Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mrt makala 113
  • Heshima Ilienda Wapi?​—Biblia Inasema Nini?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Heshima Ilienda Wapi?​—Biblia Inasema Nini?
  • Habari Zaidi
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Heshima ilienda wapi?
  • Mwongozo wenye kutegemeka kuhusu tabia yenye heshima
  • Mwongozo Ulio Mkamilifu wa Kiadili
    Amkeni!—1993
  • Mema na Mabaya: Mwongozo Unaofuatwa na Wengi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2024
  • Jinsi Unavyoweza Kubadili Namna Ulivyo
    Amkeni!—1992
  • Je, Maadili Yanazorota?
    Amkeni!—2003
Pata Habari Zaidi
Habari Zaidi
mrt makala 113
Mwanamke kijana akimsaidia kwa fadhili mwanamke mwenye umri kubwa kupata kiti kwenye basi.

ENDELEA KUKESHA!

Heshima Ilienda Wapi?​—⁠Biblia Inasema Nini?

Idadi ya watu wanaotenda kwa heshima inazidi kupungua. Wagonjwa wasio na heshima wanawagombeza madaktari; wateja katika mikahawa huwatendea wahudumu kwa njia isiyo na heshima; abiria huwatendea vibaya wahudumu wa ndege; watoto wakaidi huwadhihaki, kuwatisha, na kuwashambulia walimu; na baadhi ya wanasiasa huhusika katika kashfa huku wanasiasa wenzao wakijaribu kujionyesha kuwa watu wenye kuheshimika sana.

Hata hivyo, Biblia inatoa mwongozo unaofaa wa kuonyesha mwenendo wenye heshima ni upi. Pia, inaeleza kwa nini leo watu hawatendi kwa heshima.

Heshima ilienda wapi?

Ulimwenguni pote watu wanazidi kutenda kwa ukosefu wa heshima, yaani, hawajiendeshi kwa tabia nzuri, yenye maadili, na inayokubalika.

  •  Kulingana na utafiti uliofanywa hivi karibuni na shirika la Gallup, Wamarekani waliohojiwa walisema kwamba katika miaka 22 iliyopita viwango vya maadili nchini Marekani vimeshuka zaidi sasa kuliko wakati mwingine wowote ndani ya kipindi hicho.

  •  Utafiti mwingine uliohusisha watu 32,000 katika nchi 28, asilimia 65 kati ya waliohojiwa walisema kwamba ukosefu wa heshima leo haujawahi kuonekana wakati mwingine katika historia.

Biblia ilitabiri tabia tunayoona leo.

  •  “Katika siku za mwisho nyakati ngumu zitakuja. Watu watajipenda wenyewe na kupenda fedha. Watakuwa na majivuno na wenye jeuri. Watawatukana wengine kwa matusi. Hawatawatii wazazi wao. Watakuwa wasio na shukrani. . . . Hawatakuwa na upendo kwa wengine na . . . watakuwa wakatili.”​—2 Timotheo 3:1-3, Tafsiri ya Kusoma kwa Urahisi.

Ili upate habari zaidi kuhusiana na jinsi unabii huu unavyotimizwa, soma makala yenye kichwa, “Je, Biblia Ilitabiri Mitazamo na Matendo ya Watu Leo?”

Mwongozo wenye kutegemeka kuhusu tabia yenye heshima

Katika ulimwengu ambapo heshima inazidi kuzorota, mamilioni ya watu wameona kwamba Biblia ni mwongozo unaofaa wa kumsaidia mtu kutenda kwa heshima. Mashauri yake “yanategemeka sikuzote, sasa na milele.” (Zaburi 111:8) Fikiria mifano kadhaa:

  •  Biblia inasema hivi: “Mambo yote mnayotaka watu wawatendee ninyi, lazima ninyi pia mwatendee vivyo hivyo.”​—Mathayo 7:12.

    Maana: Tunapaswa kuwatendea wengine kwa fadhili na heshima, kama tu tunavyotaka kutendewa.

  •  Biblia inasema hivi: “Kwa sababu mmeacha udanganyifu, semeni ukweli kila mmoja na mwenzake.”​—Waefeso 4:25.

    Maana: Tunapaswa kuwa wanyoofu katika yote tunayosema na kufanya.

Ili upate habari nyingi zaidi kuhusu habari hii, tafadhali soma:

  •  Mnara wa Mlinzi toleo lenye kichwa “Mema na Mabaya—Mwongozo Unaoweza Kutegemea.”

  •  Makala yenye kichwa “Jinsi Biblia Inavyoweza Kukusaidia Kuwa Mstahimilivu.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki