Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g 10/07 uku. 27
  • “Mjionyeshe Kuwa Wenye Shukrani”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Mjionyeshe Kuwa Wenye Shukrani”
  • Amkeni!—2007
  • Habari Zinazolingana
  • “Jionyesheni Wenyewe Kuwa Wenye Shukrani”
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • “Toeni Shukrani Kuhusu Kila Jambo”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2019
  • “Mjionyeshe Kuwa Wenye Shukrani”
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • “Mjionyeshe Kuwa Wenye Shukrani”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—2007
g 10/07 uku. 27

“Mjionyeshe Kuwa Wenye Shukrani”

◼ Mara nyingi, Biblia inawatia moyo waabudu wa Mungu watoe shukrani. Zaburi 92:1 inasema: “Ni vema kumtolea Yehova shukrani.” Mtume Paulo pia alihimiza: “Mjionyeshe kuwa wenye shukrani.”—Wakolosai 3:15.

Kuna sababu nzuri za kuwa wenye shukrani. Profesa Robert Emmons wa Chuo Kikuu cha California huko Davis, anasema: “Utafiti kuhusu shukrani unadokeza kwamba kuwa na hisia za uthamini kuna uvutano mzuri kwa kuwasaidia watu washughulike na matatizo ya kila siku, hasa mfadhaiko, na kupata hisia ya kujiheshimu.”

Gazeti Time linataja jambo lingine pia: “Watu wanaosema kwamba wanahisi wana uthamini . . . wanakuwa na nguvu nyingi zaidi, mtazamo mzuri zaidi, hawana mfadhaiko mwingi, na hawashuki moyo mara nyingi wakilinganishwa na watu wengine kwa ujumla.”

Hata hivyo, inasikitisha kwamba Biblia ilitabiri kuwa “katika siku za mwisho” watu wengi wangekuwa “wenye kujipenda wenyewe” na “wasio na shukrani.” (2 Timotheo 3:1-5) Wakristo wa kweli wanaweza kuepukaje kuathiriwa na roho hiyo? Mtungaji wa Biblia anasema: “Mimi, Yehova, ni Mungu wako, Yeye anayekufundisha ili ujifaidi mwenyewe, Yeye anayekufanya uende katika njia unayopaswa kutembea ndani yake.” (Isaya 48:17) Kwa kutii sheria za Mungu, tunaepuka mateso yanayowapata watu wanaofuatilia mambo ya kibinafsi. Kwa kuongezea, tuna uhakika wa kwamba Yehova anaona jitihada zetu na atatuthawabisha. (Waebrania 6:10) Faida kama hizo zinatuchochea ‘tumtolee Yehova shukrani.’—Zaburi 107:8.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki