Mazungumzo ya Familia
Kuna Kasoro Gani Katika Picha Hii?
Soma Matendo 9:36-41. Ni mambo gani matatu katika picha hii ambayo si sahihi? Andika majibu yako kwenye mistari iliyo hapa chini, na ukamilishe picha hii kwa kuipaka rangi.
1. ․․․․․
2. ․․․․․
3. ․․․․․
ZUNGUMZENI PAMOJA:
Tabitha anajulikana kwa jina gani lingine, na majina yake yanamaanisha nini?
DOKEZO: Soma sanduku kwenye ukurasa wa 67 wa kitabu “Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu.
Je, Tabitha alikuwa mtu mwenye ubinafsi? Eleza.
DOKEZO: Soma Matendo 9:36, 39.
Maneno ya Yesu yanayopatikana katika Luka 6:38 yalithibitika kuwa ya kweli jinsi gani katika kisa cha Tabitha? Unaweza kuiga mfano wake jinsi gani?
DOKEZO: Soma Waefeso 4:28; Yakobo 2:14-17.
UTENDAJI WA FAMILIA:
Kila mshiriki wa familia na afikirie kuhusu mtu ambaye angependa kumpa zawadi. Kisha atengeneze zawadi moja rahisi kwa ajili ya mtu huyo. Kwa mfano, unaweza kutengeneza kadi, au kifaa cha kuwekea alama katika kitabu na kuandika andiko fulani la Biblia juu yake.
Kusanya na Ujifunze
Kata, kunja katikati, na uhifadhi
KADI YA BIBLIA 7 PETRO
MASWALI
A. Kwa nini Petro alianza kuzama?
B. Je, habari hii ni kweli au si kweli? Petro alibaki akiwa mseja.
C. Viongozi wa kidini walipowaamuru mitume waache kuhubiri, Petro na mitume wale wengine walijibu na kusema: “Lazima . . . ”
[Chati]
4026 K.W.K. 1 W.K. 98 W.K.
Adamu aumbwa Aliishi katika Kitabu cha
karne ya mwisho cha
ya kwanza W.K. Biblia
kinaandikwa
[Ramani]
Aliishi Bethsaida na Kapernaumu
GALILAYA
Kapernaumu
Bethsaida
Bahari ya Galilaya
PETRO
MAMBO MACHACHE KUMHUSU
Mvuvi mwenye bidii sana ambaye baadaye alikuja kuwa mmoja wa wanafunzi wa kwanza wa Yesu. Yesu alimchagua Petro awe mmoja wa mitume wake 12. Maneno ya Petro katika zile Injili nne ni mengi kuliko ya mtume mwingine yeyote. Yehova alimtumia sana katika kazi ya kuhubiri na ‘kuwatia nguvu ndugu zake.’—Luka 22:32; Marko 3:13-19.
MAJIBU
A. Alikuwa na shaka.—Mathayo 14:28-31.
B. Si kweli.—Marko 1:29-31; Yohana 1:42; 1 Wakorintho 9:5.
C. “. . . tumtii Mungu kuwa mtawala kuliko wanadamu.”—Matendo 5:18, 27-29.
Watu na Nchi
4. Jina langu ni Antonia. Nina umri wa miaka minane, na ninaishi nchini Chile, huko Amerika Kusini. Kuna Mashahidi wangapi wa Yehova nchini Chile? Ni 69,500, 96,500, au 106,500?
5. Ni alama gani inayoonyesha eneo ninaloishi? Chora duara kuzunguka alama hiyo, na uchore alama nyingine kuonyesha eneo unaloishi kisha uone kwenu ni umbali gani kutoka Chile.
A
B
C
D
Watoto Watafute Picha
Je, unaweza kupata picha hizi katika toleo hili? Kwa maneno yako mwenyewe, eleza jambo linalotendeka katika kila picha.
● Majibu ya “MAZUNGUMZO YA FAMILIA” kwenye ukurasa wa 23
MAJIBU YA UKURASA WA 30 NA 31
1. Petro hakuwa amesimama alipokuwa akisali; alipiga magoti.
2. Wanawake (wajane) walimwonyesha Petro mavazi ambayo Tabitha aliwashonea, si vyombo vya udongo.
3. Petro alisali akiwa peke yake, hakukuwa na watu wengine chumbani.
4. 69,500.
5. B.