Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g 2/11 uku. 28
  • Je, Una Miradi Inayopatana na Akili?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Una Miradi Inayopatana na Akili?
  • Amkeni!—2011
  • Habari Zinazolingana
  • Kujitegemeza na Utimizo wa Maneno ya Yehova (Makala ya Funzo la Kitabu)
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Je, Mali Zaweza Kukufanya Uwe Mwenye Furaha?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Wapende Watu, Bali Si Pesa na Mali
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Maisha Yenye Kuridhisha Katika Ulimwengu Mpya wa Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—2011
g 2/11 uku. 28

Je, Una Miradi Inayopatana na Akili?

● Unataka kufanya nini maishani? Je, unatazamia mambo yanayopatana na akili, au unaota kuhusu mambo ambayo huwezi kutimiza? Mtu fulani aliyechunguza utu wa wanadamu alitoa ushauri huu wenye hekima: “Hayo nayo ni bure kabisa; ni sawa na kufukuza upepo. Afadhali kuridhika na ulicho nacho kuliko kuhangaika kwa kutamani kitu kingine.”—Mhubiri 6:9, Biblia Habari Njema.

Maneno “ulicho nacho” yanarejelea hali zetu na mambo halisi ya sasa. Kwa kweli, hakuna ubaya kujaribu kuboresha maisha yetu. Hata hivyo, jambo kuu ambalo Biblia inataja ni kwamba si jambo la hekima kufuatia miradi isiyopatana na akili. Huenda miradi hiyo ikawa umashuhuri, utajiri, mwenzi bora kabisa wa ndoa, au afya kamilifu.

Isitoshe, huenda wale ambao hufikia miradi mingine, kama vile utajiri, wakatamani kupata zaidi. Biblia inasema hivi waziwazi: “Anayependa fedha hatatosheka na fedha, wala anayependa mali hatatosheka na mapato. Hilo pia ni ubatili.” (Mhubiri 5:10) Kwa sababu hiyo, watu wenye hekima kiroho hujaribu kuridhika na kile ‘walicho nacho.’ Naam, wanatambua ukweli wa maneno haya: “Hatukuleta chochote katika ulimwengu, wala hatuwezi kuchukua chochote nje.”—1 Timotheo 6:7.

Wanadamu wameumbwa kwa njia ya kwamba wale wanaotosheleza mahitaji yao ya kiroho ndio wanaopata furaha nyingi zaidi. (Mathayo 5:3) Tunaweza kufanya hivyo kwa njia gani? Yesu Kristo alisema hivi: “Mwanadamu ataishi, si kwa mkate tu, bali kwa kila neno linalotoka katika kinywa cha Yehova.” (Mathayo 4:4) Maneno hayo yenye thamani yanapatikana katika Biblia, na mtu yeyote anaweza kufaidika nayo.

Maneno kama hayo yanapatikana katika Zaburi 37:4. Inasema hivi: “Upate furaha tele katika Yehova, naye atakupa maombi ya moyo wako.” Akiwa Mungu Mweza-Yote, Yehova atawapa waabudu wake waaminifu vitu ambavyo hakuna mwanadamu anaweza kuwapa: afya kamilifu, vitu vya kimwili, na uzima wa milele katika Paradiso duniani. (Luka 23:43; Ufunuo 21:3, 4) Inapatana na akili kuamini maneno hayo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki