Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g 11/12 uku. 10
  • 6 Mwombe Mungu Msaada

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • 6 Mwombe Mungu Msaada
  • Amkeni!—2012
  • Habari Zinazolingana
  • Unapaswa Kusali kwa Njia Gani ili Mungu Akusikilize?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2021
  • Familia za Mzazi Mmoja Zaweza Kufanikiwa!
    Siri ya Furaha ya Familia
  • Zawadi ya Sala
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Mkaribie Mungu Kupitia Sala
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—2012
g 11/12 uku. 10

6 Mwombe Mungu Msaada

[Picha katika ukurasa wa 10]

Je, unamwomba Mungu akusaidie kulea watoto wako?

“Mume wangu aliponiacha mimi na watoto, nilimsihi Mungu atusaidie. Alijibu sala yangu. Hatujawahi kukosa mahitaji yetu. Ametusaidia na kutuongoza.”​—MAKI, JAPANI

KATIKA ulimwengu wa leo unaopenda vitu vya kimwili, watu kwa ujumla hawamfikirii Mungu. Hata hivyo, Muumba wetu anapendezwa na sisi na anataka tufanikiwe maishani. Andiko la Isaya 41:10 linaeleza vizuri hisia zake: “Usiogope, kwa maana mimi nipo pamoja nawe. . . . Nitakusaidia kwelikweli.”

Katika makala iliyotangulia, tulizungumzia jinsi Mungu anavyotusaidia kupitia viwango bora vya maadili vinavyopatikana katika Biblia. (2 Timotheo 3:16) Lakini Biblia si kitabu kinachotoa tu mwongozo. Kinatufunulia pia sifa zenye kupendeza za Mungu na kutuonyesha kwamba anatupenda. Kwa hiyo, wazazi wengi Wakristo—iwe wana wenzi au hawana—wametambua kwamba tunapofuata mafundisho ya Biblia, tunaona wema wa Mungu.

Robert, Austria: “Yehova Mungu ndiye baba au mama bora kuliko yeyote kati yetu. Anajua mahitaji ya watoto wetu, na anajua jinsi ya kuwalinda. Kwa hiyo, mimi husali kwake mara nyingi nikiwa na binti yangu.”

Ayusa, Japani: “Mimi hufurahi sana ninapomwona mwana wangu akiwa na uhakika kwamba Yehova atatutegemeza anaposema, ‘Yehova yuko pamoja nasi, kwa hiyo kila kitu kitakuwa shwari.’”

Cristina, Italia: “Ninapoona kwamba siwezi kutatua tatizo fulani, mimi husali kwa Yehova, na kuliacha mikononi mwake. Mara moja mimi huwa na amani ya akili kwa kuwa ninajua kwamba tatizo hilo litatatuliwa kwa njia inayofaa kabisa.”

Laurentine, Ufaransa: “Ninaweza kuthibitisha kwamba Yehova amenibariki nikiwa mzazi asiye na mwenzi. Kwa kweli yeye huwaokoa wanaoteseka na wasio na baba au mama.”

Keiko, Japani: “Mungu hana ubaguzi. Anataka kutunza familia zote kwa upendo, iwe zina wazazi wawili au mzazi mmoja.”​—Matendo 10:34.

Akionyesha kwamba Mungu anatuonyesha huruma na kutuhangaikia, Yesu Kristo alisema: “Njooni kwangu, nyote mnaotaabika na kulemewa na mizigo, nami nitawaburudisha ninyi . . . , kwa maana mimi ni mwenye tabia-pole na mnyenyekevu moyoni, nanyi mtapata burudisho kwa ajili ya nafsi zenu.” (Mathayo 11:28-30) Kwa kweli, Yesu pamoja ya Baba yake wa mbinguni, Yehova Mungu, wanataka tuhisi tukiwa salama chini ya utunzaji wao wenye upendo. Tunasoma hivi kwenye Zaburi 34:8: “Onjeni mwone ya kuwa Yehova ni mwema.” Ndiyo, Mungu anataka ujionee mwenyewe kwamba mashauri yake hufanya kazi, kwamba anataka ufanikiwe maishani. Je, utakubali mwaliko wake?

Nilichochewa Sana na Mfano wa Mama

Hata iwe alikuwa na shughuli nyingi au alikuwa amechoka kiasi gani, sikuzote mama yangu aliacha alichokuwa akifanya na kuja kitandani mwangu ili kusali pamoja nami. Sala zake zilifanya nitambue kwamba kweli ninaweza kuwa rafiki ya Yehova Mungu.​—Amanda, Marekani.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki