Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g 8/07 uku. 5
  • Tumia Mamlaka Yako

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Tumia Mamlaka Yako
  • Amkeni!—2007
  • Habari Zinazolingana
  • Kumpendeza Yehova Kama Jamaa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Wazazi—Wazoezeni Watoto Wenu Kwa Upendo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Heshima kwa Mamlaka—Kwa Nini Ni Muhimu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
  • Kujenga Familia Yenye Nguvu Kiroho
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—2007
g 8/07 uku. 5

Hatua ya 3

Tumia Mamlaka Yako

Kwa nini hatua hii ni muhimu? Uchunguzi unaonyesha kwamba “watoto wanaolelewa na wazazi wanaotumia mamlaka yao ifaavyo, yaani wazazi wenye upendo lakini wanaoweka mipaka imara, hufanya vema shuleni, wana uhusiano mzuri na watu wengine, wanajiheshimu, na wana furaha kuliko watoto ambao wazazi wao huwaendekeza au ni wakali kupita kiasi,” linasema gazeti Parents.

Tatizo: Kuanzia utoto hadi ujanani, watoto watapinga mamlaka yako. “Watoto hutambua haraka ikiwa wazazi wanaogopa kutumia mamlaka yao na ni wakati gani wazazi watakubali chochote wanachoombwa,” anaandika John Rosemond, mwandishi wa kitabu Parent Power! “Kuhusu suala la ‘ni nani mwenye mamlaka,’ ikiwa wazazi hawatatumia mamlaka yao, basi watoto watawatawala,” anasema mwandishi huyo.

Suluhisho: Usihofu kwamba ukitumia mamlaka watoto wako watakuchukia au utawavunja moyo. Yehova Mungu, Mwanzilishi wa familia, hakukusudia watoto wawe na mamlaka ya kuamua jinsi familia itakavyoongozwa. Badala ya hivyo, yeye amewapa wazazi mamlaka na anawaamuru watoto hivi: “Watiini wazazi wenu.”—Waefeso 3:14, 15; 6:1-4.

Unaweza kutumia mamlaka yako bila kuwakandamiza watoto. Kwa njia gani? Kwa kumwiga Yehova. Ingawa ana uwezo wa kuwalazimisha watoto wake wa kibinadamu wafanye mapenzi yake, yeye hutumia sifa zetu nzuri kutuchochea kufanya hivyo. “Laiti ungesikiliza amri zangu! Ndipo amani yako ingekuwa kama mto,” linasema Neno lake. (Isaya 48:18) Yehova anataka tumtii, si kwa sababu tunamwogopa isivyofaa, lakini kwa sababu tunampenda. (1 Yohana 5:3) Yeye hatazamii tufanye mengi kuliko uwezo wetu na anajua tutafaidika tukiishi kupatana na viwango vyake vya maadili.—Zaburi 19:7-11.

Utapataje ujasiri wa kutumia mamlaka yako kwa usawaziko ukiwa mzazi? Kwanza, unapaswa kuamini kwamba Mungu anakutazamia utumie mamlaka yako. Pili, unapaswa kusadiki kwamba kuishi kupatana na viwango vya Mungu vya maadili kutakufaidi wewe na watoto wako pia.—Waroma 12:2.

Ni mambo gani hususa unayopaswa kufanya ili kutumia mamlaka yako?

[Blabu katika ukurasa wa 5]

“Watie nidhamu watoto wako, . . . nao wataufurahisha moyo wako.”—Methali 29:17, New Revised Standard Version

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki