Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g 11/12 kur. 2-3
  • Unaweza Kufanikiwa!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Unaweza Kufanikiwa!
  • Amkeni!—2012
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Unawajali Wazazi Wasio na Wenzi wa Ndoa?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Msaada kwa Mzazi Asiye na Mwenzi wa Ndoa
    Amkeni!—2002
  • Idadi ya Familia za Mzazi Mmoja Inaongezeka
    Amkeni!—2002
  • Familia za Mzazi Mmoja Zaweza Kufanikiwa!
    Siri ya Furaha ya Familia
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—2012
g 11/12 kur. 2-3

Unaweza Kufanikiwa!

[Picha katika ukurasa wa 2 na 3]

“Mimi hufurahi sana binti zangu wawili wanaponikumbatia bila mimi kutazamia na kuniambia, ‘Tunakupenda, Mama.’”​—ANNA, MAMA ASIYE NA MWENZI, POLAND.

“Mara nyingi mimi hufurahi ninapoona watoto wangu wakinishukuru kwa mambo ninayowafanyia. Nyakati nyingine wao hunipa zawadi ndogo, kama vile picha waliyochora. Wanapofanya hivyo mimi huhisi kana kwamba jitihada zangu zote zimethaminiwa.”​—MASSIMO, BABA ASIYE NA MWENZI, ITALIA.

“Nyakati nyingine ninapohisi nimeshuka moyo, mmoja wa wana wangu hunikumbatia, na kunibusu, kisha ananiambia kwamba ananipenda sana.”​—YASMIN, MAMA ASIYE NA MWENZI, AFRIKA KUSINI.

HAYO ni baadhi ya mambo ambayo wazazi wengi wasio na wenzi walimwambia mwandishi wa Amkeni! katika uchunguzi uliofanywa sehemu mbalimbali ulimwenguni. Wazazi wengi wasio na wenzi, hasa akina mama, walisema kwamba walitamani kuwa na mwenzi mwenye upendo ambaye angewasaidia.a Hata hivyo, maelezo yao yaliyotolewa kwa unyoofu yanaonyesha pia kwamba wamefaulu kubadilikana kulingana na hali yao.

Ni nini ambacho kimewasaidia wazazi hao wasio na wenzi wabadilikane kulingana na hali na wafaulu kutimiza jukumu lao gumu? Katika makala zifuatazo, tutachunguza baadhi ya mapendekezo yao na maelezo yao ya unyoofu, na pia tutachunguza kanuni muhimu ambazo zimewasaidia. Ikiwa wewe ni mzazi asiye na mwenzi, tunatumaini kwamba makala hizi zitakusaidia ufanikiwe kutimiza jukumu lako gumu kwa shangwe na pia kwa njia inayoridhisha. Kwa kweli, hilo linaweza kuwa jambo gumu katika ulimwengu wa leo ulio na msukosuko na unaobadilika haraka.b

Makala hizi zitakazia fikira maeneo sita. Jinsi ambavyo wazazi wasio na wenzi wanaweza

  1. Kutafuta msaada kutoka kwa watu wengine

  2. Kuwasiliana kwa njia inayofaa zaidi na watoto wao

  3. Kutanguliza mambo yanayofaa

  4. Kuweka mipaka iliyo wazi kuhusu mwenendo

  5. Kufundisha maadili yanayofaa

  6. Kuhakikisha kwamba Mungu ni sehemu ya familia yao

a Ulimwenguni pote, wazazi wengi wasio na wenzi ni wanawake—jambo ambalo linaonyeshwa wazi katika mfululizo huu.

b Kanuni nyingi zilizotajwa katika mfululizo huu zinaweza pia kusaidia familia zilizo na wazazi wote wawili.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki