Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g 11/12 uku. 9
  • 5 Wafundishe Viwango Bora vya Maadili

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • 5 Wafundishe Viwango Bora vya Maadili
  • Amkeni!—2012
  • Habari Zinazolingana
  • Wazazi—Wazoezeni Watoto Wenu Kwa Upendo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Mzazi Mmoja, Matatizo Mengi
    Amkeni!—2002
  • Kuwalea Watoto Wako Wampende Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Wazazi—Wasaidieni Watoto Wenu Wampende Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2022
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—2012
g 11/12 uku. 9

5 Wafundishe Viwango Bora vya Maadili

[Picha katika ukurasa wa 9]

Wazazi wenye hekima huwafundisha watoto wao viwango bora vya maadili vinavyopatikana katika Biblia

“Mapema maishani, sikuishi kulingana na viwango vya Biblia na ilikuwa vigumu kwangu kuwafundisha watoto wangu. Lakini sasa ni rahisi kufanya hivyo kwa sababu nina msaada wa Biblia.”​—ELIZABETH, AFRIKA KUSINI.

Tatizo.

Kushinikizwa na marafiki shuleni na kuzorota kwa maadili ulimwenguni pote kunaathiri sana familia. Watoto wanahitaji viwango bora vya maadili ili kupinga uvutano huo mbaya. La sivyo, huenda hawatakuwa watu wazima wenye kutegemeka, wenye maadili yanayofaa, na wenye adabu.

Mapendekezo.

Wazazi wengi wasio na wenzi, kutia ndani wale walionukuliwa katika mfululizo huu, hutafuta mwongozo kutoka katika Biblia, kwa kuwa wanatambua kwamba ina hekima isiyo na kifani kutoka kwa Mungu. Kwa mfano, chunguza yale ambayo Biblia inasema kuhusu kanuni muhimu zaidi kuliko zote​—kuonyesha upendo wa kweli.

“Upendo ni wenye ustahimilivu na wenye fadhili. Upendo hauna wivu, haujigambi, haujivuni, haujiendeshi bila adabu, hautafuti faida zake wenyewe, hauchokozeki. Hauweki hesabu ya ubaya. Haushangilii juu ya ukosefu wa uadilifu, bali hushangilia pamoja na kweli. Huhimili mambo yote, . . . hutumaini mambo yote, huvumilia mambo yote. Upendo haushindwi kamwe.”​—1 Wakorintho 13:4-8.

Wazazi wanapoonyesha upendo wa aina hiyo, watoto wao hufaulu kutokeza sifa nzuri. Colette, aliyetajwa awali, anayeishi Ufaransa, aliandika hivi: “Mara nyingi niliwaambia watoto wangu kwamba ninawapenda. Pia niliwaambia kwamba wao ni zawadi kutoka kwa Mungu na kwa sababu hiyo walihitaji kutunzwa vizuri. Kwa upande wao, walipaswa kuwa wenye adabu na kuniheshimu mimi na baba yao [ambaye hakuwa na haki kisheria ya kuwalea]. Kanuni hizo zimefanya tuaminiane na kuheshimiana.”​—Zaburi 127:3.

Anna, anayeishi nchini Poland, aliandika hivi: “Watoto wangu wanapogombana, mimi huwakumbusha maneno ya Yesu kwamba mambo tunayotaka watu watutendee, tunapaswa kuwatendea vivyo hivyo.” (Mathayo 7:12) Roberto, aliyetajwa hapo awali, anakabiliana na tatizo ambalo huwakumba wazazi wengi wasio na mwenzi. Anasema: “Watoto wanakabili viwango vya aina mbili​—vyako na vya yule mzazi mwingine. Ninaposisitiza kwamba lazima watii viwango vya Biblia, ninajua kwamba wakati huo wanamwona yule mzazi mwingine kuwa mzuri kuliko mimi.” Zaidi ya hayo, anasema: “Huenda yule mzazi mwingine akawapa watoto zawadi ili wampende. Ni vigumu kukabiliana na hali kama hiyo, lakini kuwasiliana kwa njia nzuri na watoto kunasaidia.”

Si rahisi sikuzote kuishi kupatana na viwango vya Biblia, lakini unapofanikiwa unafurahia jitihada zako! Sarah, mzazi asiye na mwenzi anayeishi Afrika Kusini anasema: “Ninafurahi kwamba watoto wangu wamelelewa kwa mwongozo wa Yehova. Ni kweli kwamba tumekuwa na matatizo, lakini sikuzote Mungu ametusaidia.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki