulioko, majibu yanayotolewa na wanamageuzi kwa swali la ulimwengu wote, Kwa nini tupo hapa? hayaridhishi kwa idadi inayoongezeka ya watu. Je, Biblia yaweza kuandaa dira ya maadili inayohitajika ili kupata maana katika maisha ya mtu?

“Kani ya Msingi Ihamasishayo”

Kati ya viumbe vyote vya dunia, ni mwanadamu tu hufikiria kusudi la uhai. Je, wajua ni kwa nini? Biblia hutoa sababu moja kwenye Mhubiri 3:11. Kuhusu Muumba, yasema hivi: “Amewapa wanadamu ufahamu wa wakati uliopita na ujao.” (The New English Bible) Ingawaje vitu vyote vinavyoishi huelekea kushikamana na uhai, yaelekea kwamba mwanadamu ni wa kipekee katika kuwa na wazo la wakati—uliopita, wa sasa, na ujao. Mwanadamu aweza kutafakari juu ya wakati uliopita na kutazama kuelekea wakati ujao, akiupangia, ndiyo, hata akitamani sana kushiriki katika huo. Na anaweza kuvunjika moyo asipoweza kupata matazamio yake kuhusu wakati ujao kwa sababu ya asili ya ufupi wa urefu wa maisha yake.

Kwa hiyo, ni mwanadamu peke yake huuliza maswali, Kwa nini nipo hapa? Ninaelekea wapi? Mwanatiba ya akili Viktor Frankl aliandika hivi: “Kule kujikakamua kutafuta maana katika maisha ya mtu ni kani ya msingi ihamasishayo katika mwanadamu. . . . Hakuna chochote katika ulimwengu, najihatarisha kusema, ambacho kingesaidia mtu kwa matokeo hata katika hali mbaya kabisa, kama ujuzi kwamba kuna maana katika maisha ya mtu.”

Uvumbuzi wa Sulemani Wahakikishwa na Yesu

Uhitaji wa kutafuta maana katika maisha ulichochea watu wa kale. Acheni tupindue kurasa za historia nyuma hadi miaka elfu tatu kwenye ufalme wa Israeli chini ya utawala wa Sulemani. Kumhusu, Malkia wa Sheba alisema hivi: “Ndizo kweli habari zile nilizozisikia katika nchi yangu za mambo yako na za hekima yako. Lakini mimi sikuzisadiki habari hizo, hata nilipokuja na kuona kwa macho yangu; tena, tazama, sikuambiwa nusu; wewe umezidi kwa hekima na kufanikiwa kuliko habari nilizozisikia.”—1 Wafalme 10:6, 7.

Katika kuandika kitabu cha Biblia cha Mhubiri, Mfalme Sulemani alijulisha wasomaji wake matokeo ya jaribio alilofanya ili kuangaza kusudi la uhai. Lilikuwa jaribio katika fursa za kufurahia maisha ambayo yanafaa mfalme halisi wa Mashariki ya kale. Katika sura ya 2, mistari ya 1-10, alifafanua kwa mwandiko maisha ya raha yasiyowazika. Yeye alijaribu kila kitu ambacho maisha yalitoa kuhusu utajiri wa kimwili na raha za kimwili. Changanuo lake la umaana wa mifuatio hiyo lilikuwa nini? Jibu lake lapaswa kushangaza wajiaminio mno.

Alipotazama nyuma kwa kutafakari yaliyopita juu ya vitu vyote hivi, uamuzi wake mara nyingi ulikuwa hasi. Yalikuwa bure, kupoteza wakati. Yeye aliandika hivi: “Nikaziangalia kazi zote zilizofanywa kwa mikono yangu, na taabu yote niliyotaabika katika kuzitenda; na tazama, yote ni ubatili na kujilisha upepo, wala faida hakuna chini ya jua.”—Mhubiri 2:11.

Yeye alifikia mkataa kwamba, katika hali nzuri zaidi, anasa za kidunia huleta raha ya muda tu. Hata hekima ya kibinadamu haiwezi kuokoa mwanadamu kutoka kwenye maumivu na uchungu wa maisha.

Yesu Kristo alifikia mkataa vivyohivyo wakati, katika kuitikia hangaiko la kupita kiasi la mtu mmoja juu ya urithi wa kimwili, alisema kwa umati uliokuwa ukisikia: “Angalieni, jilindeni na choyo, maana uzima wa mtu haumo katika wingi wa vitu vyake alivyo navyo.”—Luka 12:15.

Ni Yehova Mungu pekee anayeweza kushinda udhaifu wa kibinadamu katika maisha ya kila siku na kutoa kusudi lenye hekima kwa matendo ya mwanadamu. Kwa hiyo, maisha bila Mungu ni bure. Kama ilivyorekodiwa kwenye Mhubiri 12:13 (NW), Sulemani alieleza hivi: “Mkataa wa mambo, yote yakiwa yamekwisha sikiwa, ni: Mhofu Mungu wa kweli na uzishike amri zake. Kwa kuwa huu ndio wajibu wote wa mwanadamu.”

Kuvumbua Maana ya Uhai

Uamuzi wa Sulemani kwamba maana ya uhai haiwezi kutenganishwa kutoka hofu inayofaa ya Mungu ulihakikishwa na Yesu Kristo kwa kurudia. “Imeandikwa,” Yesu akasema, akinukuu Neno la Mungu, “Mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu.” (Mathayo 4:4; Kumbukumbu la Torati 8:3) Ndiyo, ili maisha ya mtu yaridhishe, mambo ya kiroho hayawezi kupuuzwa. Kuhusu yeye mwenyewe, Yesu alisema hivi zaidi: “Chakula changu ndicho hiki, niyatende mapenzi yake aliyenipeleka, nikaimalize kazi yake.” (Yohana 4:34) Kumtumikia Baba yake wa kimbingu kwa utii kulikuwa chanzo cha shangwe na uradhi. Kulimjenga. Kulitoa kusudi kwa maisha yake.

Hivyo basi, je, uhai waweza kufikia uwezo wake kamili bila Mungu? La! Kwa kupendeza, mwanahistoria Arnold Toynbee aliandika hivi wakati mmoja: “Kusudi la kweli la dini safi ni kueneza mashauri ya kiroho na kweli ambazo ndizo msingi wazo kwa nafsi nyingi kadiri iwezavyo kufikia, ili kwamba kila moja ya nafsi hizi iweze kutimiza kusudi la kweli la Mwanadamu. Kusudi la mwanadamu la kweli ni kumtukuza Mungu na Kumfurahia milele.” Nabii Malaki alionyesha maoni ya Mungu hivi: “Nanyi mtapambanua kati ya wenye haki na waovu, na kati ya yeye amtumikiaye Mungu na yeye asiyemtumikia.”—Malaki 3:18.

[Picha katika ukurasa wa 26]

“The Thinker,” na Rodin

[Credite Line]

Scala/Art Resource, N.Y.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki