Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ijwbv makala 4
  • Mathayo 6:34—“Msihangaike Kamwe Kuhusu Kesho”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mathayo 6:34—“Msihangaike Kamwe Kuhusu Kesho”
  • Mistari ya Biblia Yafafanuliwa
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Maana ya Mathayo 6:34
  • Muktadha wa Mathayo 6:34
  • Ishi Ukifikiria ya Kesho
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Usihangaike
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2016
  • Ninaweza Kukabilianaje na Mahangaiko?
    Vijana Huuliza
  • Ninawezaje Kuacha Kuwa na Wasiwasi Mwingi Mno?
    Amkeni!—2001
Pata Habari Zaidi
Mistari ya Biblia Yafafanuliwa
ijwbv makala 4

MISTARI YA BIBLIA YAFAFANULIWA

Mathayo 6:34—“Msihangaike Kamwe Kuhusu Kesho”

“Msihangaike kamwe kuhusu kesho, kwa maana kesho itakuwa na mahangaiko yake yenyewe. Kila siku ina matatizo yake ya kutosha.”—Mathayo 6:34, Tafsiri ya Ulimwengu Mpya.

“Msiwe na wasiwasi juu ya kesho; kesho inayo yake. Matatizo ya siku moja yanawatosheni kwa siku hiyo.”—Mathayo 6:34, Biblia Habari Njema.

Maana ya Mathayo 6:34

Yesu aliposema maneno hayo alikuwa akiwahakikishia wasikilizaji wake kwamba hawakuhitaji kuwa na wasiwasi kupita kiasi kuhusu matatizo ya wakati ujao. Badala yake, ingekuwa afadhali kushughulikia matatizo maishani siku moja baada ya nyingine.

Yesu hakumaanisha kwamba tunapaswa kuepuka kufikiria kuhusu kesho au tusipange kwa ajili ya mambo ya wakati ujao. (Methali 21:5) Badala yake alikuwa akitusaidia tusiwe na wasiwasi, au mahangaiko, kupita kiasi, kuhusu mambo ambayo huenda yakatokea kesho. Mahangaiko kama hayo yanaweza kutunyima shangwe na kutukengeusha tusikazie fikira mambo tunayopaswa kufanya sasa. Hatuwezi kutatua matatizo ya wakati ujao kwa kuwa na wasiwasi sasa. Na mara nyingi mambo ambayo tunahangaishwa nayo hayatokei au hayawi mabaya kama tulivyofikiria.

Muktadha wa Mathayo 6:34

Maneno hayo ya Yesu ni sehemu ya Mahubiri yake ya Mlimani yanayojulikana sana, yaliyo kwenye Mathayo sura ya 5-7. Katika mahubiri hayo, Yesu alisema kwamba kuwa na wasiwasi hakuboreshi wala kuongeza uhai wetu. (Mathayo 6:27) Pia alisema kwamba tunapomtanguliza Mungu maishani mwetu, hatuhitaji kuwa na wasiwasi kupitia kiasi kuhusu kesho. Mungu anajali mimea na wanyama, naye sikuzote atawatunza wale wanaomjali.—Mathayo 6:25, 26, 28-33.

Soma Mathayo sura ya 6 pamoja na maelezo ya chini, marejeo ya pambizoni, na picha.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki