Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g95 7/8 kur. 25-27
  • Je, Haidhuru Hata Uamini Nini?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Haidhuru Hata Uamini Nini?
  • Amkeni!—1995
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Itikadi Huathiri Mwenendo?
  • Kwa Nini Sisi Twahitaji Maarifa Sahihi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Imani Yako Inategemea Nini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Je, Kuwa na Imani Kunapatana na Mambo Hakika?
    Amkeni!—2011
  • Timotheo Anapata Mashauri kwa Mwanamume Mzee
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1995
g95 7/8 kur. 25-27

Maoni ya Biblia

Je, Haidhuru Hata Uamini Nini?

“MWANADAMU HUPENDELEA KUAMINI KILE AONELEACHO KUWA KWELI.”—FRANCIS BACON, 1561-1626, MTUNGA-INSHA MWINGEREZA NA WAZIRI.

KUHUSIANA na mafundisho ya kidini, watu wengi wanahisi kwamba mradi mtu anaamini kwa unyofu kwamba ‘kuna Mtu Fulani kule juu’ na ikiwa anampenda mwanadamu mwenzake, kwa kweli haidhuru mambo mengine anayoamini mtu. Wengine huenda wakatazama dhana zenye kupingana ambazo vikundi vya kidini hutetea kuhusu Mungu, kusudi lake, na jinsi ya kumwabudu na kufikia mkataa kwamba tofauti hizo ni za kijuu-juu tu, kama vile mitindo tofauti ya mavazi yavaliwayo na mtu yule yule. Huenda hata wakahisi kwamba wale ambao wanabishania tofauti kama hizo wamekosa kabisa ile roho ya Ukristo wa kweli.

Maandiko yanakubali kwamba si mazungumzo yote ya mafundisho ya kidini yafaayo. Kwa kielelezo, katika barua zake zilizopuliziwa kwa Timotheo, mtume Paulo alirejezea wanaume waliochochea “mabishano makali mno juu ya mambo hafifu.” Paulo aliwafafanua kuwa “wenye maradhi ya kiakili juu ya maswali-maswali na mashindano juu ya maneno.” (1 Timotheo 6:4, 5, NW) Yeye alimwagiza Timotheo “akatae maswali-maswali ya upumbavu na yasiyo na ujuzi, akijua hayo hutokeza mapigano,” na aagize makutaniko “yasipigane kuhusiana na maneno, ambalo ni jambo lisilofaa kamwe.” (2 Timotheo 2:14, 23, NW) Mijadala mingi ya kidini katika wakati wetu imefaana na ufafanuzi huu na imethibitika kuwa upotezo usiokuwa na maana wa wakati.

Ingawa hivyo, je, hilo lamaanisha kwamba mazungumzo yote ya itikadi za kidini hayana maana? Hatungeacha kuvaa nguo kabisa kwa sababu tu nguo fulani hazifai kuvaliwa, au sivyo? Kwa hiyo kwa nini tuache kwa kuiona kuwa isiyofaa mada yote ya itikadi za kidini eti kwa sababu maswali fulani ya kimafundisho hayastahiki kufikiriwa? Muktadha wa maneno ya Paulo yaliyonukuliwa hapo juu unaonyesha kwamba yeye aliona suala la kimafundisho kuwa la ufikirio muhimu sana. Yeye alionya kwa kurudia-rudia kwamba mafundisho bandia yangeweza kutokeza kuongozwa kando kwa mtu kutoka kwenye imani, na akamwagiza Timotheo ‘awaamuru watu fulani kutofundisha fundisho tofauti.’ (1 Timotheo 1:3-7; 4:1; 6:3-5; 2 Timotheo 2:14-18, 23-26; 4:3, 4, NW) Kwa hakika, hangelifanya taarifa hizo zenye mkazo isipokuwa kile walichoamini Wakristo wa karne ya kwanza kilikuwa muhimu.

Kwa nini basi, shauri kuhusu kukataa maswali juu ya fundisho? Ilikuwa kwa sababu katika siku ya Paulo watu fulani—waliofafanuliwa naye kuwa “waliofisidika katika akili na kuporwa ile kweli”—walikuwa wakizusha masuala ya kimafundisho nia yao hasa ikiwa kupindua imani ya wengine. (1 Timotheo 6:5, NW) Ilikuwa tu kuhusu maswali yaliyozushwa na watu hao waliofisidika kwamba Paulo alimshauri Timotheo aepuke mazungumzo kuhusu itikadi za kidini.

Je, Itikadi Huathiri Mwenendo?

Ingawa hivyo, huenda wengine wakatilia shaka ikiwa itikadi zetu za kidini huwa na athari nyingi juu ya namna ya watu ambao sisi hupata kuwa—sifa zetu za kibinafsi na mwenendo. Huenda wakaona itikadi na mwenendo kuwa vitu viwili vilivyotenganishwa na visivyohusiana, kama koti na suruali ndefu ambazo zaweza kuvaliwa pamoja au kupangwa kulingana na mapendezi ya mvaaji. Hata hivyo, katika Biblia, itikadi na mwenendo zafanana sana na suti ambayo hutokea tu ikiwa seti inayofanana.

Biblia hufunua uhusiano wa moja kwa moja kati ya kile tunachoamini na aina ya watu tunayopata kuwa. Wale Mafarisayo wa siku ya Yesu wenye kujiona kuwa wenye haki walikuwa kielelezo cha itikadi zenye kuongozwa vibaya zinazoathiri mwenendo. (Mathayo 23:1-33; Luka 18:9-14) Kwa upande ule mwingine Wakolosai 3:10 (NW) hutushauri hivi: “Mjivike wenyewe utu mpya, ambao kupitia ujuzi sahihi unafanywa upya kulingana na mfano wa Yule aliyeuumba.” Angalia kwamba nguvu ya kuwa na maisha ya kimungu yahusianishwa na kuwa na ujuzi sahihi kuhusu Mungu.

Neno la Kigiriki lililotafsiriwa “ujuzi sahihi,” ambalo latokea mara 20 katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo, hurejezea ujuzi barabara, sahihi, au kamili. Msomi Mgiriki Nathanael Culverwel analifafanua kuwa “kupata kujua vizuri zaidi kitu nilichokijua mbeleni; mwono barabara zaidi wa kitu ambacho nilikiona kutoka umbali fulani.” Hivyo kama vile tu mwuza vito huchunguza kito ili kukadiria ubora na thamani yacho, Mkristo lazima achunguze Neno la Mungu ili aje kupata maarifa barabara, sahihi na kamili juu ya Mungu anayemtumikia. Hili latia ndani kupata kujua utu wa Mungu, makusudi yake, viwango vyake, na mafundisho yote yanayofanyiza “kiolezo cha maneno yenye afya”—tofauti sana na kuamini tu kwamba ‘kuna Mtu Fulani kule juu.’—2 Timotheo 1:13, NW.

Kielelezo cha aina ya matunda yanayopatikana mtu ajuapo Mungu kutoka umbali fulani tu kimerekodiwa katika sura ya kwanza ya barua iliyopuliziwa kwa Warumi. Hapo, rejezo lafanywa kwa watu fulani ambao, “ijapokuwa walimjua Mungu, . . . hawakukubali kuwa na Mungu katika ujuzi sahihi.” Matokeo ya itikadi zao zenye makosa yanaelezewa na mtume Paulo hivi: “Mungu aliwaacha katika hali ya akilini iliyokataliwa, ili wafanye mambo yasiyofaa, wakiwa wamejawa na ukosefu wote wa uadilifu, uovu, choyo, ubaya, wakiwa wamejaa husuda, uuaji-kimakusudi, zogo, udanganyi, mwelekeo wenye nia ya kudhuru, wakiwa wanong’onezi, wasengenyaji, wachukiaji Mungu, wafidhuli, wenye kiburi, wenye kujitanguliza, wabuni wa mambo mabaya, wasiotii wazazi, wasio na uelewevu, wasio wa kweli katika mapatano, wasio na shauku ya asili, wasio na rehema.”—Warumi 1:21, 28-31, NW.

Bila shaka, itikadi zilizoshikiliwa na watu hao ziliathiri uwezo wao wa kuishi maisha ya Kikristo. Vivyo hivyo leo, itikadi na mwenendo waweza kulinganishwa na vazi lililofumwa kipande kimoja, lililofumwa pamoja isivyoweza kuachana. Kwa hivyo, ni jambo muhimu kwamba wote wanaotamani kupata upendeleo wa Mungu wahakikishe itikadi zao za kidini ni za kweli kabisa, zilizotegemezwa kabisa na Neno la Mungu. Kwa kuwa “Mapenzi ya [Mungu] ni kwamba watu wa namna zote waokolewe na kuja kwenye ujuzi sahihi wa kweli.”—1 Timotheo 2:4, NW.

[Picha katika ukurasa wa 25]

Kujiona kuwa mwenye haki kwa yule Farisayo kulionyesha itikadi zakey

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki