Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g 11/07 uku. 3
  • Je, Tuitegemee au Tusiitegemee?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Tuitegemee au Tusiitegemee?
  • Amkeni!—2007
  • Habari Zinazolingana
  • Kuwatumaini Wengine Ni Muhimu kwa Maisha Yenye Furaha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • Unaweza Kuwatumaini Ndugu Zako
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2022
  • Kutumaini au Kutotumaini
    Amkeni!—1996
  • Mkusanyiko Ambao Uliongeza Itibari Yetu Katika Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—2007
g 11/07 uku. 3

Je, Tuitegemee au Tusiitegemee?

“Usitumaini mbao zilizooza,” akaandika William Shakespeare, mwandishi wa tamthilia Mwingereza. Kwa kweli, kabla ya kukanyaga mbao za mashua, unapaswa kuhakikisha kwamba hazijaoza.

MANENO ya Shakespeare yanapatana na maneno ya Mfalme Sulemani mwenye hekima wa Israeli la kale ambaye aliandika hivi miaka 3,000 hivi iliyopita: “Mujinga anaamini kila neno: lakini mwenye akili anaangalia sana namna anavyokwenda.” (Methali 14:15, Zaire Swahili Bible) Naam, ni mjinga tu ambaye atakubali kila kitu anachosikia, akifanya maamuzi na kutenda kupatana na mashauri au mafundisho yasiyo na msingi. Kutegemea vitu visivyofaa, kama tu kukanyaga mbao zilizooza, kunaweza kutuletea msiba. Huenda ukajiuliza, ‘Je, kuna mwongozo wowote ambao kwa kweli tunaweza kuutegemea?’

Mamilioni ya watu ulimwenguni pote hutegemea kabisa kitabu kimoja cha kale. Kitabu hicho ni Biblia Takatifu. Wanategemea kitabu hicho kiongoze hatua zao. Maamuzi yao yanategemea mashauri ya kitabu hicho na matendo yao yanapatana na mafundisho yake. Je, watu hao wanakanyaga mbao zilizooza? Jibu la swali hilo linategemea sana jibu la swali lingine, Je, kuna sababu nzuri za kuitegemea Biblia? Toleo hili la pekee la Amkeni! linachunguza uthibitisho uliopo.

Toleo hili la Amkeni! halijakusudiwa kukulazimisha uwe na imani au maoni fulani ya kidini. Badala yake, limekusudiwa kuonyesha uthibitisho wenye nguvu ambao umewasadikisha mamilioni ya watu kwamba wanaweza kuitegemea Biblia. Baada ya kusoma makala zinazofuata, unaweza kujiamulia ikiwa unaweza kuitegemea Biblia.

Unapaswa kuchunguza habari hii kwa uzito. Kwa kweli, ikiwa Biblia ni chanzo chenye kutegemeka cha kupata mwongozo kutoka kwa Muumba wetu, basi utafaidika ikiwa wewe na wapendwa wako mtachunguza kile ambacho Biblia inasema.

Hata hivyo, acheni kwanza tutaje mambo fulani ya hakika kuhusu Biblia. Kwanza kabisa, Biblia ni kitabu cha pekee.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki