Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mrt makala 112
  • Vita Vitakwisha Lini?​—Biblia Inasema Nini?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Vita Vitakwisha Lini?​—Biblia Inasema Nini?
  • Habari Zaidi
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Ulimwengu uliojaa vita
  • Vita vya kukomesha vita vyote
  • 2023: Mwaka Uliojaa Msukosuko—Biblia Inasema Nini?
    Habari Zaidi
  • Vita Nchini Ukrainia Vyaingia Mwaka wa Pili—Biblia Inatoa Tumaini Gani?
    Habari Zaidi
  • Matrilioni Yatumiwa Katika Vita—Gharama Halisi Ni Ipi?
    Habari Zaidi
  • Jinsi Vita na Ukatili Vinavyotuathiri Sisi Sote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2025
Pata Habari Zaidi
Habari Zaidi
mrt makala 112
Picha: Picha ya maeneo yaliyoathiriwa na vita katika Mashariki ya Kati. 1. Milipuko katika mji kwenye Ukanda wa Gaza. 2. Picha ya Jerusalem baada ya shambulizi la kombora.

Kushoto: Yasser Qudaih/Anadolu via Getty Images; kulia: RONALDO SCHEMIDT/AFP via Getty Images

ENDELEA KUKESHA!

Vita Vitakwisha Lini?​—Biblia Inasema Nini?

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres alisema hivi kuhusu shambulizi la moja kwa moja la Iran dhidi ya Israel Jumamosi, Aprili 13, 2024: “Huu ndio wakati wa kujaribu kupunguza uhasama unaongezeka. Sasa ndio wakati wa kujidhibiti kikamili.”

Vita vinavyoendelea katika Mashariki ya Kati ni mfano mmoja tu wa kinachoendelea ulimwenguni pote.

“Sasa hivi kuna mapambano mengi zaidi yanayoendelea ulimwenguni pote kuliko wakati mwingine wowote tangu Vita vya Pili vya Ulimwengu na vinawaathiri watu bilioni 2, yaani, robo ya wanadamu wote.”​—Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, Januari 26, 2023.

Maeneo ambayo yanahusika katika vita yanatia ndani Israel, Gaza, Siria, Azerbaijan, Ukrainia, Sudan, Ethiopia, Niger, Myanmar, na Haiti.a

Vita vitakwisha lini? Je, viongozi wa ulimwengu wanaweza kutokeza amani? Biblia inasema nini?

Ulimwengu uliojaa vita

Mapambano yenye jeuri yanayoendelea leo ulimwenguni pote yanaonyesha kwamba hivi karibuni vita vyote vitakwisha. Vita vinavyoendelea vinatimiza unabii wa Biblia kuhusu kipindi cha wakati tunamoishi. Biblia inaita kipindi hicho “umalizio wa mfumo wa mambo.”​—Mathayo 24:3.

  •  “Mtasikia kuhusu vita na habari za vita. . . . Taifa litapigana na taifa na ufalme kupigana na ufalme.”​—Mathayo 24:6, 7.

Soma makala yenye kichwa “Ni Nini Ishara ya ‘Siku za Mwisho’?” ili uone jinsi vita vinavyoendelea vinavyotimiza unabii wa Biblia?

Vita vya kukomesha vita vyote

Biblia inatabiri mwisho wa mapambano ya wanadamu. Hilo litatukiaje? Si kwa jitihada za wanadamu, bali kupitia Har-Magedoni, “vita vya siku kuu ya Mungu Mweza-Yote.” (Ufunuo 16:14, 16) Baada ya vita hivyo, Mungu atatimiza ahadi yake kwa wanadamu ya kuwaletea amani ya kudumu.​—Zaburi 37:10, 11, 29.

Ili ujifunze mengi zaidi kuhusu vita vya Mungu vya kukomesha vita vyote, soma makala yenye kichwa “Vita vya Har-Magedoni Ni Nini?”

a Orodha ya ACLED ya Mapambano, “Inaorodhesha mapambano yenye jeuri zaidi ulimwenguni pote,” Januari 2024

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki