Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g92 5/8 kur. 7-10
  • Jinsi Unavyoweza Kubadili Namna Ulivyo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jinsi Unavyoweza Kubadili Namna Ulivyo
  • Amkeni!—1992
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Hatua 1: Tafuta Kujua Jinsi Ulivyo Kikweli
  • Hatua 2: Amua Jinsi Unavyotaka Kuwa
  • Hatua 3: Tafuta Vielelezo Vinavyostahili
  • Hatua 4: Pata Nguvu Unayohitaji Ili Kufanikiwa
  • Hatua 5: Kabiliana Na Udhaifu wa Kurudia
  • Kuvumbua Jinsi Ulivyo Hasa
    Amkeni!—1992
  • Kwa Nini Ubadili Jinsi Ulivyo?
    Amkeni!—1992
  • “Neno la Mungu Li Hai, Tena Lina Nguvu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Dhibiti Maisha Yako Sasa!
    Amkeni!—1996
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1992
g92 5/8 kur. 7-10

Jinsi Unavyoweza Kubadili Namna Ulivyo

NI NINI kimekosekana kwenye njia zilizozungumziwa tayari za kusitawisha tabia na za kufanya badiliko? Nia ya mtu mwenyewe na utumizi wa uwezo wa kusudio! Ni matakwa ya mtu mwenyewe kwa uchaguzi wa kibinafsi. Kwa ufupi, kujidhibiti kwake kunakosekana!

Matabibu wa tabia wameona kwamba wana nafasi nzuri zaidi ya kupata matokeo ya kudumu ikiwa mtu anayetibiwa ana uhuru wa kutoa maoni juu ya kujiwekea miradi yake mwenyewe. Vance Packard anaandika hivi katika kitabu chake The People Shapers: “Ni wazi kwa shauri dogo, kila mtu mwenye akili ya kufikiri anaweza kuwa mrekebishi wa tabia yake mwenyewe.” Hili laitwa kujiweza-mwenyewe. Yaani ni kusema, palipo na kujidhibiti binafsi, maendeleo yenye kutokeza yameonekana.

Wakristo wana manufaa ya ziada wakati kujidhibiti kunapotumiwa, kwa kuwa wamejifunza kuzoea hili kama moja la matunda tisa ya roho takatifu ya Mungu. (Wagalatia 5:22, 23) Hili lamaanisha kwamba kani ya utendaji ya Mungu Mweza Yote yaweza kutumika katika badiliko la tabia yako na kukusaidia ufaulu.

Kwa hivyo, unataka kufanya nini kuhusu tabia yako? Je! kweli unataka kweli kubadilika! Ikiwa ndivyo, kutoka kwenye nini? Uwe nini? Na kwa nini? Je! unaweza kuamini udhibiti wako mwenyewe? Ni wapi unapoweza kupata msaada unaotoa manufaa tu?

Acha tuangalie baadhi ya njia na mambo yanayohusika katika kubadili tabia.

Hatua 1: Tafuta Kujua Jinsi Ulivyo Kikweli

Wewe ndiwe chanzo cha vile unavyotaka kuwa. Ni lazima uundwe upya kwa kubadilisha ulivyokuwa. Kwa hivyo ni lazima ujijue kwa usahihi. Je! unaweza kuonyesha ni sehemu zipi za tabia yako ungependa kubadilisha?

Kwa vile ni vigumu kujua tabia yako, unahitaji kutafuta kiwango kinachostahiwa na chenye kustahili. Biblia Takatifu inafaa kwa jambo hili. Tumia Biblia, na utapata kuona jinsi ulivyo kabla ya jinsi ungeweza kujiona hapo mwanzoni. Huenda hata usipendezwe na sura yako inayoonyeshwa hapo, lakini waweza kuwa na hakika kwamba ni mfano sahihi.

Biblia imefananishwa na kioo, na watu wanasihiwa waichungulie ndani. “mtu akiwa ni msikiaji wa neno tu, wala si mtendaji, mtu huyo ni kama mtu anayejiangalia uso wake katika kioo. Maana hujiangalia, kisha huenda zake, mara akasahau jinsi alivyo. Lakini aliyeitazama sheria kamilifu iliyo ya uhuru, na kukaa humo, asiwe msikiaji msahaulifu, bali mtendaji wa kazi, huyo atakuwa heri katika kutenda kwake.” (Yakobo 1:23-25) Biblia, ikieleweka na kutumiwa vizuri, ina uwezo wa kuchanganua ambao hautakuonyesha tu jinsi ulivyo kama mtu bali pia itafunua makusudio yako na mitazamo yako. Hivyo, Paulo aliandika: “Maana Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili . . . tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo.” Neno la Mungu hata hutoa uongozi zaidi juu ya ni nini lifaalo kikweli na nini lililo kosa kikweli.—Waebrania 4:12; 5:14.

Biblia yaweza kukufanyia mambo yote hayo kwa sababu ni Neno la Yehova, Mungu wa kweli mwenye ufahamu. Kulingana na Zaburi 139, Mungu anakuchunguza na kufanya uchanganuzi sahihi wa jinsi ulivyo. Kama vile mstari wa 1 usemavyo: “Ee BWANA [Yehova, NW] umenichunguza na kunijua.” Mungu amekuwa akikuangalia tangu kutungwa kwako. Anakujua kabisa kabisa. Ameandikisha maelezo juu ya maisha ya kibinadamu kwenye Biblia katika hali zote ziwezekanazo. Utaona sura yako mwenyewe katika kurasa zake, iwe ni kwa njia inayofaa au isiyofaa.

Hivyo, unaweza kujua jinsi ulivyo—ikiwa unataka.

Hatua 2: Amua Jinsi Unavyotaka Kuwa

Ili ubadilike, hakikisha badiliko litastahili. Hakikisha kwamba ni lile unalotaka na ni bora kuliko vile ulivyo sasa. Ni miradi ipi ya tabia unayopasa kuweka? Unaweza kupata wapi shauri linalofaa la tabia zenye kupendeza? Tena, Biblia inafaa kwa jambo hili.

Biblia hukusihi ubadilike kuwa mzuri zaidi, kuwa na “utu mpya.” Paulo alishauri: “Mvue kwa habari ya mwenendo wa kwanza utu wa zamani, unaoharibika kwa kuzifuata tamaa zenye kudanganya; na mfanywe wapya katika roho ya nia zenu; mkavae utu mpya, ulioumbwa kwa namna ya Mungu katika haki na utakatifu wa kweli.” (Waefeso 4:22-24) Biblia yakuonyesha zile zilizo tabia nzuri zaidi. Je! unakumbuka ulimwengu mkamilifu uliozungumziwa mapema? Ikiwa unataka kuwa sehemu ya ulimwengu huo, ni lazima uone uhitaji wa kutokeza sifa zinazoelezwa katika Wakolosai 3:12-17, sifa kama vile huruma, fadhili, unyenyekevu, upole, saburi, msamaha, upendo, amani, na shukrani.

Kwa hiyo baada ya kutafuta ushauri katika Biblia yako, weka miradi yako. Ichunguze. Patia kila mradi nafasi yake. Ifanyie kazi!

Hatua 3: Tafuta Vielelezo Vinavyostahili

Sehemu kubwa ya tabia yako ilisitawishwa kwa kuiga wengine—marafiki, mashirika, wazazi, walimu wa shule.

Kwa nini, basi, baada ya kuamua miradi ya tabia zinazokupendeza, usitafute mtu ambaye ana tabia unayotamani kuiga? Halafu tafuta msaada wa mtu huyo. Mithali ya Biblia yasema hivi kwa hekima: “Enenda pamoja na wenye hekima, nawe utakuwa na hekima.”—Mithali 13:20.

Biblia ina usimulizi wa maisha ya aliye kielelezo bora zaidi kwetu sote, Yesu Kristo mwenyewe. Soma jinsi alivyojiendesha chini ya hali zote, mwenendo wake wa kiadili, ufahamu wake na hekima, adhama yake, ufikirio wake na fadhili isiyo ya kawaida na hangaikio lake kwa binadamu mwenzake. Anasikika kuwa mwenye kuburudisha kama nini asemapo: “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha. Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu; kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi”!—Mathayo 11:28-30.

Mamilioni katika nchi zote tayari wamemgeukia Yesu kama kielelezo chao na wanajitahidi kufuata hatua zake, kama vile yeye mwenyewe, alivyotembea katika njia aliyoagizwa na Baba yake wa kimbingu, Yehova Mungu. Mamilioni hawa, wakiwa wametosheka na tabia mbaya ya ulimwengu kwa ujumla leo, wamegeukia kundi la kwao la Mashahidi wa Yehova ili wapate msaada na uongozi na hawajatamaushwa. Katika Majumba ya Ufalme yao, mifano bora ya Kikristo imejaa, na msaada zaidi umetolewa kwa wale wanaotaka kubadilisha tabia yao ya kibinafsi iwe nzuri zaidi. Bila shaka, Mashahidi wana udhaifu mbalimbali ulio kawaida ya ainabinadamu isiyo kamilifu; lakini wana nguvu ya kiroho inayofaa ambayo inatendesha akili zao.—Waefeso 4:23.

Hatua 4: Pata Nguvu Unayohitaji Ili Kufanikiwa

Litakuwa jambo lenye kufariji kwa wale wanaotamani kubadili njia zao kujua kwamba msaada unapatikana. “Utu mpya” unaelezwa kuwa ‘unaumbwa kwa namna ya Mungu katika haki na utakatifu wa kweli.’ (Waefeso 4:24) Hili lathibitisha kwamba usaidizi uzidio ule wa kibinadamu upo kwa Mungu mwenyewe ili upatikane na wale wanaoutamani. Unawezaje kupata msaada wa Yehova Mungu?

Moja ya misaada mikubwa ni sala ya kibinafsi. Sala huandaa huduma muhimu ya kupata ushauri kwa chanzo cha uwezo unaohitajiwa kubadili njia zako. Sala hukurusu uongee kwa uhuru na waziwazi wakati wowote, hata katikati ya shida. Njia hiyo ya kumfikia Mungu aliye halisi na mwenye kujali inashindia mbali njia yoyote ya msaada wa kibinadamu na ina matokeo mara iyo hiyo. Hivyo basi, mtume Yohana angeweza kuandika hivi: “Na huu ndio ujasiri tulio nao kwake, ya kuwa, tukiomba kitu sawasawa na mapenzi yake, atusikia.” (1 Yohana 5:14) Na maneno ya nabii Isaya yatutia moyo: “Mtafuteni BWANA [Yehova, NW] maadamu anapatikana, Mwiteni, maadamu yu karibu; Mtu mbaya na aache njia yake, na mtu asiye haki aache mawazo yake; Na amrudie BWANA [Yehova, NW] naye atamrehemu; na arejee kwa Mungu wetu, naye atamsamehe kabisa.”—Isaya 55:6, 7.

Funzo la Biblia pia hutia nguvu, likikutolea burudisho, likikuwezewesha kila siku uikazie fikira miradi yako. Biblia hutoa msaada unaofaa kadiri uendeleavyo kujitahidi kuelekea kufikia shabaha ya tabia yako. Zaidi ya hilo, huchochea hisi ya machukio kwa njia zako za awali. Kutwaa maarifa ya Biblia kila siku na yaliyomo kutasaidia pia kuzisonga habari zozote mbaya ambazo zaweza kupenya kutoka vyombo vya habari vya ulimwengu na mifumo yao ya uelimishaji.

Mikutano ya Kikristo kwenye Jumba la Ufalme la kwenu la Mashahidi wa Yehova huandaa si elimu ya viwango vya Biblia tu bali pia tegemezo la kikundi cha watu kwa ujumla na himizo la kuwa na tabia iliyofanyiwa maendeleo. Tegemezo hili linalopatikana katika kundi limesaidia wengi kufanikiwa katika tabia. Kwa nini usizungumzie msaada huo pamoja na mtu uliyepokea kutoka kwake gazeti hili?

Hatua 5: Kabiliana Na Udhaifu wa Kurudia

Wengi wamejaribu kutengeneza njia zao lakini wamevunjwa moyo na udhaifu wa kurudia usioepukika. Matokeo ni kwamba wengine hujiachilia kabisa. Watu kama hao hufikiri kwamba ikiwa walilotumainia kuwa tumaini lao limekosa kufaulu sasa, hakuna tumaini hata kidogo. Huenda wakajitoa wafuate shawishi za ulimwengu. Kwa kawaida wanakuwa wabaya zaidi ya walivyokuwa hapo kwanza kabla ya kujaribu kubadilika.

Endelea kujihakikishia mwenyewe kwamba mwendo wowote wa zamani usioupenda unahitaji jitihada kuepukwa. Mtume Paulo aliieleza tabia yake ya zamani na njia yake ya maisha kuwa kama rundo la mavi, au takataka. (Wafilipi 3:8) Kwa hiyo, ikiwa wewe unapofanya badiliko, unakwazwa na kizuizi au udhaifu wa kurudia, simama tena, na endelea kwenda mbele. Endelea! Zidi kupigana! Itastahili!

Kumbuka, nyingi za njia na tabia zako ziliingizwa kwako na misukumo ya nje bila chaguo lako au udhibiti wako wakati ule. Misukumo hii bado yafanya kazi. Je! utaacha ikufinyange katika umbo layo? Hapana? Basi usikate tamaa!

Mamilioni ya watu kutoka tamaduni mbalimbali—hata wahalifu na watu waliojiingiza katika tabia isiyo ya adili—wamefanikiwa kubadili tabia yao. Wamesitawisha viwango vizuri mpaka sasa, wengi kwa miongo ya miaka, wakibaki katika njia zao nzuri zaidi kwa ushika-ukamilifu wa hiari unaotamanika. Lakini wanamshukuru Mungu kwa nguvu na kichocheo cha kufanya hivyo. Kama vile mtume Paulo alivyosema: “Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.”—Wafilipi 4:13.

Wao wanashinda katika vita ya kufanya yaliyo mema. Wewe pia waweza kufanya badiliko hilo ikiwa kweli unataka, na unaweza kufurahia maisha katika ulimwengu mpya wa Mungu.—Zaburi 37:29; 2 Petro 3:13.

[Picha katika ukurasa wa 7]

Hatua 1: Tafuta Kujua Jinsi Ulivyo

[Picha katika ukurasa wa 8]

Hatua 2: Amua Jinsi Unavyotaka Kuwa

[Picha katika ukurasa wa 8]

Hatua 3: Tafuta Vielelezo Vinavyostahili

[Picha katika ukurasa wa 9]

Hatua 4: Pata Nguvu Unayohitaji Ili Kufanikiwa

[Picha katika ukurasa wa 9]

Hatua 5: Kabiliana na Udhaifu wa Kurudia

[Picha katika ukurasa wa 10]

Wale wanaobadilika wanaweza pia kurithi dunia iliyobadilishwa

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki