Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g95 12/8 kur. 11-13
  • Kile Tulichojifunza Kutokana na Andrew

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kile Tulichojifunza Kutokana na Andrew
  • Amkeni!—1995
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Shauri Lifaalo
  • Kujifunza Huruma Zaidi
  • Nguvu za Upendo
  • Masomo Ambayo Tumejifunza
  • Familia Zilizofanikiwa—Sehemu ya Kwanza
    Amkeni!—2009
  • Kutoka kwa Wasomaji Wetu
    Amkeni!—1996
  • Yesu Aanza Kufanya Wanafunzi
    Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
  • Mazungumzo ya Familia
    Amkeni!—2010
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1995
g95 12/8 kur. 11-13

Kile Tulichojifunza Kutokana na Andrew

NILIPOKUWA nikiendesha gari kwenda kazini, niliona likiwa jambo lenye kufurahisha kufikiri kuhusu kile kilichokuwa kimetukia katika siku chache zilizotangulia. Nilikuwa tu nimekuwa baba ya mwana, mtoto wangu wa pili. Leo mke wangu Betty Jane na Andrew wetu mdogo watakuja nyumbani kutoka hospitalini.

Hata hivyo, kabla ya kuruhusiwa kutoka, mke wangu alipiga simu. Kulikuwa na hali ya wasiwasi katika sauti yake. Nilifanya haraka kwenda hospitalini. “Kuna jambo baya!” ilikuwa salamu yake. Tuliketi pamoja, tukingoja daktari arudi akiwa na mtaalamu mwenye kushauri juu ya magonjwa ya watoto.

Maelezo ya kwanza ya huyo mtaalamu yalikuwa habari yenye kuhuzunisha mno. Yeye alitaarifu hivi: “Tuna uhakika kabisa kwamba mwana wenu ana tatizo la Down’s syndrome.” Yeye alieleza kwamba yaelekea mwana wetu atadumaa akili. Sikushika maelezo yake zaidi ya hapo. Ubongo wangu uliokufa ganzi kwa sababu ya mshtuko ulikuwa umekata mipwito yote ya kusikia. Lakini niliendelea kuona.

Yeye alimnyanyua Andrew na kuvuta uangalifu wetu kwa moja ya mambo ambayo yalimtahadharisha juu ya uhakika kwamba kulikuwa na jambo baya. Kichwa cha mtoto kilicheza-cheza kwa ulegevu. Ukosefu huu wa hali nzuri ya misuli ulikuwa jambo lenye kuainisha vitoto vilivyozaliwa karibuni vyenye Down’s syndrome. Kwa kipindi kilichofuata pamoja na huyo mtaalamu, tulimuuliza maswali mengi yaliyojaa akili zetu huku uwezo wetu wa kufahamu ukirudi polepole. Angekuwa punguani kwa kadiri gani? Tungeweza kutazamia nini? Tungeweza kumfunza kwa kadiri gani? Angeweza kujifunza kwa kadiri gani? Yeye alieleza kwamba majibu ya maswali yetu mengi yangetegemea mazingira ambayo angeishi na vilevile uwezo wake wa kiasili.

Kwa miaka zaidi ya 20 tangu wakati huo, tumejaribu kumpa Andrew upendo na shauku anayostahili na kumfunza yote tuwezayo kumtolea. Lakini tukitazama nyuma, sasa twatambua kwamba hayajakuwa tu mazoezi katika kutoa bali katika kupokea pia.

Shauri Lifaalo

Kabla ya kupata wakati wa kujirekebisha kwa ajili ya kuwako kwa Andrew, marafiki wenye upendo walitupatia shauri walilokuwa wamepata kutokana na kuvumilia majaribu yao wenyewe. Walitutakia mema, lakini kama ilivyoweza kutazamiwa, si shauri lote lililokuja kuwa lenye hekima au lenye mafaa. Hata hivyo, baada ya miaka mingi ya kujaribu, shauri lao lilitokea kuwa madokezo mawili yenye thamani na hekima.

Wengine walijaribu kutuliwaza kwa kusema kwamba Andrew hakuwa amedumaa kabisa. Lakini rafiki wa zamani alionya kwa upole hivi: “Msikatae kukubali ukweli wa mambo! Mara mkubalipo mapungukio yake, ndivyo itakavyokuwa rahisi kurekebisha matarajio yenu na kuanza kumsaidia jinsi alivyo.”

Hilo lilikuja kuwa moja ya masomo ya maana zaidi tuliyojifunza katika kukabili hali mbaya. Hakuwezi kuwa na kupona kihisia hadi kuwe na kukubali uhalisi wa mambo. Ingawa kukataa mara nyingi ni kwa kawaida, kadiri kukataa kunavyoendelea, ndivyo tuzidivyo kuahirisha kuchukua hatua za lazima, na kutenda kulingana na mapungukio yanayosababishwa na, ‘matukio yasiyotazamiwa ambayo hupata watu wote.’—Mhubiri 9:11, NW.

Kwa miaka yote ambayo tumekutana na wazazi wenye watoto ambao hawakuweza kukabili masomo ya kawaida ya shule au waliokuwa katika shule za kurekebishia, mara nyingi tumejiuliza ni watoto wangapi ambao huenda walikuwa wamedumaa au kulemazwa kwa namna nyingine. Je, baadhi yao wangekuwa miongoni mwa “wenye upungufu usioonekana wazi”—wale ambao, tofauti na Andrew, hawakuwa na tofauti iliyo wazi ya kimwili na huonekana kama watoto wa kawaida? Watu wenye Down’s syndrome hutambuliwa kwa urahisi. Lakini aina nyinginezo za ulemavu hazina ishara zilizo dhahiri. Ni wazazi wangapi wanaoshikilia kwa nguvu matarajio yasiyo halisi na kukataa kukubali mapungukio ya mtoto, ikitokeza udhiko kwa kila mtu?—Linganisha Wakolosai 3:21.

Shauri la pili ambalo uzoefu wetu ulihakikisha ni hili: Hatimaye ni NYINYI mtakaoathiri jinsi watu wengi watakavyomtendea mtoto wenu. Vile mtakavyomtendea, yaelekea ndivyo wengine watakavyomtendea pia.

Kumekuwa na mabadiliko mengi katika miongo michache iliyopita katika mitazamo ya watu kuelekea watu wenye upungufu wa kimwili na kiakili. Lakini mengi ya mabadiliko haya yamechochewa na baadhi ya watu wenye upungufu wenyewe, watu wao wa ukoo, na waungaji mkono wengine wa kawaida na watetezi wa kitaaluma. Wazazi wengi wamepuuza kwa ujasiri shauri la kupeleka watoto wao katika makao ya kipekee na kama tokeo wamerekebisha maoni yaliyoko juu ya jinsi ya kutendea watoto wenye upungufu. Miaka hamsini iliyopita vitabu vingi vya kufunzia vya kitiba kuhusu Down’s syndrome vilitegemea habari iliyokusanywa kutoka makao ya kutunzia walemavu kiakili. Leo matarajio yamerekebishwa kabisa, mara nyingi kwa sababu wazazi na watu wengine wamefuata njia mpya za kushughulika na watoto hao.

Kujifunza Huruma Zaidi

Inashangaza jinsi ilivyo rahisi kujidanganya kufikiria kwamba sisi ni wenye huruma kikweli. Lakini hadi tunapohusika kibinafsi, ufahamu wetu wa matatizo mengi mara nyingi huenda ukawa wa kijuu-juu tu.

Hali ya Andrew imetulazimisha kutambua kwamba watu waliopungukiwa mara nyingi hawawezi kudhibiti hali yao. Kwa hakika, imetufanya tukabili swali, Mtazamo wangu kwa kweli ni nini kuelekea walio dhaifu, wasioshika mambo kwa wepesi, na wazee-wazee?

Mara nyingi tumekuwa hadharani na Andrew na kumekuwa na watu wageni, ambao wakitazama ukubali wetu usio na aibu kuelekea Andrew akiwa mshiriki kamili wa familia yetu, wametujia na kushiriki nasi matatizo yao ya siri. Ilikuwa kana kwamba kuwapo kwa Andrew kuliwahakikishia kwamba tungeweza kuwa na hisia-mwenzi kwa matatizo yao.

Nguvu za Upendo

Kwa kiwango kikubwa somo la maana zaidi ambalo Andrew ametufunza ni kwamba upendo si kazi ya akili tu. Ebu nieleze. Moja ya mambo ya msingi ya ibada yetu tukiwa Mashahidi wa Yehova ni kwamba Ukristo wa kweli hupita migawanyiko na ubaguzi wa jamii, kijamii na kisiasa. Tukiwa na uhakika na kanuni hii, tulijua kwamba Andrew angekubaliwa na ndugu na dada zetu wa kiroho. Tukipuuza shauri la wataalamu waliosema kwamba halikuwa jambo halisi kumtarajia akae kwa staha katika vipindi vyote vya ibada, tangu alipozaliwa tumehakikisha kwamba amekuwa akiandamana nasi kwenye mikutano na pia nyumba kwa nyumba katika kazi yetu ya kuhubiri. Kama inavyotarajiwa, kutaniko humtendea kwa fadhili na huruma.

Lakini kuna wale wanaopita hili. Wana upendo wa kipekee kumwelekea. Yaonekana Andrew huona hili kwa uwezo wa kipekee ambao hauzuiwi na akili yake iliyopungua. Akiwa na watu hawa yeye hushinda haya yake ya asili kwa urahisi, naye huwaendea moja kwa moja baada ya mikutano. Mara nyingi, tumetazama uwezo wake wa kisilika wa kuweza, hata katika umati, kutambua wale wanaompenda kipekee.

Na ndivyo ilivyo na udhihirisho wake wa upendo. Andrew ni mwanana sana kuelekea vitoto, watu wenye umri mkubwa, na wanyama-rafiki. Nyakati fulani anapokikaribia kitoto cha mtu fulani tusiyemjua bila kusita, tunakaa karibu, tukiwa tayari kukiokoa kitoto hicho ikiwa Andrew bila kutahadhari atashughulika nacho kikatili. Hata hivyo ni mara nyingi kama nini tumeaibika juu ya hofu zetu tulipomtazama akikishika kitoto kwa wororo kama mama mwenye kitoto kichanga afanyavyo!

Masomo Ambayo Tumejifunza

Kwa kuwa watoto wote wenye Down’s syndrome wana sura inayofanana, tulitazamia kwamba wote wangekuwa na utu unaofanana. Hata hivyo, baada ya muda mfupi tulipata kujua kwamba wanafanana na washiriki wa familia yao kuliko wenzao. Kila mmoja ana utu wa kipekee.

Andrew, sawa na vijana wengine wengi, hafurahii kazi ngumu. Lakini tulipata kwamba kama tungekuwa na subira na uvumilivu kumfanya apitie kazi fulani tena na tena hadi iwe zoea, hakuiona kama kazi tena. Kazi zake ndogo-ndogo nyumbani sasa zimekuwa kama jambo la kawaida, na ni kazi ndogo-ndogo za ziada tu zinazoonekana kuwa kazi.

Tunapotazama nyuma kwa masomo ambayo tumejifunza wakati wa maisha ya Andrew, jambo fulani lisiloonekana kuwa kweli na lenye kupendeza lazuka. Karibu mambo makuu yote tuliyojifunza katika kumlea Andrew yalikuja kutumika sawasawa kwa mahusiano yetu na watoto wengine pamoja na watu kwa ujumla.

Kwa kielelezo, ni nani kati yetu asiyeitikia ifaavyo kwa upendo wa kweli? Ikiwa kuna wakati wowote ulipolinganishwa kwa njia isiyofaa na mtu fulani ambaye uwezo au uzoefu wake ulitofautiana sana na wako, je, hukuona hilo likiwa jambo lisilo haki na lenye kutamausha? Mwishowe, je, haijakuwa kweli kwa wengi wetu kwamba kazi ambazo mwanzoni hazikuwa zenye kufurahisha zilikuja hatimaye kuwa zenye kuvumilika, hata zenye kutosheleza, tulipokuwa na uwezo wa kujidhibiti na kushikamana nazo?

Ingawa tumetiririsha machozi mengi kuhusiana na Andrew kwa sababu ya kutoelewa kwetu kwa kibinadamu, tumeshiriki pia shangwe nyingi, kubwa na ndogo. Na tumepata kwamba katika maeneo yasiyohusiana kabisa na Andrew, tumekua kwa sababu yake. Tulijifunza kwamba ono lolote katika maisha, haidhuru ni lenye kujaribu kadiri gani, lina uwezo wa kutufinyanga kuwa watu bora zaidi badala ya kuwa watu wenye uchungu.

Kuna jambo jingine lenye umaana mkubwa kwetu. Tunapata furaha nyingi sana kutokana na kutarajia wakati mtukufu ambapo tutashuhudia kurekebishwa kwa upunguani wa Andrew. Biblia yaahidi kwamba karibuni katika ulimwengu mpya mwadilifu wa Mungu, watu wote walio vipofu, viziwi, walemavu, na mabubu watarudishiwa afya bora. (Isaya 35:5, 6; Mathayo 15:30, 31) Wazia shangwe ambayo wote watakuwa nayo katika kujionea wenyewe kuponywa kwa akili na mwili huku wanadamu wote wakifikia uwezo wao kamili! (Zaburi 37:11, 29)—Imechangwa.

[Sanduku katika ukurasa wa 12]

Viwango vya Upungufu

Wataalamu fulani hugawanya watu wenye Down’s syndrome katika vikundi vitatu. (1) Wawezao Kuelimishwa (Wasio wabaya sana): wale ambao wanaweza kupata stadi za kielimu za kadiri fulani. Kikundi hiki hutia ndani wengine ambao wamekuwa waigizaji au hata wahadhiri. Wengine wamefaulu kuishi kwa kujitegemea wakiwa na usimamizi mchache. (2) Wawezao Kuzoezwa (Wenye Upungufu Kadiri): wale wawezao kujifunza stadi fulani zenye mafaa. Ingawa wanaweza kufunzwa kujitunza kufikia kiwango fulani, usimamizi zaidi wahitajiwa. (3) Wagumu (Wenye Hali Mbaya): kikundi kisichoweza kabisa kufanya mambo ya kawaida, ambao huhitaji usimamizi mwingi.

Namna gani Andrew? Sasa tunajua kwamba yeye anaangukia katika kikundi kinachotajwa kuwa “Wawezao Kuzoezwa.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki