Njoo, Usikilize Ujumbe Wenye Tumaini la Kweli
UTAUSIKIA ujumbe huo katika hotuba ya watu wote yenye kichwa “Kufanya Vitu Vyote Kuwa Vipya—Kama Ilivyotabiriwa,” itakayotolewa kwenye “Neno la Mungu la Kiunabii” Mkusanyiko wa Wilaya wa Mashahidi wa Yehova mwaka huu. Watu wengi wanatumaini kwamba mwaka wa 2000 utaletea wanadamu baraka.
“Milenia yamaanisha kwamba tunaweza kuepuka daraka la karne iliyo mbaya sana,” akasema profesa mmoja wa chuo kikuu. Na ijapokuwa “mwaka wa 2000 huenda ukawa mwaka mwingine tu kwenye kalenda,” gazeti Maclean’s lilisema hivi, “huenda ikatukia kwamba utasadifu mwanzo mpya kabisa.” Hata hivyo, mambo yaliyoonwa yanadokeza kwamba huenda hilo lisitukie.
Jitihada za binadamu za kuleta “mwanzo mpya” hazijafua dafu. Basi, kwa nini tunaweza kuamini ahadi ya Mungu iliyosemwa zaidi ya miaka 1900 iliyopita, “Tazama! Mimi ninafanya vitu vyote kuwa vipya”? (Ufunuo 21:5) Sababu zenye kusadikisha zitatolewa katika hotuba hii ya watu wote yenye kuchangamsha moyo. Unaweza kuisikiliza mahali palipo karibu nawe, kwa kuwa mwanzoni mwa mwezi huu, itatolewa kwenye maelfu ya mikusanyiko ulimwenguni pote.
Wasiliana na Mashahidi wa Yehova walio karibu nawe, au andikia wachapishaji wa gazeti hili kwa habari za mahali pa mkusanyiko palipo karibu nawe. Toleo la Februari 15, 1999 la gazeti-jenzi letu, Mnara wa Mlinzi, laorodhesha tarehe za mikusanyiko yote katika Burundi, Kongo (Kinshasa), Kenya, Rwanda, Tanzania, na Uganda.