Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g 11/13 uku. 16
  • Je, Wewe “Huwa na Karamu Siku Zote”?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Wewe “Huwa na Karamu Siku Zote”?
  • Amkeni!—2013
  • Habari Zinazolingana
  • Mathayo 6:34—“Msihangaike Kamwe Kuhusu Kesho”
    Mistari ya Biblia Yafafanuliwa
  • Ishi Ukifikiria ya Kesho
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • 4 | Linda Tumaini Lako
    Amkeni!—2022
  • Biblia Inaweza Kukusaidia Upate Shangwe
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—2013
g 11/13 uku. 16

Je, Wewe “Huwa na Karamu Sikuzote”?

“Siku zote za mwenye kuteseka ni mbaya, lakini mtu aliye mchangamfu moyoni huwa na karamu sikuzote.”​—Methali 15:15.

MANENO hayo yanamaanisha nini? Yanarejelea hali ya akili na kihisia ya mtu. “Mwenye kuteseka” hufikiria sana kuhusu mambo mabaya​—mtazamo unaofanya siku zake ziwe “mbaya” au zenye kuhuzunisha. Tofauti na hilo, mtu “aliye mchangamfu moyoni” hujaribu kukazia fikira mambo mazuri​—mtazamo unaochochea shangwe ya moyoni, ukimfanya awe na “karamu sikuzote.”

Sisi sote tuna matatizo yanayoweza kutunyang’anya furaha yetu kwa kadiri fulani. Hata hivyo, tunaweza kufanya mambo fulani yatakayotusaidia kudumisha shangwe yetu tunapokumbwa na matatizo. Ona Biblia inasema nini.

  • Usiruhusu mahangaiko ya kesho yakulemee leo. Yesu Kristo alisema hivi: “Msiwe na wasiwasi juu ya kesho; kesho inayo yake. Matatizo ya siku moja yanawatosheni kwa siku hiyo.”​—Mathayo 6:34, Biblia Habari Njema.

  • Jaribu kukazia fikira mambo mazuri yanayokupata. Unaposhuka moyo, kwa nini usijikumbushe mambo hayo mazuri na kutafakari kuyahusu? Pia, usikazie fikira makosa au mambo mabaya uliyofanya zamani. Jifunze kutokana nayo, na usonge mbele. Uwe kama dereva ambaye mara kwa mara hutumia kioo cha kuangalia nyuma lakini hakazii fikira kioo hicho. Pia, kumbuka kwamba kwa “[Mungu] kuna msamaha wa kweli.”​—Zaburi 130:4.

  • Unapolemewa na mahangaiko, mweleze mtu anayeweza kukutia moyo. “Hangaiko” huufanya moyo wetu “uiname, lakini neno jema huufanya ushangilie,” inasema Methali 12:25. “Neno [hilo] jema” linaweza kutoka kwa mtu wa familia au rafiki anayetumainiwa​​—mtu ambaye hachambui-chambui au hana mtazamo mbaya bali “anapenda nyakati zote.”​—Methali 17:17.

Maneno yenye hekima yanayopatikana katika Biblia yamewasaidia wengi kupata shangwe zaidi maishani mwao, hata wanapokabili magumu. Maneno hayo yenye thamani na yakusaidie wewe pia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki