Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g 5/13 kur. 12-13
  • Koreshi Mkuu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Koreshi Mkuu
  • Amkeni!—2013
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • JINSI KORESHI ALIVYOTEKA BABILONI
  • UNABII WENYE KUSHANGAZA
  • KUKOMBOLEWA KIMUUJIZA
  • KWA NINI HABARI HII IKUPENDEZE?
  • Watu wa Mungu Wanatoka Babeli
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Kitabu Kinachotegemeka—Sehemu ya 4
    Amkeni!—2011
  • Yehova—“Mungu Mwenye Haki, Mwokozi”
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
  • Mtumaini Yehova—Si “Mpango wa Hila!”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—2013
g 5/13 kur. 12-13
Picha katika ukurasa wa 12]

Kaburi la Koreshi

TUNAYOJIFUNZA KUTOKANA NA HISTORIA

Koreshi Mkuu

Kulingana na kalenda ya kisasa, usiku wa Oktoba 5/6, 539 K.W.K., jambo lililoonekana kuwa haliwezekani lilitendeka katika jiji la Babiloni, mji mkuu wa Milki ya Babiloni. Katika usiku huo wenye matukio muhimu, jiji hilo lilipinduliwa na jeshi la Wamedi na Waajemi, likiongozwa na Mfalme Koreshi Mwajemi, ambaye pia anaitwa Koreshi Mkuu. Mbinu aliyotumia ilikuwa ya werevu sana.

JINSI KORESHI ALIVYOTEKA BABILONI

“Koreshi alipoamua kulishambulia Babiloni, tayari lilikuwa jiji lililotukuka zaidi kati ya majiji ya Mashariki ya Kati—labda hata kati ya majiji yote ulimwenguni,” kinasema kitabu Ancient World Leaders—Cyrus the Great. Mto Efrati ulipitia Babiloni na pia maji ya mto huo yalijaa kwenye mahandaki yaliyozunguka kuta kubwa za jiji hilo—na hilo lilifanyiza mfumo wa ulinzi uliofanya jiji hilo lionekane kuwa haliwezi kushindwa.

Wanaume wa Koreshi walibadili mkondo wa mto huo umbali fulani kabla ya kufika Babiloni na hivyo kufanya kiwango cha maji katika jiji hilo kupungua. Kisha wanajeshi wakapita ndani ya mto huo na kufika kwenye malango ya jiji, yaliyokuwa yameachwa wazi, na kuliteka Babiloni bila upinzani mkubwa. Kulingana na wanahistoria Wagiriki Herodoto na Xenophon, usiku walioshambuliwa, Wababiloni walijihisi wakiwa salama nyuma ya mfumo wa ulinzi wa jiji lao, na hata wengi wao walikuwa katika karamu, kutia ndani mfalme! (Ona sanduku lenye kichwa “Maandishi ya Mkono Yako Ukutani.”) Isitoshe, mashambulizi ya Koreshi yalitimiza unabii wa Biblia wenye kushangaza.

Biblia ilitabiri ushindi wa Koreshi dhidi ya Babiloni

UNABII WENYE KUSHANGAZA

Unabii huu mbalimbali wa Isaya ni wenye kushangaza sana kwa kuwa uliandikwa miaka 200 hivi kabla ya wakati ulipotimia—huenda miaka 150 hivi kabla ya Koreshi kuzaliwa! Fikiria yafuatayo:

  • Mwanamume anayeitwa Koreshi angeshinda Babiloni na kuwakomboa Wayahudi.—Isaya 44:28; 45:1.

  • Mto Efrati ungekaushwa, na hivyo kuruhusu jeshi la Koreshi lipite.—Isaya 44:27.

  • Malango ya jiji yangeachwa wazi.—Isaya 45:1.

  • Jeshi la Wababiloni ‘lingeacha kupigana.’—Yeremia 51:30; Isaya 13:1, 7.

KUKOMBOLEWA KIMUUJIZA

Mapema, katika mwaka wa 607 K.W.K., majeshi ya Babiloni yaliteketeza jiji la Yerusalemu na kuwapeleka waokokaji wengi uhamishoni. Wayahudi wangekuwa mateka kwa muda mrefu kadiri gani? Mungu alisema hivi: “Miaka 70 itakapotimia nitatoza hesabu juu ya mfalme wa Babiloni na juu ya taifa lake . . . nami nitaifanya kuwa mahame yenye ukiwa mpaka wakati usio na kipimo.”—Yeremia 25:12.

Kama ilivyotajwa, Koreshi aliliteka Babiloni mnamo 539 K.W.K. Muda mfupi baada ya hapo, aliwaachilia Wayahudi, na baadhi yao waliwasili nyumbani kwao mnamo 537 K.W.K.—miaka 70 kamili baada ya uhamisho wao. (Ezra 1:1-4) Mwishowe, Babiloni likawa “mahame yenye ukiwa”—na hivyo kuthibitisha tena usahihi wa unabii wa Biblia.

KWA NINI HABARI HII IKUPENDEZE?

Fikiria hili: Biblia ilitabiri (1) Wayahudi wangepelekwa uhamishoni kwa miaka 70, (2) ushindi wa Koreshi dhidi ya Babiloni na mbinu muhimu ambazo angetumia, na (3) ukiwa wa Babiloni ambao ungetukia baadaye. Ujuzi kama huo wa mapema haungeweza kutoka kwa wanadamu! Mkataa unaopatana na akili zaidi ni huu: “Unabii haukuletwa wakati wowote kwa mapenzi ya mwanadamu, bali wanadamu walisema yaliyotoka kwa Mungu.” (2 Petro 1:21) Kwa kweli, tunapaswa kuichunguza Biblia.

TAARIFA FUPI

  • Inaaminiwa kwamba Koreshi alizaliwa karibu na mwaka wa 600 K.W.K. Alikufa katika vita mwaka wa 530 K.W.K. hivi.

  • Kaburi la Koreshi bado liko kule Pasargadae, jiji la Uajemi ya kale ambalo lilianzishwa na Koreshi na ambalo sasa ni eneo lililotengwa kwa ajili ya kuchimbuliwa kwa vitu vya kale nchini Iran.

  • [Picha katika ukurasa wa 12]

    The Cyrus Cylinder

    Mwanzi wa Koreshi, ambao ni bamba la udongo lenye urefu wa sentimita 23 lina maandishi yanayoonyesha ushindi wa Koreshi dhidi ya Babiloni na kuachiliwa huru kwa mateka, kutia ndani Wayahudi. Mwanzi huo umesemekana kuwa “mojawapo ya ugunduzi muhimu zaidi kati ya vitu vya kale vya Biblia vilivyochimbuliwa.”

  • Waajemi bado wanamheshimu sana Koreshi.

“MAANDISHI YA MKONO YAKO UKUTANI”

[Picha]

Usiku ambao Koreshi alishambulia Babiloni kwa ghafula, Mfalme Belshaza wa Babiloni alikuwa katika karamu pamoja na “wakuu wake elfu” wakati ambapo mkono ulipojitokeza kimuujiza. Mkono huo uliandika hivi mbele yao wote, “MENE, MENE, TEKELI na PARSINI” juu ya lipu ya ukuta wa jumba la mfalme.a—Danieli 5:1, 5, 25.

Huku Belshaza akiwa ameogopa sana, nabii Danieli alimtafsiria maana ya fumbo hilo. Kwa ufupi, Danieli alimwambia mfalme huyo kwamba ufalme wake ulikuwa ‘umekomeshwa,’ na kwamba alikuwa ‘amepimwa katika mizani’ na kuonekana kuwa amepungukiwa, na kwamba Babiloni lilikuwa ‘limepewa Wamedi na Waajemi.’ (Danieli 5:26-28) Maneno hayo yote yalitimia. Isitoshe, katika lugha nyingi leo, msemo “Maandishi ya mkono yako ukutani” unamaanisha kwamba msiba, au ushinde, unakaribia.

a Maneno hayo yanarejelea kipimo cha uzito wa pesa. Kwa maelezo zaidi, ona sura ya 7 ya kitabu Sikiliza Unabii wa Danieli! kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki