Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • wp25 Na. 1 kur. 4-5
  • Jinsi Vita na Ukatili Vinavyotuathiri Sisi Sote

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jinsi Vita na Ukatili Vinavyotuathiri Sisi Sote
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2025
  • Habari Zinazolingana
  • Vita Vitakwisha Lini?​—Biblia Inasema Nini?
    Habari Zaidi
  • Matrilioni Yatumiwa Katika Vita—Gharama Halisi Ni Ipi?
    Habari Zaidi
  • Jinsi Vita na Ukatili Vitakavyoisha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2025
  • Vita
    Amkeni!—2017
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2025
wp25 Na. 1 kur. 4-5
Mkusanyo wa picha: 1. Mwanajeshi akitembea huku kifaru cha jeshi kikimfuata nyuma yake. 2. Wanaume, wanawake na watoto kutoka mataifa mbalimbali ambao wameathiriwa na vita.

Jinsi Vita na Ukatili Vinavyotuathiri Sisi Sote

“Tangu Vita vya Pili vya Dunia, idadi ya jeuri imeongezeka zaidi ulimwenguni, hivi kwamba mtu mmoja kati ya watu wanne wanaoishi duniani leo anaishi katika maeneo yaliyoathiriwa na vita.”

Naibu katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Amina J. Mohammed, Januari 26, 2023.

Vita na jeuri vinaweza kuanza ghafla katika maeneo ambayo sasa yana amani. Hata wale ambao wanaishi katika maeneo ambayo hayajapatwa na vita huathiriwa pia. Na madhara yanayotokana na vita yanaweza kudumu kwa muda mrefu hata baada ya vita hivyo kwisha. Fikiria mifano ifuatayo:

  • Picha inayoonyesha mikono miwili iliyoshika bakuli tupu.

    Upungufu wa chakula. Kulingana na Shirika la Chakula Duniani, “vita ndio chanzo kikuu cha njaa. Watu wengi ambao hawana chakula cha kutosha wanaishi katika maeneo yaliyo na vita.”

  • Picha inayomwonyesha mwanamke mwenye huzuni akiwa amefunika uso wake kwa mikono.

    Matatizo ya afya ya kimwili na ya kiakili. Uwezekano wa vita kutokea unaweza kuwasababishia watu mkazo na mahangaiko mengi sana. Wale wanaoishi katika maeneo yaliyoathiriwa na vita hawakabili tu hatari za kimwili bali pia, wanakabili hatari ya kupatwa na matatizo ya afya ya akili. Na inasikitisha kwamba mara nyingi wanashindwa kupata huduma za kitiba wanazohitaji.

  • Picha inaonyesha familia ikiwa imebeba mabegi makubwa yaliyojaa vitu vyao.

    Vita vinasababisha watu wakimbie makao yao. Kulingana na Shirika la Wakimbizi Ulimwenguni, kufikia Septemba 2023, zaidi ya watu milioni 114 ulimwenguni pote wamelazimika kuyakimbia makao yao. Sababu kuu ya janga hilo ni vita na ukatili.

  • Picha inaonyesha familia ikiwa imesimama nje ya nyumba yao ya kawaida.

    Hali ngumu ya kiuchumi. Kwa kawaida, watu hukabili hali ngumu ya kiuchumi, kama vile kupanda kwa bei za bidhaa kwa sababu ya vita. Huenda watu wakateseka kwa sababu serikali inatumia pesa nyingi kwa ajili ya kugharimia vita, hata pesa ambazo kwa kawaida zingetumiwa kugharimia huduma za kiafya na elimu. Na baada ya vita kwisha, gharama kubwa hutumiwa kujenga upya majengo yaliyoharibiwa wakati wa vita.

  • Picha inaonyesha mafuta yakimwagika kutoka kwenye bomba.

    Uharibifu wa mazingira. Watu huteseka wakati eneo wanaloishi linapoharibiwa kimakusudi. Uchafuzi wa maji, hewa, na udongo unaweza kusababisha matatizo ya kiafya ya muda mrefu, na mabomu yaliyofichwa na kusahauliwa ardhini yanaweza kusababisha madhara kwa muda mrefu hata baada ya vita kwisha.

Bila shaka, vita husababisha uharibifu na gharama kubwa sana.

Vita na Unabii wa Biblia

Unabii wa Biblia unaonyesha kwamba vita na ukatili vingekuwa sehemu ya ile ishara ya “umalizio wa mfumo wa mambo.” (Mathayo 24:3) Yesu Kristo alitabiri hivi:

  • “Mtasikia kuhusu vita na habari za vita. . . . Kwa maana taifa litapigana na taifa na ufalme kupigana na ufalme.”—Mathayo 24:​6, 7.

  • “Mtakaposikia kuhusu vita na machafuko msiogope.”—Luka 21:9.

    Katika lugha ya awali, neno linalotafsiriwa “machafuko” linaweza kumaanisha vurugu, mizozo, upinzani dhidi ya mamlaka zilizowekwa, uasi, vurugu za kisiasa, na maandamano.

Ili ujifunze mengi zaidi, soma makala yenye kichwa “Ni Nini Ishara ya “Siku za Mwisho?” kwenye jw.org.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki