Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g96 2/22 uku. 15
  • “Ikiwa Ningeweza Kubadili Hali Fulani ya Wakati”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Ikiwa Ningeweza Kubadili Hali Fulani ya Wakati”
  • Amkeni!—1996
  • Habari Zinazolingana
  • Yesu Huokoa—Jinsi Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Kwa Nini Watu Hufa?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Kwa Nini Wanadamu Wanateseka na Kupatwa na Mambo Mabaya?
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Kwa Nini Vita na Ukatili Vinaendelea?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2025
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1996
g96 2/22 uku. 15

“Ikiwa Ningeweza Kubadili Hali Fulani ya Wakati”

WANAFUNZI katika shule iliyoko California, Marekani, waliombwa waandike insha juu ya kichwa kilichopo juu. Mmoja wa washiriki katika fainali ya shindano hilo alikuwa Eric, mwana mwenye umri wa miaka 11 katika familia ya Mashahidi wa Yehova. Aliandika insha ifuatayo yenye msingi katika Biblia.

“Vita ya Ulimwengu 2 ilikuwa vita yenye kufisha. Watu wengi wasio na hatia walikufa. Lakini hali ambayo nimechagua kubadili ingefanya vita hii isiwepo kamwe katika vitabu vya historia. Fikiria juu ya mauaji ya John F. Kennedy. Mwanamume huyu alikufa kifo kibaya, lakini hali ambayo nimechagua kubadili ingefanya jambo hilo nalo lisiwepo katika vitabu vya historia. Martin Luther King, Jr. alikufa 1968 akijaribu kubadili kufikiri kwa ulimwengu, lakini hali ambayo nimechagua kubadili ingetangulia kipindi hiki nacho. Ikiwa ningeweza kubadili hali hiyo ya wakati, ulimwengu ungekuwa tofauti, kila kitu kama tukijuavyo kingebadilika, na mambo yote, kutia ndani nyakati na watu, yangekuwa tofauti. Hali hii ilipotokea historia ilibadilika na kuufanya ulimwengu uwe kama tuujuavyo leo—wenye kufisha, mjeuri, mgonjwa, na mwovu.

“Huenda ukawa unajiuliza, ‘Je, hali hii ni ugonjwa? Je, ni serikali? Au hali hii ni vita?’ Jiulize mwenyewe, ‘Ikiwa ingekuwa ni ugonjwa, ingewezaje kuyazuia matendo ya wanadamu yasiwe maovu?’ ‘Haingeweza,’ ungesema. Kisha unafikiri, ‘Lazima iwe ni serikali ambayo itasuluhisha matatizo yetu yote.’ Lakini serikali inaongozwa na wanadamu, na wanadamu wote ni wasiokamilika na wenye kufa. Basi je, kazi zao nzuri hazingekufa pamoja nao? Kisha unasema, ‘Lazima iwe ni vita kama ile Vita ya Ulimwengu 2.’ La! Haingeweza kuwa hivyo kwa sababu katika vita upande mmoja hushinda, na hivyo ule upande mwingine hushindwa. Hakuna lolote la mambo hayo yote yaliyotajwa lingeweza kumaliza kabisa kifo, jeuri, ugonjwa, na uovu. Huenda ukawa unajiuliza ni ipi iliyo hali ambayo ningebadili.

“Dhambi. Kifo. Dhambi na kifo ndiyo mambo ambayo ningebadili. Lakini jinsi gani? Sikuzote tumekuwa na dhambi na kifo. Dhambi na kifo ni sehemu ya maisha zetu za kila siku. Basi wawezaje kubadili jambo ambalo limekuwapo sikuzote? Ingekulazimu kulizuia wakati ule lilipoanza. Ule uasi wa Adamu na Hawa dhidi ya serikali ya Mungu ulifanya mambo yawe yalivyo leo. Waliohusika walichagua kufanya mambo kwa njia yao, na hivyo tuna dhambi na kifo.

“Hivyo hali hususa ambayo ingebadilishwa ni wakati ule uwongo wa kwanza ulisemwa na Shetani Ibilisi dhidi ya ile serikali kamilifu. Kwa sababu ya uwongo huo, sisi sote tunateseka kwa sababu ya yale ambayo wazazi wetu wa kwanza, Adamu na Hawa, walifanya. Walitenda dhambi dhidi ya Kiongozi wa pekee wa kweli wa serikali, Mungu.”

Jumamosi, Agosti 12, 1995, Eric alisoma insha yake kwenye siku ya kusanyiko la pekee la Mashahidi wa Yehova huko Norco, California. Wahudhuriaji walifurahi kusikia juu ya kijana aliyetumia kwa manufaa fursa aliyopata shuleni kutoa ushahidi wenye kuchochea fikira kuhusu kisababishi cha kuteseka kwa binadamu. Utakuwa utukufu kama nini wakati Yehova Mungu atakapomharibu “nyoka wa zamani” na kuondoa kuteseka kwote ambako kunasababishwa na Ibilisi!—Ufunuo 12:9; 21:3, 4; Mwanzo 3:1-6.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki