Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • wp25 Na. 1 kur. 10-13
  • Jinsi Vita na Ukatili Vitakavyoisha

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jinsi Vita na Ukatili Vitakavyoisha
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2025
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • MUNGU ATAONDOA SERIKALI ZA WANADAMU
  • MUNGU ATAONDOA DHAMBI
  • MUNGU ATAMWONDOA SHETANI NA ROHO WAKE WAOVU
  • Maoni ya Mungu Kuhusu Vita Leo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Kwa Nini Vita na Ukatili Vinaendelea?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2025
  • Majibu ya Maswali ya Biblia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Biblia Inasema Nini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2017
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2025
wp25 Na. 1 kur. 10-13
Mwanajeshi anatafakari akiwa ameketi juu ya kifusi cha jiji lililoharibiwa na vita.

Wanadamu hawawezi kukomesha vita

Jinsi Vita na Ukatili Vitakavyoisha

Biblia inasema kwamba Mungu ndiye “[atakayekomesha] vita katika dunia yote” na si wanadamu.”—Zaburi 46:9.

MUNGU ATAONDOA SERIKALI ZA WANADAMU

Mungu ataondoa serikali za wanadamu kupitia kile ambacho Biblia inakiita vita vya Har–​Magedoni.a (Ufunuo 16:16) Wakati huo, “wafalme wa dunia nzima inayokaliwa” watakusanywa pamoja kwa ajili ya “vita vya siku kuu ya Mungu Mweza-Yote.” (Ufunuo 16:14) Har–​Magedoni ni vita ya Mungu itakayokomesha vita vyote.

Mungu ataziondoa serikali za wanadamu na kusimamisha Ufalme au serikali yake, ambayo itatawala kutoka mbinguni na serikali hiyo haitaharibiwa kamwe. (Danieli 2:44) Mungu amemchagua Mwana wake, Yesu Kristo, awe Mfalme. (Isaya 9:​6, 7; Mathayo 28:18) Serikali hiyo ni Ufalmeb ambao Yesu aliwafundisha wanafunzi wake wasali kuuhusu. (Mathayo 6:​9, 10) Wanadamu wote wataunganishwa chini ya serikali ya ulimwenguni pote, Yesu akiwa Mtawala.

Tofauti na watawala wa kibinadamu, Yesu hatatumia mamlaka yake ili kujifaidi. Kwa kuwa yeye hutenda haki na hana ubaguzi, hakuna atakayehitaji kuogopa kwamba atatendewa isivyo haki au kupuuzwa kwa sababu ya rangi, taifa, au utamaduni wake. (Isaya 11:​3, 4) Na watu hawatahitaji tena kupigania haki zao. Kwa nini? Kwa sababu Yesu atashughulikia mahitaji ya kila mtu. “Atamwokoa maskini anayelilia msaada, pia mtu wa hali ya chini na yeyote ambaye hana msaidizi. . . . Atawaokoa kutoka katika ukandamizaji na ukatili.”—Zaburi 72:​12-14.

Ufalme wa Mungu utaondoa duniani silaha zote zinazoua. (Mika 4:3) Pia, utawaondoa wanadamu waovu ambao wanakataa kuacha vita na kuvuruga amani ya wengine. (Zaburi 37:​9, 10) Kila mwanamume, mwanamke, na mtoto watahisi wakiwa salama mahali popote watakapokuwa duniani.—Ezekieli 34:28.

Ufalme wa Mungu utakapotawala watu watafurahia maisha bora. Utaondoa matatizo yote yanayosababisha watu wapigane kama vile umaskini, njaa, na ukosefu wa makao. Kila mtu atakuwa na chakula kingi chenye lishe na atafurahia kuwa na mahali bora pa kuishi.—Zaburi 72:16; Isaya 65:​21-23.

Chini ya Ufalme wa Mungu, madhara yote yanayosababishwa na vita yataondolewa. Hilo linatia ndani maumivu yote ya kimwili, kiakili, na kihisia yanayowapata watu kwa sababu ya mambo mabaya yanayotokea wakati wa vita. Hata wale waliokufa watafufuliwa ili waishi tena duniani. (Isaya 25:8; 26:19; 35:​5, 6) Familia zitaungana tena na kumbukumbu zenye kuumiza za vita zitakuwa sehemu ya “mambo ya zamani [yaliyopitilia] mbali.”—Ufunuo 21:4.

MUNGU ATAONDOA DHAMBI

Ufalme wa Mungu utakapotawala dunia, watu wote watamwabudu Mungu wa pekee wa kweli, Yehovac, “Mungu wa upendo na amani.” (2 Wakorintho 13:11) Watu watajifunza jinsi ya kuishi pamoja kwa amani. (Isaya 2:​3, 4; 11:9) Wale wote wanaotumia mambo wanayojifunza watawekwa huru, kutokana na matokeo ya dhambi.—Waroma 8:​20, 21.

MUNGU ATAMWONDOA SHETANI NA ROHO WAKE WAOVU

Ufalme wa Mungu utawaharibu waanzilishi wa vita, Shetani na roho wake waovu. (Ufunuo 20:​1-3, 10) Bila ya uvutano wao mwovu, “amani itakuwa nyingi.”—Zaburi 72:7.

Unaweza kuwa na uhakika kwamba ahadi ya Mungu ya kukomesha vita itatimia. Ana uwezo na anatamani sana kuondoa vita.

  • Mungu ana hekima na nguvu zinazohitajika ili kukomesha vita na ukatili. (Ayubu 9:4) Hakuna jambo lolote ambalo hawezi kutimiza.—Ayubu 42:2.

  • Mungu huchukia kuona watu wakiteseka. (Isaya 63:9) Pia, “humchukia mtu yeyote anayependa ukatili.”—Zaburi 11:5.

  • Sikuzote Mungu hutimiza ahadi zake; na hawezi kamwe kusema uwongo.—Isaya 55:​10, 11; Tito 1:2.

Mungu ataleta amani ya kweli na ya kudumu wakati ujao

Familia ikicheka pamoja huku wakiwa wameketi juu ya mlima katika dunia paradiso. Farasi wanakula majani katika eneo lililo karibu.

Mungu atakomesha vita

Kwa nini Mungu ameruhusu vita?

Huenda ukajiuliza, kwa nini Mungu ameruhusu vita viendelee hadi sasa? Ili kujibu swali hilo tazama video yenye kichwa Kwa Nini Mungu Anaruhusu Kuteseka? kwenye jw.org.

a Soma makala yenye kichwa “Vita vya Har–​Magedoni Ni Nini?” kwenye jw.org.

b Tazama video yenye kichwa Ufalme wa Mungu Ni Nini? kwenye jw.org.

c Yehova ni jina la kibinafsi la Mungu.—Zaburi 83:18.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki