Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • wp25 Na. 1 uku. 9
  • Kwa Nini Vita na Ukatili Vinaendelea?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kwa Nini Vita na Ukatili Vinaendelea?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2025
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • DHAMBI
  • SERIKALI ZA WANADAMU
  • SHETANI NA ROHO WAKE WAOVU
  • Jinsi Vita na Ukatili Vitakavyoisha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2025
  • Kusudi la Mungu kwa Wanadamu Ni Nini?
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Dhambi ya Kwanza Ilikuwa Nini?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Jinsi Vita na Ukatili Vinavyotuathiri Sisi Sote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2025
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2025
wp25 Na. 1 uku. 9

Kwa Nini Vita na Ukatili Vinaendelea?

Biblia inafunua mambo yanayosababisha vita na ukatili na sababu zinazofanya matukio hayo yenye kuhuzunisha yaendelee kutukia.

DHAMBI

Mungu aliwaumba wazazi wetu wa kwanza, Adamu na Hawa, kwa mfano wake. (Mwanzo 1:27) Hilo linamaanisha kwamba wangeonyesha sifa za Mungu kama vile amani na upendo. (1 Wakorintho 14:33; 1 Yohana 4:8) Hata hivyo, Adamu na Hawa walikosa kumtii Mungu na kutenda dhambi. Na matokeo ni kwamba sisi sote tumerithi dhambi na kifo. (Waroma 5:12) Dhambi tuliyorithi hutuchochea kuwa na mawazo na matendo ya kikatili.—Mwanzo 6:5; Marko 7:​21, 22.

SERIKALI ZA WANADAMU

Mungu hakutuumba ili tujitawale sisi wenyewe. Biblia inasema hivi: “Mwanadamu anayetembea hana uwezo wa kuongoza hatua yake.” (Yeremia 10:23) Kwa sababu hiyo, serikali za wanadamu haziwezi kuondoa kabisa vita na ukatili.

SHETANI NA ROHO WAKE WAOVU

Biblia inafunua kwamba “ulimwengu mzima unakaa katika nguvu za yule mwovu.” (1 Yohana 5:19) “Yule mwovu” anaitwa Shetani Ibilisi, naye ni muuaji mwenye ukatili. (Yohana 8:44) Yeye pamoja na roho wake waovu, ndio wanaowachochea watu wapigane na wawe wakatili.—Ufunuo 12:​9, 12.

Hatuwezi kuondoa mambo yanayosababisha vita na ukatili, lakini Mungu anaweza.

Dini na Vita

Mara nyingi, dini huchochea kuunga mkono na kuendeleza vita. Dini hizo ni miongoni mwa dini za uwongo ambazo kwa pamoja hujulikana kuwa “Babiloni Mkubwa.” (Ufunuo 18:2) Mungu anasema kwamba Babiloni Mkubwa atawajibika kwa sababu ya vifo vya “wale wote ambao wameuawa duniani.” (Ufunuo 18:24) Ili kujifunza mengi zaidi soma makala yenye kichwa “Babiloni Mkubwa Ni Nani?” kwenye jw.org.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki