Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g96 4/22 kur. 23-24
  • Je, Wewe Huthamini Uhuru wa Kidini?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Wewe Huthamini Uhuru wa Kidini?
  • Amkeni!—1996
  • Habari Zinazolingana
  • Nusu Karne Chini ya Utawala wa Kiimla
    Amkeni!—1999
  • Wajumbe wa Amani Katika Ulaya Mashariki
    Amkeni!—1997
  • Nilijifunza Kumtegemea Mungu
    Amkeni!—2006
  • Jinsi Dini Ilivyoshambuliwa na Sovieti
    Amkeni!—2001
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1996
g96 4/22 kur. 23-24

Je, Wewe Huthamini Uhuru wa Kidini?

Na mleta-habari wa Amkeni! katika Estonia

PÄRNU ni jiji la bandari litembelewalo nyakati za likizo lililoko Estonia, nchi ndogo ya Baltiki, iliyokuwa jamhuri ya Muungano wa Sovieti. Hilo jiji lina idadi ya watu zaidi ya 50,000. Hao watu sasa wanafurahia uhuru wa kuabudu katika dini wanayochagua—uhuru ambao hawakuwa nao miaka michache iliyopita. Katika Juni 17, 1995, Pärnu Leht, gazeti la huko, lilitaja kwamba Pärnu lilikuwa na dini 11 na kwamba hilo gazeti lilipanga kuchapisha mfululizo wa makala kuzihusu.

Makala ya kwanza ilieleza: “Twaanza na kutaniko ambalo kazi yao yaonekana kuwa imetuathiri sote—Mashahidi wa Yehova—ambao kwa sasa wanafanya mikutano yao kwenye jumba la kiwanda cha pombe. . . . Katika 1931 Wanafunzi wa Biblia walianza kujiita Mashahidi wa Yehova, na hilo ndilo jina walilo nalo kufikia leo hii. Kuna Mashahidi wa Yehova zaidi ya milioni tano ulimwenguni pote. Makao makuu ya Mashahidi wa Yehova katika Estonia yako Tallinn.”

Hiyo makala iliendelea kusema: “Kutaniko la wapiga-mbiu wa Yehova lilianzishwa katika Pärnu mwaka mmoja na nusu uliopita. Mwanzoni kulikuwa na washiriki 25; sasa limeongezeka kufikia 120 . . .

“Kuwaona kwa mara ya kwanza kwavutia. Watu—sanasana wenzi wa ndoa walio wachanga—ni wenye urafiki, wamevalia vizuri, na wasiopendelea. Inashangaza kwamba watoto walikuwa wenye nidhamu sana, kwa kuwa si rahisi kwa mtoto mchanga kukaa mahali pamoja kwa saa moja na nusu—lakini wao walifanya hivyo.”

Likieleza jinsi Mashahidi wa Yehova hutofautiana na dini nyinginezo, hilo gazeti lilisema: “Wao hutilia mkazo Paradiso itakayokuja. Pia yaweza kuonekana wazi jinsi kutaniko lijuavyo sana Biblia, nao huinukuu kila iwezekanapo.” Katika kumalizia hiyo makala ilisema: “Watu hao 120, walio wapiga-mbiu wa Yehova, wameamua; nao wana uhakika kuwa wamefanya uamuzi ufaao. Imani yao na upigaji-mbiu wayo ndilo jambo kuu katika maisha yao.”

Si kila mtu katika Pärnu waliofurahishwa na makala hii ya kwanza katika mfululizo ulionuiwa kuchapishwa juu ya dini za hilo jiji. Katika Julai 8, 1995, Pärnu Leht liliripoti: “Tungependa kuchapisha ombi tulilopata kutoka kwa makanisa manne kuhusiana na kuanzishwa kwa safu mpya.” Ombi hilo au barua hiyo iliyoandikiwa hilo gazeti ilikuwa imetiwa sahihi na wawakilishi wa Kanisa Othodoksi katika Estonia, Evangelical Lutheran Church la Estonia, Muungano wa Estonia wa Wakristo wa Kievanjeli na Wabaptisti, na Kanisa la Kimethodisti la Estonia.

Wawakilishi hawa wanne wa kidini walilalamika: “Laonekana kuwa ajabu sana kwamba mlianza ule mfululizo kwa makala juu ya Mashahidi wa Yehova.” Zaidi ya hayo, walisema: “Kuhusiana na mfululizo huo, tungependa kusema kwamba twaona haitawezekana kuhojiwa na Pärnu Leht.”

Hao wawakilishi wa kidini walimalizia kwa kusema: “Katika jumuiya ambamo wengi wametatanishwa kwa sababu ya mkazo wenye kuendelea kutokana na dini mpya na mafarakano mapya mbalimbali zinazoendeleza ‘hali ya kiroho,’ twaona uhitaji wa vichapo kufikiria hali ya kidini ya hapa na kuweza kutofautisha makanisa ya kihistoria kutoka kwa mafarakano na harakati zenye kupita kiasi. Washiriki wa Baraza la Makanisa la Estonia, linalowakilisha makanisa ya Kikristo yanayofurahia umoja wa kidini, wapaswa kutoa nuru nyangavu vya kutosha kuongoza katika suala hilo.”

Hata hivyo, kufuatia barua hii, mwandikaji wa Pärnu Leht alitoa maoni haya yenye busara: “Yote tuonayo kuwa sawa huenda yasiwe sawa. Na mtazamo na maoni ya Mungu juu ya makundi tofauti-tofauti huenda yasiwe sawa na mitazamo ya dini hizi nne zenye kuheshimiwa, au vinginevyo. Hakuna yeyote kati yetu asiyeweza kukosea, hata makanisa yenye mapokeo ya karne nyingi.”

Wewe wahisije juu ya mwelekeo uliobadilika kuelekea dini katika zile zilizokuwa jamhuri za Muungano wa Sovieti? Tuna uhakika kwamba watu watafutao kweli kila mahali huthamini uhuru wa kidini unaofurahiwa huko.

[Ramani katika ukurasa wa 23]

(Ona mpangilio kamili katika nakala iliyochapishwa)

FINLAND

Helsinki

Bahari ya Baltiki

ESTONIA

Tallinn

Pärnu

LATVIA

Riga

LITHUANIA

Vilnius

URUSI

St. Petersburg

Moscow

BELARUS

Minsk

[Picha katika ukurasa wa 24]

Kutaniko la Mashahidi wa Yehova Katika Pärnu

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki