Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g98 4/8 kur. 12-14
  • Wanawake Wana Wakati Ujao Gani?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wanawake Wana Wakati Ujao Gani?
  • Amkeni!—1998
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kuwaelimisha Waume na Akina Baba
  • Hangaiko la Mungu kwa Ajili ya Wanawake
  • Wanawake Wanaostahiwa
  • Suluhisho la Kudumu
  • Heshima na Staha Chini ya Utunzaji wa Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • ‘Wanawake Wenye Bidii Katika Bwana’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Wanawake Wakristo Wastahili Heshima na Staha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Je, Kweli Mungu Anawajali Wanawake?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1998
g98 4/8 kur. 12-14

Wanawake Wana Wakati Ujao Gani?

“HISTORIA ya mwanadamu ni historia ya kurudia-rudia kwa wanaume kuwajeruhi na kutumia vibaya mamlaka juu ya wanawake.” Ndivyo lilivyosomeka Julisho Wazi la Mawazo la Seneca Falls, New York, lililoandikwa huko Marekani karibu miaka 150 iliyopita ili kuteta dhidi ya ukosefu wa haki kuelekea wanawake.

Bila shaka maendeleo yamefanywa tangu wakati huo, lakini kama vile kichapo cha Umoja wa Mataifa The World’s Women 1995 kinavyosema, bado kuna mengi ya kufanya. “Mara nyingi, wanaume na wanawake huishi katika ulimwengu tofauti,” charipoti, “ulimwengu unaotofautiana katika nafasi za elimu na kazi, na katika afya, usalama wa kibinafsi na wakati wa wasaa wa mapumziko.”

Ongezeko la ufahamu wa hili limeongoza mataifa mengi kupitisha sheria za kulinda haki za wanawake. Lakini sheria haziwezi kubadili mioyo, ambako mizizi ya ukosefu wa haki na upendeleo huwa. Kwa kielelezo, fikiria hali mbaya ya wasichana makahaba. Gazeti Newsweek lilisema kuhusu fedheha ya kimataifa: “Utungaji-sheria unaolenga katika kuzuia kutumia watoto kwa kujifaidi kingono huwa wenye makusudi mema lakini mara nyingi huwa hauna matokeo.” Vivyo hivyo, kuwepo kwa sheria hakuzuii jeuri. “Uthibitisho wafunua jeuri kuelekea wanawake kuwa tatizo lililoenea tufeni pote,” lataarifu Human Development Report 1995. “Sheria nyingi hazitoshi ili kusimamisha jeuri kama hiyo—isipokuwa kanuni za sasa za kitamaduni na kijamii zibadilike.”—Italiki ni zetu.

“Kwa kawaida msingi wa kanuni za kitamaduni na kijamii” huwa mapokeo yaliyotia mizizi—jambo lililo gumu sana kubadili. “Mapokeo huwafanya wanaume kuamini kwamba wanawake wanapasa kutumiwa badala ya kupendwa, kufanyizwa kazi badala ya kutunzwa,” asema mwanamke mmoja kutoka Mashariki ya Kati. “Likiwa tokeo, mwanamke hawezi kusema, hana haki zozote, na ana nafasi ndogo sana ya kuboresha hali yake.”

Kuwaelimisha Waume na Akina Baba

Programu ya Utendaji iliyopendekezwa katika Beijing, China, na mkutano wa 1995 wa wanawake wa ulimwenguni pote ilijulisha wazi kwamba “tendo la mara moja na la umoja la watu wote” ndilo tu liwezalo kutimiza “ulimwengu wenye amani na wenye ubinadamu” ambao katika huo wanawake watastahiwa.

Tendo lolote la kufanya maisha ya wanawake yawe yenye ‘amani zaidi, yenye haki, na yenye ubinadamu’ lazima lianzie nyumbani, na waume na akina baba. Katika hili, Mashahidi wa Yehova wamesadikishwa kwamba elimu ya Biblia ndiyo ufunguo wa mafanikio. Wameona kwamba mara tu wanaume wajifunzapo kuwa Mungu atazamia wawatendee wake zao na binti zao kwa staha na ufikirio wao hutilia jambo hilo maanani na kufanya hivyo.

Katika Afrika ya Kati, Pedro, mwanamume aliyeoa na aliye baba ya watoto wanne, sasa ni msikivu kwa mahitaji ya mke wake. Yeye humsaidia mke wake kuwatunza watoto, na hata hupakua chakula wageni wajapo kula pamoja na familia yao. Mtazamo wenye ufikirio kama huo si wa kawaida katika nchi yao. Ni nini kinachomfanya amthamini mke wake na kushirikiana naye?

“Nilipoanza kujifunza Biblia, nilijifunza kanuni mbili za maana kuhusu daraka la mume,” aeleza Pedro. “Zimekuwa na athari kubwa kwangu katika njia ninayomwona mke wangu. Ya kwanza, katika 1 Petro 3:7, yaeleza kwamba mume apaswa kumpa mke heshima “kama chombo dhaifu zaidi, kile cha kike.” Ya pili, katika Waefeso 5:28, 29, yasema kwamba mume apaswa kumtendea mke wake ‘kama mwili wake mwenyewe.’ Tangu nitumie shauri hilo, tumekuwa na ukaribu zaidi. Kwa hiyo sisi wanaume twapaswa kuthamini zaidi shauri la Mungu kuliko desturi za kienyeji.”

Michael, kutoka Afrika Magharibi, akiri kwamba kabla hajaanza kujifunza Biblia na Mashahidi, hakumtendea mke wake vizuri. “Hata nilikuwa nikimpiga nilipokasirika,” yeye aungama. “Lakini Biblia ilinifunza kwamba lazima nibadili njia zangu. Sasa najaribu sana kudhibiti hasira yangu na kumpenda mke wangu kama mwili wangu mwenyewe. Nasi sote tuna furaha zaidi.” (Wakolosai 3:9, 10, 19) Mke wake Comfort, akubali hivi: “Sasa Michael hunitendea kwa staha na shauku zaidi kuliko ilivyo desturi ya wengi wa wanaume wa jumuiya yetu. Twaweza kuyazungumzia matatizo yetu na kufanya kazi pamoja kwa kushirikiana.”

Pedro na Michael walijifunza kuwastahi na kuwapenda wake zao kwa sababu walitilia maanani maagizo kutoka katika Neno la Mungu, ambayo huonyesha wazi kwamba ukosefu wa haki kuelekea wanawake haumpendezi Muumba wetu hata kidogo.

Hangaiko la Mungu kwa Ajili ya Wanawake

Kila wakati Mungu amekuwa akiwahangaikia wanawake na hali njema yao. Ingawa aliwaambia wazazi wetu wa kwanza kwamba kwa sababu ya uasi wao, kutokamilika kungewaongoza wanawake kuwa ‘wakitawalwa,’ hili halikuwa kamwe kusudi la Mungu. (Mwanzo 3:16) Alikuwa amemuumba Hawa akiwa “msaidizi” wa Adamu na akiwa mwandamani wake. (Mwanzo 2:18) Katika Sheria ya Kimusa, iliyopewa Israeli la kale, Yehova alilaumu kihususa kuwatenda vibaya wajane na akawaagiza Waisraeli kuwatendea kwa fadhili na kuwasaidia.—Kutoka 22:22; Kumbukumbu la Torati 14:28, 29; 24:17-22.

Yesu, katika kumwiga Baba yake wa kimbingu, hakufuata mapokeo yaliyoenea ya siku yake yaliyowashusha wanawake. Alisema kwa fadhili kuwaelekea wanawake—hata wale waliokuwa na sifa mbaya. (Luka 7:44-50) Zaidi ya hilo, Yesu alipendezwa kuwasaidia wanawake waliokuwa na matatizo ya afya. (Luka 8:43-48) Katika pindi moja, alipomwona mjane akilia kwa sababu ya kifo cha karibuni cha mwanawe pekee, mara moja alienda kwenye msafara wa maziko na kumfufua mwanamume huyo kijana.—Luka 7:11-15.

Wanawake walikuwa miongoni mwa wanafunzi wa Yesu wa kwanza na walikuwa wa kwanza kushuhudia ufufuo wake. Biblia husema kwa kuwathamini wanawake kama vile Lidia, Dorkasi, na Priska wakiwa vielelezo vya ukaribishaji-wageni, huruma, na moyo mkuu. (Matendo 9:36-41; 16:14, 15; Waroma 16:3, 4) Na Wakristo wa mapema walizoezwa kuwastahi wanawake. Mtume Paulo alimwambia mishonari mwenzake Timotheo awatendee “wanawake wazee zaidi kama mama, wanawake vijana zaidi kama dada kwa usafi wote wa kiadili.”—1 Timotheo 5:2.

Wanawake Wanaostahiwa

Ikiwa wewe ni mwanamume Mkristo, utaonyesha staha ileile kuwaelekea wanawake. Hutatumia mapokeo kama kisababu cha kuwatenda vibaya. Zaidi ya hilo, kuwatendea wanawake kwa staha, kwatoa ushuhuda ulio wazi wa imani yako. (Mathayo 5:16) Salima, mwanamke mchanga kutoka Afrika, aeleza jinsi alivyofaidika kwa kushika kanuni za Kikristo.

“Nililelewa katika mazingira ambapo wanawake na wasichana walitendwa vibaya. Mama yangu alifanya kazi kwa muda wa saa 16 kila siku, na yote aliyopata ni malalamishi ikiwa kazi fulani iliachwa bila kufanywa. Vibaya hata zaidi, ni kwamba baba yangu angempiga alipokuwa amekunywa pombe kupita kiasi. Wanawake wengine katika eneo letu waliteseka vivyo hivyo. Lakini nilijua kwamba kuwatenda hivyo kulikuwa kosa—kwamba kulikuwa kukiyajaza maisha yetu na hali ya kutamauka na kukosa furaha. Hata hivyo, kulionekana kana kwamba hakukuwa na njia ya kubadili hali hii ya mambo.

“Hata hivyo, nilipokuwa tineja, nilianza kujifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova. Nilipendezwa sana niliposoma maneno ya mtume Petro, aliyesema kwamba wanawake wapaswa kutendewa kwa heshima. Lakini nikafikiri, ‘Ni vigumu kwa watu kutumia kanuni hii, hasa kwa sababu ya mapokeo yetu ya kienyeji.’

“Hata hivyo, nilipoenda kwenye Jumba la Ufalme, ambapo Mashahidi walifanyia mikutano yao, wanaume na vilevile wanawake walinitendea kwa fadhili. Lenye kushangaza hata zaidi, ni kwamba waume miongoni mwao waliwatunza sana wake zao. Kadiri nilivyoendelea kuwajua watu huko vema zaidi, nilijifunza kuwa hili lilikuwa jambo ambalo Mashahidi wote walitarajiwa kufanya. Hata ingawa baadhi ya wanaume walikuwa wametoka katika mazingira sawa na yangu, sasa walikuwa wakiwatendea wanawake kwa staha. Nilitaka kuwa mshiriki wa familia hii kubwa.”

Suluhisho la Kudumu

Staha ambayo Salima aliona haikuwa ya kujitokeza tu. Ilikuwa tokeo la programu yenye kufundisha, yenye msingi katika Neno la Mungu ambayo huwasaidia watu kuthaminiana kama afanyavyo Mungu. Huu ni wonyesho wa lile liwezalo kufanywa hata sasa na litakalofanywa wakati Ufalme wa Mungu utawalapo dunia yote. (Danieli 2:44; Mathayo 6:10) Serikali hii ya kimbingu itaondosha ukosefu wote wa haki. Biblia yatuhakikishia hivi: “Maana hukumu zako [Yehova] zikiwapo duniani, watu wakaao duniani hujifunza haki.”—Isaya 26:9.

Hata sasa, elimu katika uadilifu inabadili njia ambayo mamilioni ya watu wanafikiri. Wakati wanadamu wote wawapo katika ujitiisho kwa Ufalme wa Mungu, elimu hii itaendelea ulimwenguni kote na itamaliza hali ya kutenda wanawake kwa kuwaonea ambalo ni tokeo la dhambi ya Adamu. Yesu Kristo, Mfalme mwekwa rasmi wa Mungu, hataruhusu ukosefu wa haki kuelekea wanawake uharibu utawala wake. Ikieleza juu ya utawala huo wa Kristo, Biblia husema: “Atamkomboa mhitaji aliapo, na mtu aliyeonewa iwapo hana msaidizi. Atamhurumia aliye dhaifu na maskini, na nafsi za wahitaji ataziokoa. Atawakomboa nafsi zao na kuonewa na udhalimu.”—Zaburi 72:12-14.

Mfululizo huu wa makala umekazia matatizo ya wanawake. Hata hivyo, inatambuliwa kwamba wanaume wengi pia wametendwa vibaya. Kote katika historia wanaume wenye nguvu na waovu wametenda machukizo mabaya kuwaelekea wanaume na vilevile wanawake. Na wanawake fulani wamefanya vivyo hivyo. Kwa mfano, Biblia hutaja kuhusu kumwagwa kwa damu isiyo na hatia na wanawake waovu kama vile Yezebeli, Athalia, na Herodia.—1 Wafalme 18:4, 13; 2 Mambo ya Nyakati 22:10-12; Mathayo 14:1-11.

Hivyo, wanadamu wote wanahitaji ulimwengu mpya wa Mungu, chini ya utawala wa Ufalme wake. Karibuni, siku hiyo ifikapo, wala wanawake wala wanaume hawatabaguliwa tena wala kutendwa vibaya. Badala ya hivyo, kila siku kila mmoja ‘atajifurahisha.’—Zaburi 37:11.

[Picha katika ukurasa wa 13]

Waume Wakristo hufuata miongozo ya Biblia na kuwastahi na kuwaheshimu wake zao

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki